Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/98 uku. 1
  • Jenganeni kwa Kutoa Maelezo Mikutanoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jenganeni kwa Kutoa Maelezo Mikutanoni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Wasaidie Wapya Watoe Maelezo Mikutanoni
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Tianeni Moyo Katika Mikutano ya Kutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Msifu Yehova ‘Katikati ya Kutaniko’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 11/98 uku. 1

Jenganeni kwa Kutoa Maelezo Mikutanoni

1 Kwenye Waebrania 10:24 twahimizwa ‘tuchocheane kwenye upendo na kazi zilizo bora.’ Hilo latia ndani kujengana kwa kutoa maelezo yenye maana kwenye mikutano ya kutaniko. Kwa nini tutoe maelezo? Twaweza kufanyaje hivyo? Ni nani mwenye kunufaika?

2 Fikiria mara nyingi ambazo unanufaika kutokana na kusikia wengine wakitoa maelezo sahili, yaliyo waziwazi ambayo huboresha uelewevu wako na kukuimarisha kiroho. Una pendeleo la kufanyia wengine vivyo hivyo. Unaposhiriki, waonyesha tamaa yako ya “kuwapa baadhi ya zawadi ya kiroho” kwa kuwatia moyo wote wanaohudhuria.—Rom. 1:11, 12.

3 Jinsi ya Kutoa Maelezo Mazuri: Usitoe maelezo marefu, ukieleza kila wazo katika fungu. Maelezo marefu kwa kawaida hukosa kukazia jibu mahususi na huenda yakawazuia wengine kushiriki. Elezo la kwanza la fungu lapaswa kuwa fupi, likiwa jibu la moja kwa moja kwa swali lililochapwa. Wale wanaotoa maelezo ya ziada wanaweza kueleza matumizi yanayofaa ya habari hiyo au kuonyesha jinsi maandiko yanavyoweza kutumiwa. Ona kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 90-92.

4 Ikiwa una wasiwasi kutoa maelezo, tayarisha maelezo mafupi mapema, na umwombe mwenye kuongoza akuite mfikiapo fungu hilo. Baada ya kufanya hivi kwenye mikutano michache, itakuwa rahisi zaidi kushiriki. Kumbuka kwamba Musa na Yeremia walieleza ukosefu wa uhakika katika uwezo wao wa kusema hadharani. (Kut. 4:10; Yer. 1:6, kielezi-chini katika New World Translation—With References) Lakini Yehova aliwasaidia waseme kwa niaba yake, naye atakusaidia pia.

5 Ni Nani Atakayenufaika na Maelezo Yako? Wewe mwenyewe wanufaika kwa sababu maelezo yako hukazia kweli kwa imara zaidi katika akili na moyo wako, yakifanya iwe rahisi zaidi kukumbuka habari hiyo baadaye. Pia, wengine hunufaika kwa kusikia maelezo yako yenye kujenga. Twatiwa moyo wakati ambapo watu wote, wawe wazoefu, wachanga, wenye haya, au wapya, wanajitahidi kueleza imani yao kwenye mikutano ya kutaniko.

6 Kwa hakika tutaona kwamba ‘maneno yanenwayo wakati wa kufaa ni mema kama nini’ yanapotumiwa kujengana mikutanoni!—Mit. 15:23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki