Weka Mambo Yaliyo ya Maana Zaidi Kwanza
1 Ni gani baadhi ya mambo yaliyo ya maana yaliyo muhimu katika hali-njema yetu ya kiroho? Hapana shaka hayo yatatia ndani funzo la kibinafsi, hudhurio la mikutano, kudumu katika sala, ushirika mzuri, na huduma ya Kikristo. Hatuwezi kudumisha afya nzuri ya kiroho bila kuweka mambo yaliyo ya maana kwanza kabisa katika maisha yetu.
2 Hata hivyo, sisi sote tuna pigano dhidi ya tamaa za kimwili na twahitaji nidhamu. (Gal. 5:17) Hatupaswi kuhisi kamwe kwamba tungenufaika zaidi kwa kufuatia upendezi wa ubinafsi. (Yer. 17:9) Kwa hiyo, ikiwa tutalinda moyo wetu na kuepuka kuongozwa vibaya, uchunguzi wa kibinafsi wa kawaida ni wa muhimu sana.—Mit. 4:23; 2 Kor. 13:5.
3 Chunguza Moyo Wako Mwenyewe: Waweza kufanya hivyo kwa kujiuliza mwenyewe maswali ya wazi: Je, natamani sana kusoma Neno la Mungu? (1 Pet. 2:2) Je, nathamini umaana wa kuhudhuria mikutano yote ya kutaniko? (Ebr. 10:24, 25) Je, mimi hudumu katika sala? (Rom. 12:12) Je, natafuta ushirika wa watu wenye kukazia mambo ya kiroho? (Rom. 1:11, 12) Je, nahisi nikiwa na daraka la kibinafsi la kutangaza habari njema? (1 Kor. 9:16) Majibu chanya yataonyesha kwamba unatamani kuweka mambo yaliyo ya maana zaidi kwanza.
4 Chunguza Kawaida Yako ya Kila Siku: Wahitaji kuendelea kufuatia uchunguzi wa tamaa za moyo wako kwa kusitawisha mambo ya kutangulizwa kwa ajili ya matumizi ya wakati. Hilo latia ndani kuratibu wakati wa kusoma Biblia kwa ukawaida na kila toleo la Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, na vilevile kutayarisha kwa ajili ya mikutano. Pia lazima wakati utengwe wa familia kujifunza na kusali pamoja. Weka mpaka wa kiwango cha wakati kinachotumiwa kutazama televisheni au kutumia kompyuta. Azimia kutanguliza kuhudhuria mikutano yote ya kutaniko, na upange mambo mengine yote baadaye. Panga familia yote ishiriki katika utumishi wa shambani kila juma.
5 Bila shaka, kuweka mambo yaliyo ya maana zaidi kwanza katika maisha yetu kutathibitika kuwa sababu ya shangwe.