Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Septemba: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu chaweza kutolewa kikiwa toleo la badala. Oktoba: Toa maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi toa nakala mojamoja za magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Kuanzia sehemu ya mwisho ya mwezi huu, trakti Habari za Ufalme Na. 35 itagawanywa. Novemba: Ugawanyaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35 utaendelea. Makutaniko yatakayomaliza eneo lao kwa kufikia wenye nyumba katika kila nyumba au makao kwa nakala ya trakti Habari za Ufalme Na. 35 wanaweza kutoa kitabu Ujuzi. Desemba: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeagizwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hilo lifanywapo.
◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyotolewa kwenye ukurasa wa 21-23 katika Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991, kuhusu watu wowote waliotengwa au waliojitenga na ushirika ambao huenda wakawa na mwelekeo wa kurudishwa.
◼ Wale wanaoshirikiana na kutaniko wapaswa kutuma maandikisho yote mapya na ya kufanywa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho yao ya kibinafsi, kupitia kutaniko.
◼ Sosaiti haishughulikii maagizo ya fasihi ya wahubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-msimamizi apaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla agizo la kila mwezi la kutaniko la fasihi halijapelekwa kwa Sosaiti ili wote wenye kupendezwa kupata fasihi za kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia fasihi. Tafadhali kumbuka ni vichapo gani vilivyo vifaa vya kuagizwa kipekee.
◼ Sasa makutaniko yanaweza kuanza kutoa maombi ya The Secret of Family Happiness—On Videocassette (Buku la 1 hadi la 6) katika Lugha ya Ishara ya Kimarekani. Hayo yataonekana yakiwa “Yanayokuja” katika orodha ya upakizi ya kutaniko hadi vidiokaseti hizi zipatikane. Jitihada zitafanywa kusafirisha kila ya vidiokaseti hizo kwa wakati ili habari iliyomo ichunguzwe kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko. Vidiokaseti hizi zapasa kuagizwa na wale tu wanaoifahamu Lugha ya Ishara ya Kimarekani.
◼ Makutaniko yanapofanya ombi la fasihi, yapasa kukumbuka kwamba maktaba ya Sosaiti ya CD-ROM si ya kugawanywa bila kuchagua kwa busara. Ni ya kutumiwa hasa na wahubiri.
◼ “Sanduku la Swali” katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1997 lilipendekeza kwamba tuwe wenye hadhari juu ya kuhubiri katika huduma na wahubiri wa jinsia tofauti. Kuna sababu nzuri kwa wote kutumia uamuzi mzuri kuhusu jambo hili. Hili halimaanishi kwamba waangalizi wasafirio au hata ndugu wengine hawawezi kuhubiri katika huduma ya shambani pamoja na akina dada. Badala ya hivyo, wazo hilo lilionyesha kwamba si jambo la hekima kwa ndugu kushinda kwa ukawaida peke yake akiwa na mtu yuleyule wa jinsia tofauti ambaye si wa jamaa yake.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Jina la Mungu Litakaloendelea Milele —Kiarabu
Siri ya Kupata Furaha ya Familia —Kiurdu
Hellfire—Is It Part of Divine Justice? (Trakti Na. 74) —Kiarabu
How to Start and Continue Bible Discussions —Kigujarati
Watch Tower Publications Index 1996 —Kiingereza