Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 7
  • Juma Linaloanza Desemba 14
  • Juma Linaloanza Desemba 21
  • Juma Linaloanza Desemba 28
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 12/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba

Juma Linaloanza Desemba 7

Wimbo 186

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi. Pia, “Tulipita Kile Kiwango cha 28,500!” Taja kuhusu ripoti ya utumishi wa shambani ya Agosti ya nchi na ya kutaniko la kwenu. Chochea azimio la wahubiri la kuwa katika utumishi wa shambani kwa ukawaida na kutoa ripoti bila kukawia mwisho wa kila mwezi.

Dak. 15: “Lazima Turudi Tena na Tena.” Maswali na majibu. Toa maelezo kifupi kuhusu Ezekieli 3:17-19, ukikazia daraka letu la kuendelea kutoa ujumbe wa onyo.

Dak. 20: “Kutoa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.” Ndugu azungumzia makala hiyo na wahubiri wawili au watatu wenye uwezo. Tia ndani mambo machache yanayofaa kutoka katika kitabu “Kila Andiko” ukurasa wa 327-331. Toa wonyesho wa jinsi ambavyo toleo la Desemba laweza kutolewa.

Wimbo 176 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 14

Wimbo 206

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Toa madokezo ya jinsi ya kuitikia kwa busara salamu za sikukuu za kilimwengu. Ikiwa kutaniko lina nakala za kitabu Mtu Mkuu Zaidi au Mwalimu Mkuu akibani, onyesha jinsi vinavyoweza kutumiwa kwa matokeo katika huduma wakati wa sikukuu za Krismasi. Eleza mipango ya pekee ya utumishi wa shambani kwa ajili ya Desemba 25 na Januari 1 mahali ambapo hakuna mikusanyiko.

Dak. 15: “Waangalizi Wanaoongoza—Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi.” Hotuba itolewe na kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi. Aeleza madaraka yake na jinsi ambavyo wote wanaohudhuria wanavyoweza kusaidia kufanya funzo liwe lenye kuchangamsha, lenye kuarifu, na lenye kujenga kiroho.—Ona Huduma Yetu, ukurasa wa 67.

Dak. 20: “Wanaweza Kuona Kwamba Sisi Ni Tofauti.” Maswali na majibu. Pitia kifupi kila sifa inayotufanya tuwe watu wa pekee. Onyesha jinsi ambavyo habari hii yaweza kutumiwa katika kuelekeza wapya katika tengenezo na kuwaonyesha jinsi ambavyo kweli hutokeza sifa za Kikristo katika wale wanaoishi kulingana nazo.

Wimbo 146 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 21

Wimbo 163

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ikiwa kutaniko lenu litabadili saa za kukutana mwaka mpya, toa kitia-moyo chenye fadhili ukiwasihi wote wadumishe kuhudhuria mikutano kwa ukawaida kutanikoni kwa saa zake mpya. Wakumbushe wahubiri wawajulishe wanafunzi wao wa Biblia na watu wengine wenye kupendezwa kuhusu mabadiliko yoyote. Tia moyo wahubiri wote wahifadhi nakala zao za kibinafsi za Huduma ya Ufalme Yetu, hasa nyongeza. Yaelekea tutakuwa tukizirejezea wakati ujao.

Dak. 12: Mahitaji ya kwenu na “Kikumbusha” kilicho katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1998 kuhusu kukamilisha Majumba ya Ufalme.

Dak. 25: “Jenga Maisha Yako Katika Msingi wa Utumishi wa Yehova.” Maswali na majibu. Hoji mseja na kichwa cha familia ambaye amefanikiwa kudumisha ratiba thabiti, iliyo ya kawaida katika huduma ya shambani kila juma. Panga waeleze mpango wa kibinafsi unaohitajiwa ili kutanguliza masilahi ya kiroho.

Wimbo 119 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 28

Wimbo 178

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Desemba. Onyesha vitabu vinavyopatikana katika kutaniko lenu kwa bei ya pekee kwa toleo la Januari. Tia moyo wahubiri wachukue kadhaa ili kuvigawanya mwisho-juma huu.

Dak. 15: “Nufaika na Programu ya 1999 ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Panga wahubiri kadhaa waeleze juu ya manufaa ambazo wamepata kutokana na kwenda sambamba na “Ratiba ya Kuongezea ya Usomaji wa Biblia” kila juma. Tia moyo wote wasome Neno la Mungu kila siku.

Dak. 20: “Maoni ya Mkristo Kuhusu Desturi za Mazishi.” Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea makala iliyo katika Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1998, ukurasa wa 20-24.

Wimbo 195 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki