Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Aprili na Mei: Andikisho la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi, toa magazeti yote mawili. Juni: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, au kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichotiwa ndani ya toleo la pekee kama vile Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?, Kumsikiliza Mwalimu Mkuu, Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya, Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani,” na Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa kweli. Julai na Agosti: Yoyote ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 zaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?, na Serikali Itakayoleta Paradiso. Broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia Au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa mahali panapozifaa. Vijitabu Wakati Ujao Salama—Jinsi Unavyoweza Kuuona na Roho Zisizoonekana—Je! Zinatusaidia? au Zinatuumiza? zaweza kutumiwa kulingana na toleo la pekee lililoonyeshwa katika barua kutoka ofisi ya tawi.
◼ Wanapohubiri eneo lisilogawiwa, wahubiri wanaweza kutoa kitabu Ujuzi au broshua Anataka. Kichapo chochote chaweza kutolewa ikiwa mwenye nyumba ana vichapo hivi viwili tayari. Wote wanapaswa kubeba aina mbalimbali za trakti ili kuzitoa kwa wasiokuwako nyumbani au watu wasiokubali fasihi. Trakti Habari za Ufalme Na. 35 yoyote ambayo wahubiri au kutaniko huenda likawa nayo bado yapaswa waachiwe wenye nyumba. Jitihada zapasa kufanywa kufuatia kupendezwa, hasa pale ambapo eneo lisilogawiwa huenda likafanywa na mapainia wa pekee au kutaniko la karibu.
◼ Kukiwa na miisho-juma mitano, mwezi wa Mei ni wakati mzuri kwa wengi kufanya upainia-msaidizi.
◼ Beji za mkusanyiko za 1998 zitatiwa ndani ya agizo la fasihi moja kwa moja. Beji za ziada zikihitajiwa na kutaniko, zaweza kuombwa kupitia Fomu ya Kuomba Fasihi (S-14-SW). Inabidi kuagiza vifuko vya kuwekea beji kwa sababu ya yeyote kutanikoni anayevitaka.
◼ Toleo la Watchtower Library la 1997 katika CD-ROM limetayarishwa katika lugha tisa. Kwa mara ya kwanza, chombo hiki chenye thamani cha utafiti kitapatikana katika Kifaransa pia. Kitakuwa na vichapo vilivyotolewa kuanzia 1980 hadi 1997. Tarehe ya kuanzia ya vichapo ni 1970 kwa matoleo ya Kiingereza (Mnara wa Mlinzi kuanzia 1950). Vinatengenezwa katika nchi kadhaa, kwa hiyo maombi ya kuagiza ya matoleo ya lugha za kigeni yatatekelezwa vichapo hivyo vipatikanapo.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Mwimbieni Yehova Sifa—Chapa Kubwa (Maneno ya wimbo pekee) —Kiswahili
◼ Vichapo Vinavyopatikana:
Je! Uamini Utatu? —Kiswahili
Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi —Kiswahili
Mashahidi wa Yehova na Elimu —Kiswahili
Mungu Anataka Tufanye Nini? —Kikamba, Kikuyu
Insight on the Scriptures —Kiingereza
New World Translation of the Holy Scriptures (Deluxe; DLbi12), yenye jalada la rangi iliyo kama nyekundu —Kiingereza
New World Translation of the Holy Scriptures (Deluxe, toleo la mfukoni; DLbi25), yenye jalada jeusi —Kiingereza
◼ Kaseti Zinazopatikana:
Singing Kingdom Songs (kaseti moja) —Kiingereza
◼ Compact Disc Mpya Zinazopatikana:
Kingdom Melodies, Buku la 8
Singing Kingdom Songs—On Compact Disc (seti ya diski nane) —Kiingereza
◼ Vidiokaseti Mpya Zinazopatikana:
Siri ya Kupata Furaha ya Familia (Buku la 1) —Lugha ya Ishara ya Kimarekani
Siri ya Kupata Furaha ya Familia (Buku la 2) —Lugha ya Ishara ya Kimarekani