Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/98 uku. 1
  • Lazima Wote ‘Walikubali Neno kwa Moyo Mkunjufu’!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Lazima Wote ‘Walikubali Neno kwa Moyo Mkunjufu’!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako wa Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Kutumia Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 11/98 uku. 1

Lazima Wote ‘Walikubali Neno kwa Moyo Mkunjufu’!

1 Mamilioni ya watu wanajifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Ili wastahili kupata uhai udumuo milele, lazima ‘walikubali neno kwa moyo mkunjufu,’ kama walivyofanya wale 3,000 waliojitoa na kubatizwa siku ya Pentekoste 33 W.K. (Mdo. 2:41) Hilo latufanya tuwe na daraka gani leo?

2 Twahitaji kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wasitawishe ujitoaji kwa Yehova. (1 Tim. 4:7-10) Kwa sababu hiyo, nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996, fungu la 20, yadokeza: “Wakati wote wa funzo, tafuta fursa za kujenga uthamini kwa sifa za Yehova. Onyesha hisia zako mwenyewe [zenye kina] kwa Mungu. Saidia mwanafunzi afikiri kuhusu kusitawisha uhusiano wenye uchangamfu na wa kibinafsi pamoja na Yehova.”

3 Ugumu Tunaokabili: Watu wengi, wakichochewa na dini isiyo ya kweli, wametosheka na aina ya ibada inayotia ndani wakati na jitihada ndogo, bila kutaka badiliko lolote halisi katika njia yao ya maisha. (2 Tim. 3:5) Ugumu tunaokabili ni wa kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia waone kwamba ibada ya kweli yatia ndani mengi zaidi ya kuwa tu wasikiaji wa neno la Mungu. Lazima watumie wanayojifunza maishani mwao. (Yak. 1:22-25) Ikiwa jambo fulani kuhusu mwenendo wao wa kibinafsi haukubaliki kwa Mungu, wanahitaji kutambua wajibu wao ‘kugeuka’ na kufanya yaliyo sawa kumpendeza yeye. (Mdo. 3:19) Ili kupata uhai wa milele, lazima ‘wajikakamue wenyewe kisulubu’ na kuchukua msimamo imara kwa ajili ya kweli.—Luka 13:24, 25.

4 Mnapozungumzia sehemu mbalimbali za adili, mwulize mwanafunzi wako wa Biblia jinsi kwa kweli anavyoona mambo haya na kile anachopaswa kufanya akiona uhitaji wa kufanya mabadiliko katika maisha yake. Elekeza uangalifu wake kwenye tengenezo ambalo kupitia hilo anajifunza kweli, nawe umtie moyo ahudhurie mikutano ya kutaniko kwa ukawaida.—Ebr. 10:25.

5 Na tufanye liwe lengo letu kufikia moyo wa mwanafunzi kupitia kufundisha kwetu. Tutashangilia tuchocheapo wapya wakubali neno la Mungu kwa moyo mkunjufu na kubatizwa!—1 The. 2:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki