Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari
Juma Linaloanza Januari 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Maelezo kuhusu ripoti ya utumishi ya Septemba ya nchi na ya kutaniko la kwenu.
Dak. 20: Wakati wa Kufanya Upya Kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia. Mzee mwenye kustahili azungumza umaana wa kujaza kadi kikamili na kuibeba nyakati zote. Hati hii hukusemea unapokuwa huwezi kujisemea wakati wa dharura. (Linganisha Mithali 22:3.) Kadi mpya yahitaji kujazwa kila mwaka ili kutoa julisho rasmi la kukataa damu, kwa kuwa madaktari fulani na wengine wamedai kwamba hati zilizopitisha mwaka mmoja na zaidi huenda zisionyeshe usadikisho wa mtu wa karibuni. Baada ya mkutano, watangazaji wote waliobatizwa watapewa kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia, na wale walio na watoto wadogo wasiobatizwa watapokea Kadi ya Utambulishi kwa kila mtoto. Eleza kwamba kadi hizi hazijazwi kwenye mkutano huo. Zapaswa kujazwa kwa uangalifu nyumbani lakini HAZIPASWI kutiwa sahihi. Kutia sahihi, kushuhudia, na kuandika tarehe kutafanywa katika Funzo la Kitabu la Kutaniko litakalofuata, chini ya usimamizi wa kiongozi wa funzo la kitabu. Ataangalia kuona kwamba wote walio katika kikundi chake walipokea kadi na wana usaidizi unaohitajiwa. Wale wanaotia sahihi wakiwa mashahidi kwa hakika wapaswa kuona mwenye kadi akitia sahihi hati hiyo. Mtu yeyote asiyekuwako wakati huo atasaidiwa na viongozi/wazee kwenye Mkutano wa Utumishi unaofuata hadi watangazaji wote waliobatizwa wawe wamejaza kadi zao vizuri na kutia sahihi. (Pitia barua ya Oktoba 15, 1991.) Kwa kugeuza usemi ulio katika kadi hii kulingana na hali zao na masadikisho yao wenyewe, watangazaji wasiobatizwa wanaweza kuandika mwelekezo wao wenyewe wa kutumia na wa watoto wao. Kuwa na ufahamu wenye kina katika kutunza mambo haya muhimu kutatustahilisha mema kutoka kwa Yehova.—Mit. 16:20.
Dak. 15: “Wenye Sifa za Kustahili na Kuandaliwa Vifaa ili Kufundisha Wengine.” (Mafungu 1-6) Toa maelezo mafupi juu ya mafungu 1-2, ukikazia uhitaji wa sisi kuwa na uhakika kwamba kwa msaada wa Yehova twaweza kufundisha wengine kwa matokeo. Panga watangazaji wanne watoe wonyesho wa utoaji mbalimbali katika mafungu 3-6, kila wawili-wawili wakionyesha jinsi ya kufanya ziara ya kwanza na ya kurudia.
Wimbo 14 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 13
Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Kazia mambo ya kuzungumzia katika magazeti ya karibuni. Toa madokezo ya jinsi ya kujijulisha tunapowafikia watu ili tuwatolee ushahidi kivivi hivi. Alika wasikilizaji wasimulie maneno ya kwanza ambayo wametumia wanaposema na wengine kwenye maduka, barabarani, bustanini, katika usafiri wa umma, na kadhalika. Eleza mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.
Dak. 15: “Wenye Sifa za Kustahili na Kuandaliwa Vifaa ili Kufundisha Wengine.” (Mafungu 7-9) Simulia jambo lililoonwa kuhusu kufanya ziara za kurudia lipatikanalo katika Kitabu-Mwaka cha 1995 (Kiingereza) ukurasa 45, kukazia umaana wa kufuatia kupendezwa kokote kunakopatikana. Panga mtangazaji mwenye sifa ya kustahili atoe wonyesho wa utoaji mbalimbali katika mafungu 7-8. Ingawa vichapo vingine vyatolewa ziara ya kwanza, twapaswa kukazia jitihada zetu hatimaye katika kuongoza mafunzo katika kitabu Ujuzi. Tia moyo wote waratibu wakati fulani wakati wa juma linalokuja ili wafanye ziara za kurudia.
Dak. 17: Epuka Uulimwengu Katika Karamu za Arusi. Hotuba itolewe na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi, la Septemba 15, 1984, kurasa 8-9, 13-17.
Wimbo 15 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 20
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Watu wa Namna Zote Wataokolewa.” Maswali na majibu. Alika wasikilizaji wasimulie mambo kadhaa yaliyoonwa ya kuonyesha jinsi walivyopata itikio zuri kutoka watu wanaotoka katika namna zote za maisha.
Dak. 20: Kutoa Ushahidi kwa Mwenendo Mzuri. Mzee ana mazungumzo pamoja na vijana wawili au watatu. Mazungumzo yategemea Mnara wa Mlinzi, la Agosti 15, 1987, kurasa 10-20. Tia ndani mambo yaliyoonwa yenye kuchapishwa na vilevile mambo yoyote yaliyoonwa ya kwenu yanayoonyesha jinsi ambavyo watazamaji wamevutiwa na mwenendo mnyoofu wa vijana Wakristo.
Wimbo 23 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 27
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 10: Kupitia Sanduku la Swali kukifanywa na mwandishi.
Dak. 15: “‘Twalihubiri Neno.’” Maswali na majibu. Tia maelezo kadhaa ya kuonyesha sababu kwa nini twathamini sana thamani ya Neno la Mungu.—Ona Amkeni!, Machi 22, 1984, kurasa 9-11, la Kiingereza.
Dak. 15:Pitia Toleo la Fasihi la Februari. Onyesha sehemu zenye kupendeza za kitabu, kama vile: (1) Vichwa vya sura vyenye kutokeza, (2) picha zenye kupendeza, (3) masanduku na chati za kufundisha, na (4) maswali yenye kuamsha kufikiri yaliyochapwa. Kwa kupatana na sehemu yenye kutangulia ya mkutano, tia moyo utumizi wa andiko lililochaguliwa vizuri katika utoaji. Uwe na wonyesho mmoja au mawili mafupi. Kumbusha wote wachukue vitabu vya kutumia juma hili.
Wimbo 26 na sala ya kumalizia.