Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/97 uku. 1
  • Watu Wanakukosa!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watu Wanakukosa!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unashiriki Katika Kufanya Mikutano ya Kikristo Iwe Yenye Kujenga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Kwa Nini Tunapaswa Kukutanika Pamoja kwa Ajili ya Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Desturi Yako Ni Nini?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Ratiba ya Familia—Mikutano ya Kutaniko
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 12/97 uku. 1

Watu Wanakukosa!

1 Mara kwa mara, huenda tukakosa mkutano mmoja au miwili ya kutaniko, tukihisi ‘hakuna mtu atakayenikosa; hata hawatajua kwamba sipo.’ Hilo si kweli! Kama vile kiungo chochote kile cha mwili wetu wa kiasili, kila mmoja wetu ana fungu muhimu katika utendaji wa kutaniko. (1 Kor. 12:12) Kutokuwapo kwetu katika mkutano wa kila juma kwaweza kuathiri hali njema ya kiroho ya wengine wanaohudhuria. Usipokuwapo, uwe na hakika kwamba—watu wanakukosa!

2 Fungu Muhimu Unalotimiza: Paulo alikuwa na hamu nyingi ya kushirikiana na ndugu zake. Waroma 1:11, 12 hueleza sababu: “Ili nipate kuwapa baadhi ya zawadi ya kiroho . . . kwamba kupate kuwa na badilishano la kitia-moyo miongoni mwenu, kwa kila mmoja kupitia imani ya mwingine, yenu na yangu pia.” Hali kadhalika, kupitia maelezo yetu, sehemu zetu kwenye mkutano, na kuwapo kwetu hasa, twafanya mengi katika kujengana na kuendelea katika mwendo wa uaminifu.—1 The. 5:11.

3 Je, hutazamii kwa hamu kuona wengine kwenye mikutano ya kutaniko? Sikiliza kwa uangalifu maelezo yao na kuthamini usemi wao wa imani. Zawadi zao za kiroho huchangia kujengwa kwako. Ikiwa hawangekuwapo mkutanoni, ungehisi kwamba kitu fulani cha maana kilikosekana. Ndivyo wanavyohisi ndugu na dada zako wakati unapokosa kuwapo.

4 Fungu Muhimu Linalotimizwa na Mikutano: Wakati mmoja gazeti Mnara wa Mlinzi lilieleza juu ya umuhimu wa mikutano kwa ajili ya wokovu wetu wa kiroho, liliposema: “Katika ulimwengu huu uliogawanywa na mzozo, na usio na adili, kutaniko la Kikristo ni kimbilio la kiroho la kweli . . . , kituo cha amani na upendo. Kwa hiyo, uwe mhudhuriaji wa kawaida kwenye mikutano yalo yote.” (w93-SW 8/15 11) Kila siku, twakabili hali zinazotudhoofisha kiroho. Tusipokuwa waangalifu, twaweza kujishughulisha sana na mahangaiko yetu hivi kwamba huenda tukakosa kuona mambo ya kiroho yaliyo ya maana zaidi. Sisi sote twategemeana ili tupate kitia-moyo tunachohitaji ili tuendelee tukiwa tumeungana na wenye bidii katika utumishi wa Mungu.—Ebr. 10:24, 25.

5 Kuhudhuria kwetu mikutano ni kwa muhimu. Huenda ugonjwa au mambo yasiyotazamiwa yakatufanya tukose mara kwa mara kuhudhuria. Kama sivyo, acheni tuazimie sikuzote kuhesabiwa miongoni mwa songamano lenye kukutanika ambalo humsifu Yehova pamoja!—Zab. 26:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki