Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Novemba 2
  • Juma Linaloanza Novemba 9
  • Juma Linaloanza Novemba 16
  • Juma Linaloanza Novemba 23
  • Juma Linaloanza Novemba 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 11/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba

Juma Linaloanza Novemba 2

Wimbo 38

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Eleza juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Julai ya nchi na ya kutaniko lenu.

Dak. 15: “Lazima Wote ‘Walikubali Neno kwa Moyo Mkunjufu’!” Maswali na majibu. Tia ndani madokezo ya ziada kutoka katika nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996, fungu la 21.

Dak. 20: “Nataka Funzo la Biblia!” Mazungumzo na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Eleza jinsi jitihada hiyo ya pamoja ya kufanya ziara za kurudia itakavyopangwa kwenu. Kwa kadiri iwezekanavyo, wahubiri wenye uzoefu wanaweza kuhubiri na wapya. Vikundi vyapaswa kuwa vidogo ili ziara nyingi zifanywe. Pitia madokezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Aprili 1998, fungu la 12-15. Panga mhubiri mwenye uwezo atoe wonyesho wa jinsi ya kuanzisha funzo kwenye ziara ya kurudia. Tia moyo kila mtu ajitahidi kuanzisha funzo jipya.

Wimbo 35 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 9

Wimbo 187

Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Sanduku la Swali.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Tia ndani “Kikumbusha” kilicho katika nakala hii ya Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 17: “Jenganeni kwa Kutoa Maelezo Mikutanoni.” Maswali na majibu. Eleza jinsi ambavyo kutoa maelezo huongeza maendeleo yetu ya kiroho. (Ona kitabu Kiongozi cha Shule, somo la 38, fungu la 4.) Alika wengine wasimulie jinsi ambavyo walishinda hali ya kusitasita kutoa maelezo na jinsi ambavyo wamebarikiwa kwa kushiriki mikutanoni.

Wimbo 51 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 16

Wimbo 182

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Eleza mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.

Dak. 20: “Waangalizi Wanaoongoza—Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Pitia kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 10-11, fungu la 6-12.

Dak. 17: “Uwe Mwenye Matokeo Katika Huduma Yako.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya fungu la 1-7 katika nyongeza. Kazia mambo ambayo huenda yakatumika hasa katika eneo la kwenu.

Wimbo 167 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 23

Wimbo 89

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Simulia mambo yaliyoonwa yaliyochapishwa kwenye ukurasa wa mwisho wa Amkeni!, Agosti 8, 1998, kuhusu uvutano ambao kitabu Mtu Mkuu Zaidi kinacho kwa watu. Wahubiri wote wapaswa kuwa chonjo kutoa kitabu hiki katika pindi zinazofaa.

Dak. 17: “Uwe Mwenye Matokeo Katika Huduma Yako.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya fungu la 8-21 katika nyongeza. Kazia mambo ambayo huenda yakatumika hasa katika eneo la kwenu.

Dak. 20: Madokezo ya Kuboresha Usomaji Wako wa Biblia. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 1995, ukurasa wa 16-17. Kazia manufaa za kiroho zinazotokana na kusoma Biblia kila siku. Pitia madokezo yaliyotolewa, na uzungumzie jinsi ya kuyatumia. Panga wahubiri wawili au watatu wasimulie jinsi wanavyonufaika na kusoma Neno la Mungu kwa ukawaida.

Wimbo 46 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 30

Wimbo 64

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti za utumishi wa shambani. Tia moyo wowote ambao hawakuanzisha funzo la Biblia Novemba waendeleze jitihada zao hadi Desemba, wakati kitabu Ujuzi kitatolewa pamoja na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Panga mhubiri mwenye uwezo atoe wonyesho wa ziara ya kurudia akitumia sanduku lililo kwenye ukurasa wa 19 katika kitabu Ujuzi; mhubiri aeleza jinsi kitabu hicho kinavyoweza kutumiwa kupata uelewevu wa mafundisho ya Biblia na kuanzisha funzo.

Dak. 15: Tumia Vizuri Kalenda ya Mashahidi wa Yehova. Hotuba. Pitia sehemu za kalenda: (1) picha zenye kutokeza zinazoonyesha matukio na mafundisho makuu, (2) ratiba ya usomaji wa Biblia wa kila juma wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, (3) ratiba ya kila mwaka ya usomaji wa Biblia wa juma la kabla ya Ukumbusho, (4) taarifa ya mapitio ya kuandika yajayo, na (5) vikumbusha vya kushiriki kwa ukawaida katika utumishi wa magazeti. Zungumzia njia za kutumia nafasi iliyopo kuandika ratiba ya utumishi wa shambani, kuandika ripoti za utumishi na mipango ya kuhubiri na wengine, kuorodhesha migawo ya mikutano, kuandika vikumbusha vya ziara ya mwangalizi wa mzunguko na makusanyiko yajayo. Kuweka kalenda mahali palipo wazi nyumbani au kazini, kwaweza kutokeza fursa za kuanzisha mazungumzo ya Kimaandiko. Simulia jambo lililoonwa lililo katika Kitabu cha Mwaka cha 1988, ukurasa wa 8.

Dak. 15: Nufaika Kikamili na 1998 Yearbook. Baba apitia ukurasa wa 3-6, 31 na familia yake, akikazia matimizo ya ulimwenguni pote ya kitheokrasi ya mwaka uliopita. Fikiria manufaa zinazofurahiwa na familia kwa kusoma na kuzungumzia andiko la siku na sehemu za Yearbook pamoja wakati wa vyakula, mkiazimia kufanya hivyo mwaka wote.

Wimbo 121 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki