Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Agosti: Broshua zozote zifuatazo zenye kurasa 32 zaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, na Serikali Itakayoleta Paradiso. Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Our Problems –Who Will Help Us Solve Them?, na Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli? zaweza kutolewa mahali panapozifaa. Septemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, pia vichapo vya toleo la pekee vinavyopatikana katika kutaniko vyaweza kutolewa. Oktoba: Toa maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi, toa nakala mojamoja za magazeti. Novemba: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Pia vichapo vya bei ya pekee vyaweza kupewa watu wenye kupendezwa na mafunzo ya Biblia ambayo tayari yana kitabu Ujuzi na broshua Anataka.
◼ Kuanzia Agosti 27, 1999, hadi Agosti 31, 1999, Sosaiti itakuwa ikihesabu fasihi zote zilizomo Betheli. Kwa sababu ya kuhesabu huku, hakuna maagizo yoyote ya fasihi ya kutaniko yatakayoshughulikiwa au yatakayochukuliwa siku hizo.
◼ Katika kila jamii nyakati mbalimbali wakati wa mwaka huu, kuna sikukuu za kilimwengu ambazo watoto hawaendi shuleni na wafanyakazi hawaendi kazini. Hizo ni fursa nzuri za kutaniko kushiriki zaidi katika huduma ya shambani. Wazee wapaswa kupangia kimbele pindi hizo na kujulisha kutaniko mapema kuhusu mipango inayofanywa kwa ajili ya kutoa ushahidi mkiwa kikundi wakati wa sikukuu.
◼ Makutaniko yapaswa kuanza kuagiza 2000 Calendar of Jehovah’s Witnesses pamoja na ombi lao la fasihi la Septemba. Kalenda zitapatikana katika Kiarabu, Kichina, Kifaransa, na Kiingereza.