Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/99 kur. 3-6
  • Ibada ya Kweli Yapanuka Katika Ulaya Mashariki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ibada ya Kweli Yapanuka Katika Ulaya Mashariki
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Unasonga Mbele
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Upanuzi wa Haraka Wahitajiwa kwa Sababu ya Ongezeko Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Ujenzi wa Kimataifa wa Majumba ya Ufalme Katika Nchi Fulani za Ulaya
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kazi ya Ujenzi Inayomletea Yehova Sifa
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 9/99 kur. 3-6

Ibada ya Kweli Yapanuka Katika Ulaya Mashariki

1 Wakristo wa karne ya kwanza walikuwa wahubiri wa Ufalme wenye bidii. Walishangilia makutaniko ‘yalipoongezeka idadi siku baada ya siku.’ (Mdo. 16:5) Kuhubiri kwao kwa ujasiri kulifanya ibada ya kweli ifike Asia, Afrika, na Ulaya, kukitokeza mavuno mengi ya waamini.

2 Wakati huu wa mwisho, ibada ya kweli yaendelea kupanuka katika nchi za Ulaya Mashariki. Katika nchi ambako tulikuwa chini ya vizuizi vya serikali hadi miaka ya mapema ya 1990, sasa twaona maongezeko yenye kutokeza. Kichapo 1999 Yearbook chaonyesha kwamba mbili kati ya nchi hizo, Urusi na Ukrainia, kila moja ya ripoti wahubiri zaidi ya 100,000 wanaoshiriki katika huduma ya hadharani. Katika maeneo 15 ya ule uliokuwa Muungano wa Sovieti, tangu 1991 zaidi ya watu 220,000 wamejiweka wakfu kwa Yehova na kubatizwa! Ukuzi huo wa haraka umefanya iwe lazima kujenga Majumba ya Ufalme mapya na Majumba ya Kusanyiko na vilevile kupanua majengo kadhaa ya ofisi za tawi.

3 Kama ilivyotangazwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1997, sehemu ya Hazina ya Sosaiti ya Jumba la Ufalme sasa yatumiwa kutoa mikopo kwa makutaniko yaliyo katika nchi ambazo kuna uhitaji wa haraka sana wa Majumba ya Ufalme zaidi lakini ambapo hakuna fedha za kutosha na kuna matatizo makubwa ya kiuchumi. Kati ya Machi 1996 na Oktoba 1998, Sosaiti ilikubali maombi 359 ya mkopo wa Jumba la Ufalme kutoka katika ofisi za tawi zinazosimamia nchi 11 za Ulaya Mashariki. Fedha zilizochangwa zatumiwa kununua uwanja na vifaa vya ujenzi wa Majumba ya Ufalme mapya na kusaidia makutaniko yarekebishe majengo yaliyopo. Picha zinazoonyeshwa hapa zatudokezea jinsi michango kwa Hazina ya Sosaiti ya Jumba la Ufalme katika Marekani na nchi nyingine imenufaisha ndugu zetu katika Ulaya Mashariki.

4 Mwaka wa 1998, Bulgaria ilifurahia ongezeko la asilimia 12, na ndugu walisisimuka wakati Jumba lao la Ufalme la kwanza lilipowekwa wakfu katika Aprili mwaka huo. Kroatia ilifurahia ongezeko la asilimia 4, na wakati huu ndugu wa huko wanajenga Majumba ya Ufalme zaidi ili kusongeza mbele ibada ya kweli. Katika Hungaria Majumba ya Ufalme yapatayo 80 yanatumiwa na makutaniko 144. Hiyo yamaanisha kwamba kati ya makutaniko 235 katika nchi hiyo, asilimia 61 yana mahali pao penyewe pa ibada. Katika Makedonia programu ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme imekamilisha majumba mawili mapya, na mengi yangali yanajengwa. Katika kiangazi cha 1999, Jumba la Ufalme lenye majumba mawili lilikamilishwa katika jiji kuu la Skopje. Jumba hilo laweza kutumiwa na angalau makutaniko sita.

5 Mwaka jana katika Urusi, kwa wastani, watu 260 walibatizwa kila juma! Ikifuata kielelezo kinachotumika katika nchi nyingine, ofisi ya tawi ya Urusi sasa imepanga Halmashauri za Ujenzi za Kimkoa 12 kotekote katika eneo lao kubwa, ili kutegemeza miradi ijayo ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Sehemu ya kaskazini ya St. Petersburg, ujenzi wa Jumba la Kusanyiko la kwanza la nchi hiyo waendelea, ambalo litakuwa na nafasi ya watu 1,600. Jengo hilo pia litatia ndani Majumba ya Ufalme matano yenye nafasi ya watu 200 kila moja. Ili kutumikia mahitaji ya kiroho ya ndugu zetu na watu wengi wenye kupendezwa katika Ukrainia, Majumba ya Ufalme 84 yamekamilishwa na 80 yanaendelea kujengwa.

6 Je, ongezeko hilo katika Ulaya Mashariki halileti shangwe mioyoni mwetu? Hata tuwe twaishi wapi, upanuzi wa ibada ya kweli hutukumbusha kwamba Mungu si mwenye ubaguzi na kwamba subira yake itamaanisha wokovu kwa “umati mkubwa.” (Ufu. 7:9; 2 Pet. 3:9) Tuna pendeleo kama nini kushiriki sehemu ndogo katika kuchangia ukuzi wa kiroho wa wengine, hata wale wa nchi za mbali! Mithali 28:27 hutuhakikishia kwamba “mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu.” Utayari wetu wa kusaidia katika gharama hizi za ujenzi hutokeza “usawazisho” wa vitu vya kimwili, ukiwezesha wote wapate furaha itokanayo na kutoa na shangwe itokanayo na kuona ibada ya kweli ikipanuka ulimwenguni pote.—2 Kor. 8:14, 15; Mdo 20:35.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Săcele, Rumania

[Picha katika ukurasa wa 3]

Maardu, Estonia

[Picha katika ukurasa wa 3]

Sevnica, Slovenia

[Picha katika ukurasa wa 3]

Tiszavasvári, Hungaria

[Picha katika ukurasa wa 4]

Jūrmala, Latvia

[Picha katika ukurasa wa 4]

Tallinn, Estonia

[Picha katika ukurasa wa 4, 5 ]

Taurage, Lithuania

[Picha katika ukurasa wa 4, 5]

Belgrade, Yugoslavia

[Picha katika ukurasa wa 5]

Prievidza, Slovakia

[Picha katika ukurasa wa 5]

Mátészalka, Hungaria

[Picha katika ukurasa wa 6]

Vranov nad Topl’ou, Slovakia

[Picha katika ukurasa wa 6]

Ruma, Yugoslavia

[Picha katika ukurasa wa 6]

Tornakalns, Latvia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki