Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/97 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Julai 7
  • Juma Linaloanza Julai 14
  • Juma Linaloanza Julai 21
  • Juma Linaloanza Julai 28
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 7/97 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai

Juma Linaloanza Julai 7

Wimbo 6

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Eleza ripoti ya utumishi wa shambani ya Machi ya nchi na ya kutaniko la kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 13: “Uaminifu Unathawabishwa.” Maswali na majibu. Tia ndani kielelezo kinachosimuliwa katika Amkeni! la Januari 22, 1993, ukurasa wa 18-21.

Dak. 20: “Saidia Wengine Wapate Faraja.” Mazungumzo na wasikilizaji. Panga uwe na wonyesho mmoja au mawili. Alika wasikilizaji wasimulie njia nyingine ambazo wameanzisha mazungumzo, kwa kutumia broshua zilezile. Tia moyo kutumia maneno sahili, yaliyochaguliwa vizuri kuchochea kupendezwa. (Ona kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 7, fungu la 9-11.) Taja broshua nyingine ambazo huenda zikatolewa na ambazo kutaniko liko nazo akibani.

Wimbo 70 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 14

Wimbo 5

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Pitia “Tutajifunza Kitabu Furaha ya Familia.”

Dak. 18: “Toa Ushahidi Mahali Popote Palipo na Watu.” Hotuba. Wakati ukiruhusu, mambo yaliyoonwa ya ziada yanaweza kushirikishwa kutoka 1997 Yearbook, ukurasa wa 43-46.

Dak. 15: Wazazi—Fundisheni Watoto Wenu Tangu Utoto Sana. Mzee azungumzia kanuni za Kimaandiko akionyesha uhitaji wa wazazi kufundisha watoto wao tangu utoto sana. (Mit. 22:6; 2 Tim. 3:14, 15) Wazazi kadhaa wanahisi kwamba elimu ya Biblia kwa watoto haipasi kuandaliwa hadi wawe wakubwa vya kutosha kufanya maamuzi yao wenyewe. Katika visa hivyo watoto wengi wamepotea ulimwenguni. Mafunzo ya kiroho yapaswa kuanza tangu utoto sana. (g97-SW 3/8 26-27; w88-SW 8/1 12-13) Hoji wenzi waliooana wanaoonyesha hangaiko juu ya hali ya kiroho ya watoto wao. Onyesha jinsi baba anavyoongoza lakini kwamba wazazi wote wawili wanafanya sehemu yao katika kuandaa programu ya ufundishaji yenye upatano, iliyo kamili. Wenzi hao wasimulia kile ambacho wamekuwa wakifanya katika kujitahidi kufundisha watoto wao kweli, wakitumia madokezo ambayo tengenezo linaandaa ya kuwa na programu yenye matokeo na yenye kutumika, ya kufundisha nyumbani. Mzee akazia umaana wa kutumia yale ambayo Neno la Mungu huhimiza sana wazazi wafanye.—w85-E 4/1 23; Efe. 6:1-4.

Wimbo 71 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 21

Wimbo 14

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Pitia utendaji wa funzo la Biblia wa kutaniko lenu. Tia moyo wahubiri waanzishe mafunzo ya Biblia nyumbani mapya mwezi huu. Wakumbushe wale wanaoongoza mafunzo uhitaji wa kuyaongoza kwa ukawaida. Ikiwa lazima mtu asafiri kwa muda fulani mipango yaweza kufanywa mhubiri mwingine aongoze funzo hilo wakati ambapo mwenye kuliongoza hayuko.

Dak. 13: “Ni Nani Atakayekwenda kwa Ajili Yetu?” Hotuba chanya. Tia ndani kitia-moyo cha kufanya upainia wa kawaida na jambo lililoonwa lipatikanalo katika nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1997, fungu la 16-17. Wale ambao hawawezi kuwa mapainia wa kawaida wanaweza kutaka kupanga mwezi au miezi wanayotaka kufanya upainia-msaidizi mwaka wa utumishi ujao.

Dak. 20: Jitayarishe Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi. Kila siku, twapata fursa za kutolea watu tunaokutana nao ushahidi. Fursa itokeapo, huenda tukajipata hatuna Biblia au vichapo vya kutumia. Panga kimbele. Ukiwa nyumbani, weka fasihi kadhaa zinazoweza kufikiwa, karibu na mlango ambapo wewe husalimu wageni. Weka fasihi mbalimbali mfukoni au katika pochi, na uibebe au uiweke katika gari lako, kazini pako, au kwenye dawati lako shuleni. Beba kiasi fulani unapopanda magari ya umma. Pakia fasihi kadhaa unapoenda safari ya kibiashara, unaposafiri kwenye mkusanyiko, au unapoenda likizoni. Zungumzia madokezo yaliyo katika kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 80-82, fungu la 11-16. Toa wonyesho mfupi wa njia tofauti za kumfikia mchuuzi, mfanyakazi mwenzi, mwanashule mwenzi, na msafiri mwingine, au mtu aliye likizoni.

Wimbo 72 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 28

Wimbo 15

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote walete ripoti zao za utumishi wa shambani. Pitia toleo la fasihi la Agosti. Kazia kufuatia broshua zote zilizoangushwa katika Julai na ziara za kurudia Agosti, kwa kujaribu kuanzisha mafunzo ya Biblia. Ukitumia nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1997, onyesha baadhi ya mambo muhimu ili kufanya ziara ya kurudia yenye matokeo. Mafunzo yapasa kuanzishwa katika broshua Anataka au kitabu Ujuzi.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 18: Timiza Huduma Yako Kikamili. Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi ikitegemea kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 5-8. Kazia umaana na uharaka wa kazi ya kuhubiri, ukichochea wote wachukue kwa uzito daraka lao wakiwa wahudumu.

Wimbo 75 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki