Habari Za Kitheokrasi
Mikusanyiko: Mikusanyiko ya wilaya ya 1996 ilimalizika kwa mafanikio katika nchi zote kukiwa na vilele vifuatavyo:
Hudhurio Ubatizo
Kenya: 22,000 775
Rwanda: 6,993 318
Tanzania: 11,976 336
Uganda: 3,294 162
Tunapojitahidi kutumia shauri na mambo tuliyojifunza katika mfululizo huu wa mikusanyiko, twatazamia mbele kwa hamu “Imani Katika Neno la Mungu” Mikusanyiko ya Wilaya ya 1997.
Ujenzi wa Ofisi ya Tawi: Kufikia wakati mtakapopokea toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu, kazi kubwa yote ya ujenzi itakuwa imekamilishwa isipokuwa labda Jumba la Ufalme jipya. Yamkini kazi fulani itakuwa inaendelea ya kuweka mfumo wa simu na lifti mbili. Kazi ya kumalizia bado itabaki kukamilishwa. Inatazamiwa kwamba mradi wote utamalizika Julai hivi. Twathamini utegemezo mzuri wa kifedha na njia nyingine ambayo wengi wametegemeza mradi huu. Yehova na aendelee kubariki roho mnayoonyesha.