Mikutano Ya Utumishi Kwa Oktoba
TAARIFA: Huduma ya Ufalme Yetu itaratibu Mkutano wa Utumishi wa kila juma wakati wa miezi ya mkusanyiko. Makutaniko yanaweza kufanya marekebisho kama ihitajiwavyo ili yaruhusu uhudhuriaji wa “Imani Katika Neno la Mungu” Mkusanyiko wa Wilaya na kwa ajili ya pitio la dakika 30 la mambo makuu ya programu kwenye Mkutano wa Utumishi juma lifuatalo. Pitio la siku kwa siku la programu ya mkusanyiko wa wilaya lapaswa kugawiwa mapema ndugu wawili au watatu wenye sifa ya ustahili ambao wataweza kukazia mambo makuu yenye kutokeza. Pitio hili lililotayarishwa vizuri litasaidia kutaniko likumbuke mambo makuu ya kutumia kibinafsi na shambani. Maelezo kutoka kwa wasikilizaji na mambo yaliyoonwa yaliyosimuliwa yapaswa yawe mafupi na ya moja kwa moja.
Juma Linaloanza Oktoba 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Je, Watu Wote Watapata Kupendana?” Maswali na majibu. Pitia mambo makuu ya trakti Habari za Ufalme Na. 35. Onyesha sababu kwa nini watu katika eneo watanufaika na habari hii. Kazia uhitaji wa kufanya mipango sasa ya kushiriki kikamili katika kugawanya na kujitahidi kufuatia kupendezwa kote kunakopatikana.
Dak. 20: “Gawanya Trakti Habari za Ufalme Na. 35 kwa Kuieneza Sana.” Hotuba ya kufungua itolewe na mwangalizi wa utumishi. Shughulikia fungu la 5-8 kwa maswali na majibu. Pitia mipango ya kwenu ya utendaji mpana. Zungumzia njia za kuhakikisha eneo lote limemalizwa. Trakti Habari za Ufalme Na. 35 yaweza kutumiwa na wahubiri wanapotolea watu ushahidi kwenye vituo vya basi, biashara ndogondogo, maegesho ya magari, na kwingineko. Toa madokezo ya jinsi ya kusaidia wapya wanaotaka kuanza kuhubiri. Tia ndani habari itokayo katika nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Aprili 1995, fungu la 11. Fanya maonyesho mawili au matatu mafupi ya utoaji mbalimbali.
Wimbo 126 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Pitia mambo ya kuongea katika matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kumbusha wote kwamba wakati wa utendaji wa mwisho-juma, maandikisho ya magazeti yatatolewa pamoja na trakti Habari za Ufalme Na. 35. Twapaswa kufuatia kupendezwa kote.
Dak. 23: “‘Imani Katika Neno la Mungu’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1997.” (Fungu la 1-15) Maswali na majibu. Soma fungu la 8, 10, na 13. Kazia umaana wa Kimaandiko wa kudumisha sura na mwenendo wetu wa Kikristo wenye staha na kusimamia watoto wetu vizuri.
Dak. 12: “Je, Wewe Huitikiaje Ubaridi?” Mazungumzo kati ya wazee wawili. Tia ndani maelezo juu ya habari iliyo chini ya kichwa kidogo “Jinsi ya Kushambulia Ubaridi” katika Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1974, ukurasa wa 445-446 (la Kiingereza.)
Wimbo 130 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 20
Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Pitia baadhi ya mambo yaliyoonwa kutoka 1996 Yearbook, ukurasa wa 6-8, juu ya “Global Distribution of ‘Kingdom News.’” Kazia jitihada walizotia wahubiri mmoja-mmoja katika ugawanyaji uliopita wa trakti Habari za Ufalme. Tia moyo wote washiriki kikamili katika kugawanya trakti Habari za Ufalme Na. 35.
Dak. 14: “‘Imani Katika Neno la Mungu’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1997.” (Fungu la 16-22) Maswali na majibu. Soma fungu la 16 na maandiko yaliyotajwa. Kazia uhitaji wa kuwa wenye utaratibu na kufikiria wengine, hasa kuhusu viti. Malizia kwa hotuba fupi ukipitia “Vikumbusha vya Mkusanyiko wa Wilaya.”
Dak. 18: “Je, Wewe Ni Shahidi wa Wakati Wote?” Hotuba itolewe na mzee.
Wimbo 133 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 27
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Pitia maendeleo ya ugawanyaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35. Alika wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo. Toa ripoti ya kadiri ambayo eneo limehubiriwa kufikia sasa na kitakachohitajiwa ili kutimiza kulimaliza kufikia Novemba 16. Eneo linapohubiriwa kabisa, tutatoa kitabu Ujuzi sehemu inayobaki ya mwezi huo. Kazia mradi wa kuanzisha mafunzo kwenye ziara za kurudia mahali palipokuwa na itikio zuri kwa trakti Habari za Ufalme.
Dak. 15: Jinsi ya Kupata Tumaini Katikati ya Hali ya Kukata Tumaini. Hotuba itolewe na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1997, ukurasa wa 22-25.
Dak. 18: Nuru Yenu na Ing’ae. Hotuba na mazungumzo juu ya kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 84-88. Panga mapema wahubiri watoe maelezo mahususi kuhusu maswali yafuatayo: (1) Kwa nini Mashahidi wa Yehova huhubiri nyumba hadi nyumba? (2) Njia hii ilitumiwa kwa kadiri gani katika karne ya kwanza? (3) Kwa nini kuna uhitaji wa haraka wa kufuliza kuhubiri nyumba hadi nyumba? (4) Ni hali gani ambazo huenda zikafanya iwe vigumu kwetu kushiriki kwa ukawaida? (5) Twaweza kupataje msaada ili kuvumilia? (6) Twabarikiwaje kwa kuacha nuru yetu ing’ae? (7) Twaweza kufanya nini ili tuwe na mafanikio zaidi katika kufikia watu? Toa kielezi kwa kupanga wahubiri watatu au wanne wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo yaliyofurahiwa wakati wa kuhubiri duka hadi duka au kutoa ushahidi barabarani.
Wimbo 136 na sala ya kumalizia.