Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/97 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Mei 5
  • Juma Linaloanza Mei 12
  • Juma Linaloanza Mei 19
  • Juma Linaloanza Mei 26
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 5/97 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei

Juma Linaloanza Mei 5

Wimbo 130

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 12: “Mfuate Yesu kwa Kuendelea.” Maswali kwa majibu. Tia ndani mambo yaliyoonwa kutoka Mnara wa Mlinzi la Juni 1, 1993, ukurasa wa 12.

Dak. 23: “Onyesha Hangaiko la Kweli kwa Kupendezwa Kote Kunakopatikana.” Mazungumzo na wasikilizaji. Kazia uhitaji wa kusitawisha kupendezwa kote. Dokeza baadhi ya njia za busara za kuomba anwani ya nyumbani ya wale tunaokuta mahali pa umma ili tuweze kuwatolea ushahidi zaidi. Panga watangazaji wenye uwezo watoe maonyesho mawili kati ya utoaji mbalimbali uliodokezwa katika fungu la 6-9. Pitia sanduku, “Jinsi ya Kuwa Mwenye Mafanikio Katika Kufanya Ziara za Kurudia,” kwenye ukurasa wa 3 katika nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1997. Tia moyo wote waratibu wakati fulani kila juma kufanya ziara za kurudia.

Wimbo 151 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 12

Wimbo 133

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.

Dak. 15: “Onyesha Hangaiko la Kweli kwa Kupendezwa Kote Kunakopatikana.” Pitia na utoe wonyesho kuhusu fungu la 10 la makala hiyo. Panga mtangazaji mwenye uzoefu aonyeshe jinsi ya kufanya mpito kutoka broshua Anataka hadi kitabu Ujuzi labda kwa kusema hivi: “Baada ya kujifunza habari kadhaa katika broshua hii Mungu Anataka Tufanye Nini, naweza kuona kwamba kwa kweli unapendezwa na unajali kufanya yale yanayopendeza machoni pa Mungu. Thamani ya kujifunza yote tuwezayo juu ya Mungu inakaziwa katika mstari huu kwenye Yohana 17:3. (Soma na ulizungumzie.) Hivyo twaweza kuona uhitaji wa kutwaa ujuzi zaidi ulioongezwa juu ya Mungu ambao kitabu hiki kitaandaa.” Toa kitabu Ujuzi ukirejezea kwenye picha na habari iliyo kwenye ukurasa wa 4 na 5. Onyesha kwamba njia ya kujifunza ni kama ile ya broshua. Panga muanzie sura ya kwanza kwenye ziara itakayofuata. Tia moyo kuhamisha mafunzo kwenye kitabu Ujuzi upesi iwezekanavyo, ikitegemea uwezo wa mwanafunzi.

Wimbo 162 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 19

Wimbo 139

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Chunguzeni andiko la leo. Pitia mipango ya utumishi wa shambani ya juma.

Dak. 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Nyumbani Yenye Maendeleo.” Ndugu mwenye uwezo azungumzia makala pamoja na mtangazaji mmoja au wawili ambao ni wenye mafanikio katika kuongoza mafunzo. Wakitumia sehemu katika kitabu Ujuzi kuwa vielelezo, wanasimulia njia stadi za kufundisha ambazo huwasaidia kufahamu yale ambayo hasa mwanafunzi anajifunza.—Ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996, fungu la 5, 8, 12, na 21.

Dak. 15: Tumia Vizuri Kichapo 1997 Yearbook of Jehovah’s Witnesses. Baba apitia mambo makuu yaliyo kwenye ukurasa wa 3-9 pamoja na familia yake. Aonyesha sababu ya sisi kushangilia kuona maendeleo ya kitheokrasi ulimwenguni kote. Baba aeleza jinsi, katika mwaka huu, wanavyoweza kuchukua dakika chache kuchunguza andiko la siku. (Makutaniko yanayotumia lugha ambayo kitabu-mwaka hakipatikani wanaweza kuratibu mahitaji ya kwao katika sehemu hii au hotuba itolewe na mzee kuhusu makala “Je, kwa Kweli Wahitaji Kuomba Radhi?” kutoka Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1996, ukurasa wa 22-24.)

Wimbo 165 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 26

Wimbo 148

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Pitia toleo la fasihi la Juni. Ukitumia kitabu Ujuzi, eleza jinsi mawazo yaliyo katika fungu la 17-19 kwenye ukurasa wa 10-11 yanavyoweza kutumiwa kutayarisha utoaji mfupi. Tia moyo wote wakazie fikira kujitahidi kuanzisha mafunzo. Kazia uhitaji wa kusaidia watu wenye kupendezwa kuendelea haraka.—Ona Mnara wa Mlinzi la Januari 15, 1996, ukurasa wa 13-14.

Dak. 15: “Kwa Nini Twafuliza Kurudi?” Maswali kwa majibu. Tia ndani mambo kutoka sanduku lililo kwenye ukurasa wa 570 katika kitabu Proclaimers.

Dak. 15: Hotuba itolewe na mzee kuhusu fungu la 22-32 ya broshua Mapokeo chini ya kichwa kidogo, “Tuwawekee Watoto Wetu Miradi Gani?” na “Mambo ya Kufundisha Watoto Wako.”

Wimbo 174 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki