Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/99 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 9/99 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la fasihi la Septemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, pia vichapo vya toleo la pekee vinavyopatikana katika kutaniko vyaweza kutolewa. Oktoba: Toa maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi, toa nakala mojamoja za magazeti. Novemba: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Pia vichapo vya bei ya pekee vyaweza kupewa watu wenye kupendezwa na mafunzo ya Biblia ambayo tayari yana kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Desemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele pamoja na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

◼ Inafaa kwamba vikundi vya watu 20 au zaidi wanaopanga kutembelea majengo ya Sosaiti kwanza wawasiliane kwa barua na Ofisi ya Betheli. Tafadhali pelekeni habari kuhusu idadi ya watu wanaokuja na tarehe na saa za kutembelea ofisi ya tawi. Kabla hamjazuru, tafadhali pitieni Sanduku la Swali katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1998.

◼ Unapokuwa katika huduma, huenda ukakutana na kiziwi. Ikiwa kuna kikundi au kutaniko la lugha ya ishara katika eneo lenu, wapaswa kufuata mwelekezo ulio katika barua ya Sosaiti kwa makutaniko yote ya Oktoba 15, 1998. Hiyo yaeleza hivi: “Fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi itatumiwa kuandika majina ya watu, ambao wanasema lugha nyingine kutia ndani lugha ya ishara, wawe wanaishi katika eneo la kutaniko lenu au la. Kwa ujumla inapaswa kutumiwa kwa kusudi hili hata ikiwa mtu haonyeshi upendezi katika ujumbe wa Ufalme. . . . Baada ya kujaza fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi, yapasa kupatiwa mwandishi wa kutaniko moja kwa moja au iwekwe ndani ya sanduku la ripoti za utumishi wa shambani kwenye Jumba la Ufalme.” Kila mhubiri anapokuwa chonjo kushirikiana kwa njia hii, vikundi vya lugha ya ishara vitaweza kukusanya orodha ya viziwi walio katika eneo lao.

◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeagizwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hilo lifanywapo baada ya ripoti ya hesabu itakayofuata kusomwa.

◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyotolewa kwenye ukurasa wa 21-23 katika Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1991, kuhusu watu wowote waliotengwa au waliojitenga na ushirika ambao huenda wakawa na mwelekeo wa kurudishwa.

◼ Wale wanaoshirikiana na kutaniko wapaswa kupeleka maandikisho yote mapya na ya kufanywa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho yao ya kibinafsi, kupitia kutaniko.

◼ Sosaiti haishughulikii maagizo ya fasihi ya wahubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-msimamizi apaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla agizo la kila mwezi la kutaniko la fasihi halijapelekwa kwa Sosaiti ili wote ambao wangependa kujipatia fasihi za kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia fasihi. Tafadhali kumbuka ni vichapo gani ambavyo ni bidhaa za kuagizwa kipekee.

◼ Mikusanyiko ya Wilaya na wa Kimataifa ya 1998 “Njia ya Mungu ya Maisha” ilikuwa baraka kwelikweli kwa wote waliohudhuria. Miongoni mwa wale waliohudhuria walikuwa wamishonari 2,764 na watumishi wa kimataifa walioweza kutembelea nchi za nyumbani kwao kwa msaada wa upaji wenye ukarimu kutoka makutanikoni. Tegemezo la mpango huo lathaminiwa sana. Michango iliyotolewa kwa kusudi hilo, ambayo ilibaki baada ya mikusanyiko hiyo kumalizika, itatumiwa kutegemeza kazi ya kuhubiri ya ulimwenguni pote.

◼ Vichapo Vinavyopatikana:

Je, Kuna Muumba Anayekujali? —Kiingereza

Mungu Anataka Tufanye Nini? —Kiswahili

Ni Nini Hutupata Tunapokufa? —Kiingereza

Yehova—Yeye Ni Nani? (Trakti Na. 23) —Kiswahili

The Guidance of God—Our Way to Paradise —Kiingereza

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki