Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/97 uku. 2
  • Kwa Nini Wao Hufanya Hivyo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Wao Hufanya Hivyo?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Baraka za Huduma ya Painia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Mapainia Hutoa na Kupokea Baraka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Sasa Ndio Wakati wa Kuhubiri!
    Huduma ya Ufalme—2005
  • “Wewe Ungekuwa Painia Mzuri!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 4/97 uku. 2

Kwa Nini Wao Hufanya Hivyo?

1 Ilitabiriwa juu ya Kristo kwamba ‘wivu wa nyumba ya Mungu ungemla.’ (Zab. 69:9) Bidii ya Yesu kwa ibada ya kweli ya Yehova ulimsukuma aweke huduma kwanza. (Luka 4:43; Yn. 18:37) Bidii hiyohiyo ya kutoa ushahidi kwa ile kweli inaonyeshwa leo katika huduma ya Mashahidi wa Yehova. Mwaka wa utumishi uliopita, wastani wa 645,509 ulimwenguni pote walishiriki katika namna fulani ya utumishi wa painia kila mwezi. Kwa sababu ya wakfu wetu kwa Mungu, kila mmoja wetu apaswa kufikiria kwa sala kama twaweza kupanga hali zetu ili tutumikie tukiwa mapainia-wasaidizi au wa kawaida.—Zab. 110:3; Mhu. 12:1; Rom. 12:1.

2 Kuishi katika mfumo wa mambo ambao ni wenye ubinafsi katika kufuatia vitu vya kimwili, wengi ulimwenguni huona ikiwa vigumu kuelewa kwa nini mtu yeyote angejitahidi sana katika huduma kwa kusudi ambalo halileti faida za kifedha na utukufu wowote. Kwa nini mapainia hufanya hivyo? Wanajua kwamba wanashiriki katika kazi ya kuokoa uhai. Wakichochewa na upendo mwingi kwa Yehova na wanadamu wenzao, wanahisi wakiwa na wajibu wenye nguvu, wa kibinafsi wa kusaidia kuokoa uhai. (Rom. 1:14-16; 1 Tim. 2:4; 4:16) Wenzi mapainia waliooana walijibu hivi ifaavyo: “Kwa nini tunafanya upainia? Je, tungeweza kumjibu Yehova kwa nini hatukufanya upainia?”

3 Dada mwingine aliandika hivi juu ya uamuzi wake wa kuanza upainia: “Mume wangu nami tulipanga kuishi kwa mshahara mmoja, ambao ulimaanisha kuishi bila vitu vyote visivyo vya lazima. Hata hivyo, Yehova alitubariki sana, bila kutuacha kamwe tuwe maskini au wenye uhitaji. . . . Nimepata sababu halisi ya kuishi—ile ya kusaidia wenye uhitaji wapate kujua kwamba Yehova, Mungu wa kweli, hayuko mbali na wale wanaomtafuta.” Wakiona uharaka wa nyakati, mapainia wanaridhika na mahitaji ya lazima ya maisha wanapotafuta kwa bidii kujipatia hazina za kiroho zitakazodumu milele.—1 Tim. 6:8, 18, 19.

4 Hali zako za kibinafsi zikiruhusu, kwa nini usijiunge na mamia ya maelfu ya ndugu na dada zako ulimwenguni pote wanaopainia? Kwa njia hiyo unaweza kuona shangwe kama yao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki