Sanduku La Swali
◼ Ni tahadhari gani inayohitajiwa tunaposhirikiana na mtu wa jinsia tofauti kuhusiana na huduma yetu?
Tuna sababu ya kutazamia kwamba ndugu na dada zetu wanakusudia kushikamana na kiwango cha juu zaidi cha adili katika mwenendo wa kibinafsi. Hata hivyo, twaishi katika ulimwengu usio safi na wenye uendekevu ambao hauna mipaka mingi ya adili. Ingawa huenda tukawa na makusudio mema, lazima tulinde daima tuepuke kusababisha lawama au kujiingiza katika jambo lisilofaa. Hili latia ndani kuwa waangalifu tunapohusika katika huduma.
Katika utumishi wa shambani mara nyingi sisi hupata watu wa jinsia tofauti ambao huonyesha kule kuonekanako kuwa kupendezwa kwa moyo mweupe katika kweli. Ikiwa tuko peke yetu tunapokuwa tumezuru na hakuna mtu mwingine nyumbani, kwa kawaida lingekuwa jambo bora kutoa ushahidi mlangoni badala ya kuingia ndani. Ikiwa kupendezwa kupo, mipango yaweza kufanywa ya kurudi tukiwa tunaandamana na mtangazaji mwingine au wakati wengine kati ya watu wa nyumbani watakuwapo pia. Ikiwa hilo haliwezekani, lingekuwa jambo la hekima kumpa mtangazaji mwingine wa jinsia sawa na mwenye nyumba. Hilo pia lahusu katika kuongoza mafunzo ya Biblia na mtu wa jinsia tofauti.—Mt. 10:16.
Twahitaji kuwa waangalifu tunapochagua mtu wa kuhubiri naye katika huduma. Ijapokuwa watangazaji wa jinsia tofauti huenda wakahubiri pamoja nyakati nyingine, hilo lafaa zaidi lifanywapo kunapokuwa na kikundi. Kwa kawaida, hata tunapokuwa katika huduma, si jambo la hekima kwetu kuhubiri kila mara tukiwa peke yetu na mtu wa jinsia tofauti ambaye si mwenzi wetu wa ndoa. Kwa sababu hiyo, ndugu mwenye kusimamia kikundi cha utumishi apaswa kutumia uamuzi mzuri anapogawa watangazaji wahubiri pamoja, kutia ndani matineja.
Kwa kutumia uamuzi mzuri sikuzote, tutaepuka “[kutoa] sababu yoyote ya kukwaza” iwe ni sisi wenyewe au wengine.—2 Kor. 6:3.