Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Oktoba: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halikubaliwi toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Kuanzia Oktoba 12, trakti Habari za Ufalme Na. 35 itagawanywa. Novemba: Ugawanyaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35 utaendelea. Makutaniko yatakayomaliza eneo lao kwa kufikia wenye nyumba katika kila nyumba au makao kwa nakala ya trakti Habari za Ufalme Na. 35 wanaweza kutoa kitabu Ujuzi. Desemba: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika Kiingereza na Kiswahili na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Katika maeneo mengine Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani vyaweza kutolewa. Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kwenye karatasi ambayo hugeuka rangi kuwa manjano au huchakaa kilichochapishwa kabla ya 1985 ambacho huenda ikawa kutaniko linacho akibani kitolewe kwa nusu-bei. Kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha pia chaweza kutolewa kwa nusu-bei lakini vitabu vingine vyenye kurasa 192 vilivyochapishwa kabla ya 1985 kwenye karatasi isiyochakaa au kubadilika rangi, havitiwi ndani ya toleo hili lililopunguzwa bei. Makutaniko ambayo hayana ugavi wa vitabu hivyo yaweza kutoa Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli, Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya, au Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani.”
◼ Nyongeza moja iliyo katika toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu ni “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1998” na yapasa kuwekwa kwa ajili ya marejezo katika mwaka wote wa 1998.
◼ Kukiwa na miisho-juma mitano kamili, mwezi wa Novemba waweza kuwa wakati unaofaa kwa wengi kufanya upainia-msaidizi.
◼ Saa za mikutano za makutaniko mengi zitabadilika Januari 1. Kwa hiyo huenda kukawa na uhitaji wa kuagiza vikaratasi vipya vya kukaribisha watu ili kuonyesha saa za mikutano zilizorekebishwa.
◼ Mialiko ya Ukumbusho ya 1998 katika lugha ya msingi ya kila kutaniko imetiwa ndani pamoja na upakizi ule mwingine. Yapasa kupatikana kwa ajili ya ugawanyaji kuanzia majuma machache kabla ya Ukumbusho.
◼ Makutaniko yapaswa kuanza kuagiza Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1998 pamoja na agizo lao la fasihi la Oktoba. Vijitabu hivyo vitapatikana katika Kiamhara, Kiarabu, Kichina, Kichina (Sahili), Kifaransa, Kigujarati, Kihindi, Kiingereza, Kinyarwanda, na Kiswahili. Vijitabu hivi ni bidhaa za agizo la pekee.