Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/98 uku. 4
  • Mapainia Wasaidia Wengine

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapainia Wasaidia Wengine
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwathamini Mapainia Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Kutoa Utegemezo kwa Mapainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Saidia Wengine Wawe Stadi Katika Kutumia Neno la Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Njia za Kupanua Huduma Yako
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 9/98 uku. 4

Mapainia Wasaidia Wengine

1 Yesu alisema: “Kwa kweli, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana-mkubwa wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” Kwa kuwa wavunaji wa karne ya kwanza walikuwa wachache nao walikuwa na eneo kubwa la kuhubiri, Yesu angeweza kuwaelekeza wafikie watu wengi iwezekanavyo wakiwa na habari njema kwa kuwatuma wakiwa mmoja-mmoja. Badala yake, “a[li]watuma wawili-wawili.” (Luka 10:1, 2) Kwa nini wawili-wawili?

2 Wanafunzi hao walikuwa wapya na hawakuwa na uzoefu. Kwa kuhubiri pamoja wangeweza kufunzana na kutiana moyo. Kama vile Solomoni alivyosema, “afadhali kuwa wawili kuliko mmoja.” (Mhu. 4:9, 10) Hata baada ya roho takatifu kumwagwa kwenye Pentekoste 33 W.K., Paulo, Barnaba, na wengine waliandamana na waamini wenzao katika huduma. (Mdo. 15:35) Lazima liwe lilikuwa pendeleo kubwa kama nini kwa wengine kuzoezwa kibinafsi na wanaume wenye uwezo kama hao!

3 Programu Nzuri ya Mazoezi: Kama kifanani chake cha karne ya kwanza, kutaniko la Kikristo la kisasa ni tengenezo la kuhubiri. Pia hilo hutuandalia mazoezi. Tukiwa watu mmoja-mmoja, tamaa yetu ya moyoni yapaswa kuwa kutoa habari njema kwa matokeo iwezekanavyo. Ili wahubiri zaidi waweze kuboresha matokeo yao, usaidizi upo.

4 Kwenye Shule ya Huduma ya Ufalme iliyofanywa majuzi, Sosaiti ilitangaza programu ya mapainia kusaidia wengine katika huduma ya shambani. Je, kuna uhitaji wa kufanya hivyo? Ndiyo, kunao. Zaidi ya wahubiri milioni moja wamebatizwa katika miaka mitatu iliyopita, na wengi wao wanahitaji mazoezi ya kuwa wenye matokeo katika kazi yao ya kuhubiri. Ni nani anayeweza kutumiwa kutimiza uhitaji huo?

5 Mapainia wa wakati wote wanaweza kusaidia. Tengenezo la Yehova huwaandalia ushauri na mazoezi mengi. Mapainia hupokea maagizo yanayopatana na mahitaji yao katika Shule ya Utumishi wa Painia ya majuma mawili. Pia wao hunufaika na mikutano pamoja na waangalizi wa mzunguko na wa wilaya, na vilevile mwongozo utokao kwa wazee. Ijapokuwa si mapainia wote walio na uzoefu kama wa Paulo na Barnaba, wamepokea mazoezi yenye thamani, ambayo wanafurahi kuyashiriki na wengine.

6 Ni Nani Atakayenufaika? Je, kushiriki programu hii ni kwa wahubiri wapya au watu waliobatizwa karibuni tu? La hasha! Kuna wachanga na wenye umri mkubwa ambao wamejua kweli kwa miaka kadhaa lakini wangethamini msaada katika sehemu fulani za huduma. Wengine hufanya vizuri zaidi katika kuangusha fasihi lakini wana ugumu wa kufanya ziara za kurudia au kuanzisha mafunzo ya Biblia. Wengine huenda wakaanzisha mafunzo ya Biblia kwa urahisi lakini wanaona wanafunzi wao hawafanyi maendeleo. Ni nini kinachowazuia? Mapainia wenye uzoefu wanaweza kuombwa wawasaidie katika sehemu hizo. Mapainia fulani ni wenye matokeo katika kusitawisha kupendezwa, kuanzisha mafunzo ya Biblia, na kuelekeza wanafunzi wapya kwenye tengenezo. Uzoefu wao utasaidia katika programu hii mpya.

7 Je, wewe huona kwamba ratiba yako haikuruhusu kutegemeza kwa ukawaida mikutano ya kutaniko ya utumishi wa shambani jinsi ambavyo ungependa? Painia aweza kuhubiri nawe nyakati nyingine wahubiri wengine wanapokuwa hawapatikani.

8 Ushirikiano Mzuri Wahitajiwa: Mara mbili kwa mwaka wazee watafanya mipango kwa wahubiri ambao wangependa msaada wa kibinafsi washiriki katika programu ya Mapainia Wasaidia Wengine. Ukikubali kupata msaada huo, shirikiana na mhubiri painia aliyegawiwa kukusaidia, pangeni ratiba inayotumika ya utumishi, na mwishikilie. Timizeni kila miadi. Mhubiripo pamoja, angalia njia zenye matokeo za kuhubiri habari njema. Changanua kwa nini mifikio mingine ni yenye matokeo. Chunguza madokezo ambayo huenda mhubiri painia akatoa ili kuboresha utoaji wako. Unapotumia mambo uliyojifunza, maendeleo yako katika huduma yatakuwa dhahiri, kwako na kwa wengine. (Ona 1 Timotheo 4:15.) Hubirini pamoja mara nyingi iwezekanavyo, mkishiriki katika sehemu zote za huduma, kutia ndani ushahidi wa vivi hivi lakini mkikazia sehemu yoyote ambayo yahitaji usaidizi wa kibinafsi.

9 Mwangalizi wa utumishi anapendezwa na maendeleo yatakayofanywa. Pindi kwa pindi, atauliza kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko aone jinsi unavyonufaika na programu hiyo. Mwangalizi wa mzunguko vilevile atakusaidia anapotembelea kutaniko.

10 Yehova ataka watu wake wazoezwe na ‘kuandaliwa vifaa kikamili kwa ajili ya kila kazi njema.’ (2 Tim. 3:17) Uone mpango wa Mapainia Wasaidia Wengine kuwa uandalizi mzuri wa kusaidia wale wenye tamaa ya kuboresha uwezo wao wa kuhubiri lile neno. Ukipata pendeleo la kushiriki, fanya hivyo kwa shukrani, unyenyekevu, na shangwe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki