Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei
Juma Linaloanza Mei 4
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Roho ya Yehova Iko Nasi.” Maswali na majibu. Unaposhughulikia fungu la 3, tia ndani madondoo yafaayo kutoka katika kichapo 1998 Yearbook, ikiwa chapatikana.
Dak. 22: “Teua Makala za Kuvutia Mapendezi Hususa ya Watu.” Pitia mambo makuu katika makala hiyo. Eleza kwamba hata matoleo ya zamani ambayo yangali katika hali nzuri yaweza kutolewa kwa njia hii. Alika wahubiri wasimulie makala ambazo wametoa wakapata matokeo mazuri. Toa wonyesho wa utoaji ulio katika fungu la 7.
Wimbo 212 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 11
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 12: “Una Mipango Gani Likizo Ijayo?” Mzee azumgumza pamoja na wahubiri wawili au watatu kuhusu mipango yao ya miezi inayokuja ya likizo. Wanapitia uhitaji wa kujitayarisha mapema kuhudhuria mkusanyiko, kuongeza utendaji wao wa utumishi wa shambani, kwenda tafrija, na kutembelea marafiki na watu wa jamaa. Wote wakubali kwamba hawatapuuza funzo la kibinafsi, mikutano, au utumishi wa shambani na waeleza jinsi ambavyo wamepanga kudumisha kawaida nzuri ya kitheokrasi.
Dak. 25: Kupitia utendaji wa kutaniko wa kuongoza funzo la Biblia nyumbani kukifanywa na mwangalizi wa utumishi. Taja asilimia ya kutaniko ya idadi ya wahubiri wanaoongoza funzo la Biblia. Kisha shughulikia kwa maswali na majibu habari inayohusu mafunzo ya Biblia nyumbani kutoka katika kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, ukurasa wa 89 hadi 91. Tia moyo wote wajitahidi kuelekea kuongoza angalau funzo moja la Biblia na utoe madokezo yafaayo ya jinsi ya kupata funzo la Biblia nyumbani.
Wimbo 48 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 18
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Tangaza mipango ya pekee ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.
Dak. 15: “Je, Una ‘Mwiba Katika Mwili’”? Maswali na majibu. Toa maelezo kuhusu “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1987, ukurasa wa 29.
Dak. 22: Epuka Kuishi Maisha Maradufu. Hotuba itolewe na mzee inayotegemea makala “Vijana—Je! Mtaupita Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu wa Kikristo?” kutoka Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1991, ukurasa wa 19-21. Malizia kwa kupongeza vijana ambao wamedumu wakiwa vielelezo bora katika adili zao kwa kutafuta kibali cha Mungu badala ya kile cha marika wao, wajapokua katika ulimwengu huu usio na adili.
Wimbo 139 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: Sababu Inayonifanya Nithamini Mikutano ya Kutaniko. Mzee aongoza mazungumzo akiwa na kikundi cha wahudhuriaji wa kawaida kinachowakilisha kutaniko, labda kutia ndani wenzi waliooana, mtu mzee-mzee, na tineja. Wanaeleza sababu inayowafanya wahudhurie sikuzote: ushirika mzuri, maagizo ya kimungu, na shauri zuri, linalowasaidia wakabiliane na matatizo ya kila siku na kuendelea kuwa wenye nguvu kiroho. Maelezo yakazia jinsi sisi sote tunavyobarikiwa kwa kuhudhuria mikutano kwa kawaida.
Wimbo 222 na sala ya kumalizia.