Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/97 kur. 2-3
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 2
  • Juma Linaloanza Juni 9
  • Juma Linaloanza Juni 16
  • Juma Linaloanza Juni 23
  • Juma Linaloanza Juni 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 6/97 kur. 2-3

Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Juma Linaloanza Juni 2

Wimbo 181

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Toa maelezo kuhusu ripoti ya utumishi ya Februari ya nchi na ya kutaniko la kwenu.

Dak. 15: “Fanyeni Hata Zaidi Yote Kabisa Mwezayo.” Maswali na majibu.—Ona pia Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1993, ukurasa wa 28-30.

Dak. 22: “Ujuzi Kutoka kwa Mungu Hujibu Maswali Mengi.” Mwenyekiti azungumzia hiyo makala na watangazaji wawili au watatu, kutia na kijana mmoja. Toa maelezo kwenye fungu la 1, ukikazia sababu ambayo kitabu Ujuzi ni chenye matokeo katika kutusaidia kujibu maswali. Toa wonyesho wa kipindi cha mazoezi, na utoe madokezo ya uboreshaji baada ya kila utoaji.

Wimbo 200 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 9

Wimbo 189

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Hotuba itolewe na mzee ikishughulikia vichwa vidogo “Tohara” na “Ndoa, Mahari, Uzazi” kutoka katika broshua Mapokeo.

Dak. 20: Kuwafundisha Wengine—Uhitaji wa Haraka. Hotuba itolewe na mzee. Pitia ripoti ya utumishi wa ulimwenguni pote ya 1996 kwenye ukurasa wa 33 wa 1997 Yearbook. Jitihada iliyoongezeka ya kutolea watu ushahidi popote wanapoweza kupatikana inatokeza matokeo. Uhitaji wa haraka sasa ni kufuatia maangusho na kufundisha watu kweli. Unapowafikia mahali pa watu wote, omba jina lao na anwani kwa busara ili uweze kufanya ziara ya kurudia. Twahitaji kufanya mengi zaidi kuliko kupanda mbegu ya Ufalme tu; lazima pia tuimwagilie maji. (1 Kor. 3:6-8) Mbegu ipandwapo kwenye udongo mzuri, ufundishaji wenye matokeo waweza kusaidia mtu apate maana yayo. (Mt. 13:23) Twapaswa kushiriki kikamili na kwa ustadi iwezekanavyo katika kazi ya kufundisha. (Ebr. 5:12a) Unganisha mambo makuu kutoka nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996, fungu la 25-26. Kazia kujitahidi kuanzisha mafunzo katika ama broshua Anataka ama kitabu Ujuzi.

Wimbo 204 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 16

Wimbo 192

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Dokeza mambo ya kuzungumziwa katika magazeti ya karibuni.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: Kuitambulisha Dini Yako Kuwa ya Kweli au Isiyo ya Kweli. Mzee anaongoza mazungumzo pamoja na watangazaji wawili au watatu wenye uwezo, yakitegemea Amkeni! la Desemba 8, 1990, ukurasa wa 24. Kwa wazi watu wengi wenye mioyo myeupe wanarudiwa mara nyingi. Hata hivyo, hawajapata kamwe kukubali funzo la Biblia. Zungumza jinsi ambavyo mambo yaliyo katika makala hii ya Amkeni! yangeweza kutumiwa kuwajulisha uhitaji wa kutenda kupatana na ujuzi sahihi. Taja hoja za muhimu zilizoko katika kitabu Ujuzi, sura ya 5: “Ni Ibada ya Nani Anayoikubali Mungu?” Soma fungu la 20. Ziara za kurudia zaweza kufanywa kwa watu hao na kuwatia moyo kwa fadhili na kwa busara wakubali funzo na kuhudhuria mikutano.

Wimbo 201 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 23

Wimbo 193

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Eleza mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.

Dak. 15: Wanasema Nini Kutuhusu? Hotuba inayotegemea habari ipatikanayo katika Watch Tower Publications Index 1986-1995, ukurasa wa 341-343. (Habari kama hiyo yapatikana katika Index yoyote chini ya kichwa “Jehovah’s Witnesses” na kichwa kidogo “Statements by Others.”) Teua “Statements by Others” yenye kutokeza juu ya Mashahidi wa Yehova—mwenendo wetu na kazi yetu. Onyesha jinsi ambavyo wengine wamevutiwa vizuri na yale wanayoona kwetu. Eleza kwa nini hilo lapaswa kutuchochea sikuzote tuenende ifaavyo na kuvumilia katika kazi yetu. Taja jinsi ya kutumia maoni yenye kupendeza kama hayo tunapoongea na wajuani na watu wenye kupendezwa wanaotaka kujua mengi zaidi kutuhusu.

Dak. 20: “Wazazi—Zoezeni Watoto Wenu Kuhubiri.” Maswali na majibu. Tia ndani mwelekezo katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 99-100, chini ya kichwa kidogo “Kusaidia Vijana.”

Wimbo 211 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 30

Wimbo 197

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote walete ripoti zao za utumishi za Juni.

Dak. 20: “Vijana—Miradi Yenu ya Kiroho Ni Ipi?” Baba wawili wazungumzia makala hiyo pamoja. Wanafikiria kwa uangalifu jinsi ya kusaidia watoto wao wathamini ni kwa nini ni muhimu kuweka miradi ya kitheokrasi, itakayoleta baraka za kiroho, badala ya kufuatia mapendezi ya kimwili.—Ona pia kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 116-118.

Dak. 15: Kujitayarisha kwa Toleo la Fasihi la Julai. Chagua broshua moja au mbili ambazo zimeamsha kupendezwa katika eneo lenu, na upitie baadhi ya mambo yenye kutokeza kuhusu kila moja yazo. Dokeza njia ambazo hizo zaweza kuunganishwa katika utoaji. Kumbusha wote waandike maangusho, na kurudi kusitawisha kupendezwa.

Wimbo 109 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki