Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili
Juma Linaloanza Aprili 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Kumbusha kila mtu mahali na wakati wa mwadhimisho wa Ukumbusho Jumamosi, Aprili 11. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Huduma Yetu—Wonyesho wa Upendo wa Kweli.” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo mafupi juu ya Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 1987, ukurasa wa 16-17, fungu la 3-7.
Dak. 20: “Magazeti Yatangaza Ufalme.” Mzee ashughulikia makala akiwa na kikundi cha wahubiri watatu au wanne ambao ni wenye matokeo katika kuangusha magazeti. Zungumzia sehemu zinazovutia za majarida ya karibuni, ukidokeza njia ambazo mambo haya yanavyoweza kufanywa kuwa sehemu ya utoaji wetu. Fikirieni jinsi ugawanyaji wa magazeti unavyoweza kuongezwa katika eneo la kwenu. Ukitumia matoleo ya karibuni, onyesha makala zinazoamsha kupendezwa, kama zile zinazohusu matatizo ya jamii, familia, au jumuiya. Panga kuwe na maonyesho mawili au matatu mafupi.
Wimbo 205 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Hudhuria Mikutano ‘Zaidi Sana Hivyo.’” Maswali na majibu. Wakati uruhusupo, pitia onyo la upole lipatikanalo katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 64-65. Pongeza kwa uchangamfu wote wahudhuriao mikutano kwa ukawaida.
Wimbo 119 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 20
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Eleza kwamba haijawa kuchelewa mno kuleta ombi la upainia-msaidizi la Mei.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee anayeonyesha kwa fadhili njia mahususi ambazo maendeleo yanaweza kufanywa kwenu.
Dak. 25: “Mafunzo Zaidi ya Biblia Yanatakwa.” Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Pitia utendaji wa mafunzo ya Biblia wa kwenu. Pongeza mahali ambapo kutaniko limefanya vema. Onyesha yale yawezayo kufanywa zaidi katika kuanzisha mafunzo ya Biblia, kutia na mafunzo ya familia. Toa kielezi kuhusu fungu la 5 kwa kuhoji mzazi ambaye ni wa kawaida katika kuongoza funzo la familia. Soma fungu la 8, na ukazie mambo manane yaliyoorodheshwa. Elezea fungu la 13 kwa kumwalika mhubiri ambaye ni mwenye matokeo katika kuongoza mafunzo ya Biblia asimulie jinsi ambavyo imewezekana kushughulikia habari ya funzo bila kuchelewa isivyo lazima. Tia ndani jambo lililoonwa lililochaguliwa vizuri kuonyesha jinsi ambavyo matokeo mazuri yamefikiwa kwenu.
Wimbo 109 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 27
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Tangaza majina ya wale ambao watafanya upainia-msaidizi katika Mei. Taja mipango ya ziada inayofanywa kwenu kwa ajili ya mikutano ya utumishi. Simulia madokezo yenye kusaidia ya kutayarisha utoaji mbalimbali unaokazia magazeti ya karibuni.—Ona Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1996, ukurasa wa 12.
Dak. 15: Jinsi Ambavyo Wachungaji Wakristo Hukutumikia. Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 1996, ukurasa wa 24-27.
Dak. 18: Endeleza Mtazamo Ufaao Unapohubiri Katika Eneo Linalohubiriwa Mara Nyingi. Mzee azungumzia uhitaji huu pamoja na wahubiri wawili au watatu ambao wamevunjika moyo kwa sababu ya itikio dogo katika eneo linalorudiwa-rudiwa. Apitia pamoja nao Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1988, ukurasa wa 16-19, fungu la 4-14. Wanazungumzia kwa namna ya kutazamia mema njia za kutumia madokezo haya kwao.
Wimbo 191 na sala ya kumalizia.