28,500!
Hiyo ndiyo idadi ya wahubiri ambayo tungependa kuona wakiripoti katika Afrika Mashariki mwezi wa Agosti 1998. Je, tuna uwezekano wa kuifikia? Ndiyo, bila shaka! Hesabu yetu ya sasa ya makutaniko katika nchi 5 zilizo chini ya ofisi yetu ya tawi yaonyesha jumla ya wahubiri 28,660. Hata hivyo, kilele kisichopata kufikiwa ambacho kilipata kuripoti mwezi wowote ule mmoja kilikuwa 27,392, katika Agosti 1997. Twaweza kupitaje rekodi ya idadi hiyo? Hilo laweza kufanywa ikiwa kila mhubiri katika kutaniko atafanya mipango ya kushiriki katika huduma wakati wa Agosti na kutoa ripoti ya utendaji huo bila kukawia. Kwa kuwa siku za kwanza za mwezi huo ni Jumamosi na Jumapili, kwa nini usifanye mipango ya kushiriki katika utumishi wa shambani kuanzia mwisho-juma huo? Ikiwa utakuwa ukihudhuria kusanyiko, huenda ukaweza kutoa ushahidi wa vivi-hivi na kushiriki katika utumishi wa shambani wa kutaniko mwisho-juma unaofuata. Kwa kuanza mapema katika mwezi, hatutashindwa kutumia wakati fulani katika kazi ya kutoa ushahidi wakati wa Agosti. Kwa jitihada ya pamoja, twapaswa kuona kilele kipya kisichopata kufikiwa cha wahubiri kinachopita 28,500 kwa mara ya kwanza katika Afrika Mashariki. Hiyo itakuwa shangwe kuu ya sifa kwa Yehova kama nini!—Zab. 47:1.