Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/97 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 1
  • Juma Linaloanza Desemba 8
  • Juma Linaloanza Desemba 15
  • Juma Linaloanza Desemba 22
  • Juma Linaloanza Desemba 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 12/97 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba

Juma Linaloanza Desemba 1

Wimbo 57

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Vikumbusha vya Sikukuu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Wengi wetu twapangia utendaji wa ziada miezi ya sikukuu, na huo huenda ukatia ndani likizo, kutembelea jamaa, au kufurahia tafrija. Twaweza kupangaje mambo ili utendaji wa kitheokrasi usipuuzwe? Zungumzia yafuatayo: (1) Kuhudhuria siku zote tatu za mkusanyiko wa wilaya. (2) Kudumisha hudhurio la kawaida kwenye mikutano, iwe uko nyumbani au mbali na nyumbani. (3) Kupanga kushiriki kwa ukawaida katika huduma, na ukiwa mbali na nyumbani, kupeleka ripoti za utumishi wa shambani kwenye kutaniko. (4) Kuchukua fasihi kadhaa za kutoa ushahidi wa vivi hivi unaposafiri. (5) Kutoa ushahidi wa jioni mara nyingi zaidi. (6) Kujiandikisha uwe painia-msaidizi kwa mwezi mmoja au zaidi. (7) Wazee kupanga vizuri utendaji mbalimbali wa kutaniko na kuhakikisha kwamba kazi alizogawiwa kila mmoja zinafanywa wakati anapokuwa hayupo.

Dak. 13: “Sema Juu ya Yehova Kila Siku.” Maswali na Majibu. Unaposhughulikia fungu la 4, tia ndani maelezo kutoka kitabu Kiongozi cha Shule, somo la 16, fungu la 14-16.

Dak. 20: “Biblia—Kiongozi Ambacho Mungu Amewapa Watu Wote.” Mzee azungumzia makala hiyo akitia ndani sababu kwa nini kila mtu apasa kuchochewa kuichunguza Biblia. Hoji kifupi wahubiri wawili jinsi ambavyo wamejitayarisha kutumia madokezo ya utoaji mbalimbali ulio katika fungu la 3-8. Toa wonyesho wa ziara ya kwanza na ziara ya kurudia inayolingana.

Wimbo 165 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 8

Wimbo 58

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 20: Kwa Nini Lililo Baya Liripotiwe? Hotuba itolewe na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1997, ukurasa wa 26-30.

Dak. 15: “Watu Wanakukosa!” Mazungumzo na wasikilizaji yakiongozwa na mzee. Taja wastani wa hudhurio la mikutano ya kutaniko. Alika wengine wasimulie sababu kwa nini wao huburudishwa kwa kuwa pamoja kwenye mikutano.

Wimbo 172 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 15

Wimbo 63

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Toa madokezo ya jinsi ya kuitikia kwa busara salamu za sikukuu. Eleza mipango ya pekee ya utumishi wa shambani ya Desemba 25 na Januari 1.

Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 25: “Twapaswa Kuwa Walimu, Si Wahubiri Tu.” Maswali na majibu. Unaposhughulikia fungu la 11, soma kitabu Kiongozi cha Shule, somo la 15, fungu la 11.

Wimbo 174 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 22

Wimbo 138

Dak. 8: Matangazo ya kwenu.

Dak. 17: “Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1998.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Pitia njia ambazo wote wanaweza kunufaika nazo kikamili zaidi kutokana na shule wakati wa mwaka ujao. Tia moyo kwenda sambamba na “Ratiba ya Kuongezea ya Usomaji wa Biblia” kila juma.

Dak. 20: Hubiri Habari Njema Kila Mahali. Mazungumzo na wasikilizaji ya kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 92-97, ukitumia maswali haya: (1) Kwa nini matumizi ya fasihi zetu ni yenye matokeo katika kueneza habari njema? Kwa nini twapaswa kutoa fasihi katika kila fursa? (2) Kwa nini tutambue uhitaji wa kutoa ushahidi wa vivi hivi? Ni zipi kati ya njia za kutoa ushahidi wa vivi hivi? (Alika watu kadhaa wasimulie mambo yaliyoonwa ya kutoa ushahidi wa vivi hivi.) (3) Kwa nini kutaniko lijitahidi kutimiza mgawo wake wa eneo? Mahali palipo na eneo la kutosha, faida ya kuwa na eneo la kibinafsi ni nini? (4) Twanufaikaje na mipango ya vikundi vya kutoa ushahidi? Twaweza kupangaje utendaji wetu wa kutoa ushahidi ili kuhakikisha kwamba twatumia wakati wetu kwa njia bora zaidi?

Wimbo 222 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 29

Wimbo 181

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote walete ripoti zao za utumishi wa shambani. Ikiwa kutaniko lenu litabadili saa za mikutano mwaka mpya, toa kitia-moyo chenye fadhili ukisihi wote wadumishe hudhurio la mikutano kwa kawaida pamoja na kutaniko na saa zake mpya. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 18: Pitia Toleo la Fasihi la Januari. Onyesha vitabu vya zamani ambavyo kutaniko linavyo kwa kutosha, na utaje mambo yenye kupendeza ya kuzungumzwa ambayo yatakuwa yenye msaada katika kutayarisha utoaji mbalimbali. Tia ndani wonyesho mmoja. Twapaswa kuendeleza jitihada zetu za kuanzisha mafunzo ama katika broshua Anataka ama kitabu Ujuzi.

Dak. 15: “Pata Manufaa Zote za Shule.” Baba azungumzia makala hii na watoto, kutia na mambo yenye kusaidia kutoka Amkeni!, Desemba 22, 1995, ukurasa wa 7-11.

Wimbo 215 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki