Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/97 uku. 11
  • Je, Wewe Ni Shahidi wa Wakati Wote?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Ni Shahidi wa Wakati Wote?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Wakumbuke Watumishi wa Wakati Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Wewe Utachagua Kazi Gani ya Maisha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kufanya Yote Yote Tuwezayo Tuzitangaze Habari Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Unakadiriaje Mafanikio?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 10/97 uku. 11

Je, Wewe Ni Shahidi wa Wakati Wote?

1 Ungejibu ndiyo kwa swali hili? Ijapokuwa si wote kati ya watumishi wa Yehova waliojiweka wakfu wanaoweza kujiandikisha katika huduma ya wakati wote, je, si jambo la akili kutazamia kwamba sisi sote twapaswa kujiona wenyewe kuwa Mashahidi wa wakati wote? Bila shaka twapaswa kujiona hivyo.

2 Haiwezekani kuwa Mkristo asiye wa wakati wote. Yesu alisema kuhusu Baba yake hivi: “Sikuzote mimi hufanya mambo yale yanayompendeza.” (Yn. 8:29) Paulo, ambaye alihisi vivyo hivyo, alitusihi “[tufanye] mambo yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Kor. 10:31) Basi, yatupasa sisi sote tujione wenyewe kuwa Mashahidi wa Yehova wa wakati wote. Kufikiri kwetu kwa njia hii kutatuathiri kwa uzuri katika kila utendaji tufuatiao.

3 Fikiria Uthibitisho: Sura, usemi, na mwenendo wetu waweza kuonyesha watu wengine kwamba sisi ni Mashahidi wa Yehova kwelikweli. Twaona kuwe uhitaji wa kuwa wenye sura ya kiasi, usemi wenye kujenga, mwenendo ufaao tunaposhiriki katika utumishi wa shambani au kuhudhuria mikutano ya Kikristo. Hata hivyo, iwe twaenda shuleni, twafanya kazi ya kilimwengu, au kushiriki katika tafrija, kila kitu kutuhusu hakina budi kutupatia uthibitisho kwamba twaishi kulingana na viwango vya uadilifu vya Yehova.

4 Yesu alisema: “Jiji haliwezi kufichwa liwapo limesimama juu ya mlima. . . . Acheni nuru yenu ing’ae mbele ya watu, ili wapate kuona kazi zenu bora na kumpa utukufu Baba yenu aliye katika mbingu.” (Mt. 5:14-16) Yapasa kuwa hivyo katika kila kitu tufanyacho na nyakati zote. Tukiona kwamba tunasitasita kutoa ushahidi kwa sababu ya mahali tulipo au kile tufanyacho, twahitaji kujiuliza wenyewe hivi, ‘Namtumikia Yehova kwa wakati usio wote au kwa wakati wote?’ Tusiache kamwe fursa ipite bila kuongea na wengine kuhusu habari njema za Ufalme wa Mungu.

5 Kumbuka, twamheshimu na kumpendeza Yehova tunapoweza kujibu swali hili, “Je, wewe ni Shahidi wa wakati wote?” kwa jibu “Ndiyo!” lenye kuvuma.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki