Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/97 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Septemba 1
  • Juma Linaloanza Septemba 8
  • Juma Linaloanza Septemba 15
  • Juma Linaloanza Septemba 22
  • Juma Linaloanza Septemba 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 9/97 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba

Juma Linaloanza Septemba 1

Wimbo 26

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: “Weka Mambo Yaliyo ya Maana Zaidi Kwanza.” Maswali na majibu. Wakati ukiruhusu, toa maelezo kuhusu “Kuweka Matangulizo Yanayofaa” katika Amkeni! la Januari 8, 1988, ukurasa wa 8-9.

Dak. 20: “Kushiriki na Wengine Siri ya Kupata Furaha ya Familia.” Hotuba ishughulikie fungu la 1 na 6-8. Toa wonyesho kwa fungu la 2-5. Taja kwamba kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu chaweza kutolewa kikiwa toleo la badala, na utie moyo wahubiri watumie kichapo hiki kwa wale ambao wanaweza kunufaika na habari yake yenye mafaa. Kazia kukumbuka kufanya wanafunzi na kufikia mradi wa kuanzisha mafunzo.

Wimbo 107 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 8

Wimbo 27

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 10: “Mafunzo ya Biblia Yanayotokeza Wanafunzi.” Hotuba.

Dak. 15: Mzee azungumzia “Chochea Wanafunzi Waelekee Wakfu na Ubatizo” (km-SW 6/96 nyongeza, fu. 20-22) pamoja na wahubiri wazoefu wanaoongoza mafunzo.

Wimbo 109 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 15

Wimbo 30

Dak. 10: Matangazo ya kwenu.

Dak. 15: Tumia Vidio kwa Manufaa. Pitia madokezo ya kutumia vidio za Sosaiti na usimulie mambo yaliyoonwa yanayoonyesha jinsi ya kutumia vidio zaidi, katika familia zetu na katika huduma yetu. Mahali ambapo habari kuhusu vidio haitumiki, tumia mwingi wa wakati uliowekwa kutia moyo wahubiri wafuatie kupendezwa wakati kikaratasi (S-70) “Please Arrange . . . To Call on This Person” kinapopokewa katika kutaniko. Kupendezwa huku kwapasa kufuatiwa mara moja. Tumesikia mambo yaliyoonwa ambapo kupendezwa huko kulifuatiwa, na mtu aliyependezwa akawa ndugu yetu.

Dak. 20: Je, Unatumia Broshua Shule? Mzee azungumzia Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1985, ukurasa wa 30-31 (la Kiingereza), pamoja na baadhi ya wazazi na watoto. Wanasimulia mambo yao ya kibinafsi yaliyoonwa wakitumia broshua Shule.

Wimbo 112 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 22

Wimbo 32

Dak. 8: Matangazo ya kwenu.

Dak. 17: Jinsi ya Kuanzisha Mazungumzo. Kadiri kubwa ya mafanikio yetu katika huduma yategemea kuweza kwetu kuwahusisha watu wengine katika mazungumzo ya maana. Tunapoweza kusema jambo fulani linalowafanya wengine wasikilize, tumeshinda kimojawapo cha vizuizi vikubwa zaidi tunavyokabili tunapotoa ushahidi. Zungumza na wahubiri madokezo makuu yaliyo katika kitabu Kiongozi cha Shule, somo la 16, fungu la 11-14. Panga wasikilizaji wenye ustadi na wenye matokeo ya kuanzisha mazungumzo wasimulie maneno ya ufunguzi wanayotumia wanaposema na watu kama (1) anayetembea kwa miguu barabarani, (2) abiria kwenye basi, (3) karani mezani, (4) mnunuzi kwenye maegesho ya magari, (5) mtu aketiye kwenye kiti cha bustani, na (6) mtu anayetolewa ushahidi kupitia simu.

Dak. 20: Pitia Ripoti ya Mwaka wa Utumishi ya Kutaniko ya 1997. Mwangalizi wa utumishi apongeza kutaniko kwa jitihada nzuri, hasa wakati wa Machi, Aprili, na Mei. Atoa madokezo kutoka baraza la wazee na ripoti ya mwisho ya mwangalizi wa mzunguko ya kuongeza utendaji wa utumishi wa shambani na wa funzo la Biblia. Onyesha baadhi ya miradi ifaayo kwa ajili ya mwaka mpya wa utumishi, kutia ndani kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia na kufanya upainia-msaidizi miezi iliyo na miisho-juma mitano—Novemba, Mei, Agosti.

Wimbo 113 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 29

Wimbo 37

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote walete ripoti za utumishi wa shambani. Taja kwamba tutaanza kujifunza kitabu Furaha ya Familia juma lifuatalo kwenye funzo la kitabu. Katika kujitayarisha kwa ajili ya kazi ya magazeti katika Oktoba, zungumzia uhitaji wa “[Ku]changanua Eneo Lako,” “[Ku]yafahamu Magazeti,” “[Ku]tayarisha Utangulizi Wako,” “[Ku]badikilikana Umfae Mwenye Nyumba,” “[Kusaidiana],” kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1996, ukurasa wa 12.

Dak. 15: Mkristo Apaswa Kufanya Nini Aitwapo kwa Ajili ya Kazi ya Baraza la Mahakama? Hotuba itolewe na mzee juu ya Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 1997, ukurasa wa 27-29. Kanuni hizohizo zingetumika wakati mtu aombwapo kuwa mmoja wa wakadiriaji wa mahakama, na habari hiyo yaweza kupatanishwa na mahitaji ya kwenu.

Dak. 15: Tukuza Huduma Yako. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji ya kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 81-83. Uliza maswali haya ili kukazia mambo makuu: (1) Twanufaikaje kwa kufuata kielelezo cha Yesu? (2) Daraka letu la kuhubiri ni lenye maana kadiri gani? (3) Ni makusudi gani yaliyotuchochea tuweke maisha zetu wakfu kwa Yehova? (4) Ni mwenendo wa aina gani unaotakwa ili mtu amtumikie Mungu? (5) Twaweza kujifunza nini kutokana na alivyofundisha Yesu?

Wimbo 121 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki