Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/02 kur. 3-6
  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Unasonga Mbele

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Unasonga Mbele
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Kudhihirisha Imani kwa Matendo Mema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Upanuzi wa Haraka Wahitajiwa kwa Sababu ya Ongezeko Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Ibada ya Kweli Yapanuka Katika Ulaya Mashariki
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Fungu Lako Katika Kujenga kwa Ajili ya Wakati Ujao
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 9/02 kur. 3-6

Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Unasonga Mbele

1 Kwenye Makusanyiko ya Wilaya ya “Umoja wa Ufalme” ya mwaka wa 1983 huko Marekani, ilitangazwa kwamba hazina ya pekee ingeanzishwa kwa ajili ya ujenzi na urekebishaji wa Majumba ya Ufalme kotekote Marekani na Kanada. Hatukujua wakati huo jinsi ambavyo mwanzo huo mdogo ungebarikiwa. Tulianza kuona utimizo wa maneno ya Zaburi 92:4: “Kwa kuwa umenifurahisha, BWANA, kwa kazi yako; nitashangilia kwa ajili ya matendo ya mikono yako.”

2 Sasa tunafurahia sana kuona kile kinachotimizwa. Majumba mengi ya Ufalme hujengwa duniani pote chini ya mpango huo leo. Sisi sote tuna pendeleo la kushiriki katika ujenzi huo kwa njia moja au nyingine. Tunafanya hivyo kwa kushiriki kwa kutoa michango mikubwa au midogo ili kusaidia kulipia gharama za ujenzi wa majengo zaidi ya ibada kotekote duniani. Ndugu wengi pia hujitolea kwa kutumia vifaa vyao, na vilevile wakati, vipawa, na stadi zao katika miradi hiyo. Mpango huo umefanikiwa kwa sababu Yehova ameongoza, kutegemeza, na kubariki jitihada zetu za pamoja.—Zab. 127:1.

3 Ofisi za tawi nyingi zimefuata utaratibu uleule uliotumiwa na makutaniko huko Marekani hapo awali. Kwenye Majumba ya Ufalme katika nchi nyingi, kuna sanduku la michango kwa ajili ya Hazina ya Majumba ya Ufalme ambamo wahubiri huweka michango yao. Rekebisho katika mradi huo wa ujenzi lilitangazwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1997 huko Marekani. Huduma hiyo ilisema: “Tangu Hazina ya Majumba ya Ufalme ya Sosaiti ilipoanzishwa mwaka wa 1983, akina ndugu wamechanga kwa ukarimu, na hivyo kuwezesha makutaniko kupata mikopo kwa ajili ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Katika nchi hii makutaniko 2,700 hivi yamekwisha pata mikopo. Jambo hilo limewezesha makutaniko mengi kujenga au kurekebisha Majumba yao ya Ufalme. Kwa sasa kuna uhitaji mkubwa wa kutumia kiasi fulani cha michango hiyo ili makutaniko katika nchi zenye hali ngumu ya kiuchumi yaweze kupata mikopo. Michango yenu inathaminiwa sana na Sosaiti na makutaniko yanayonufaishwa na mpango huo.”

4 Tangazo hilo lilikuwa mwito wa kuunga mkono ujenzi wa Majumba ya Ufalme mengi zaidi. Fedha za Hazina ya Majumba ya Ufalme hutumiwa kwa ajili ya mahitaji ya ndugu zetu katika nchi zote. Huko Marekani, makala nyingine katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 1997 ilisema hivi: ‘Kuna uhitaji wa kujenga Majumba ya Ufalme kotekote duniani. Makutaniko 3,288 yalianzishwa katika mwaka wa utumishi uliopita. Mengi ya makutaniko hayo mapya yako Afrika, Asia, Amerika ya Kati na ya Kusini, na Ulaya Mashariki.’

5 Kumekuwa na matokeo gani tangu wakati huo? Kitabu 2001 Yearbook kilisema hivi: “Hadi leo, mpango huo umetumiwa kujenga Majumba ya Ufalme 453 katika nchi 30, na majumba mengine 727 yanajengwa wakati huu. Imekaziwa kwamba kila nchi iwe na michoro hususa ya Majumba ya Ufalme inayofaa nchi hiyo kwa habari ya vifaa vya ujenzi na mbinu za kujenga. Nchini Kenya mawe yaliyochimbwa hutumiwa; nchini Togo matofali hutumiwa kwa kawaida; nchini Kamerun watu hupenda kujenga kwa matofali ya saruji. Kwa hiyo, ndugu wenyeji wanaweza kuzoezwa kwa haraka kufanya kazi hiyo na kusimamia ujenzi katika nchi zao.”

6 Baraka za Yehova juu ya mpango huu zinaonekana wazi katika bara kubwa la Afrika. Unapoangalia picha za baadhi ya Majumba ya Ufalme ambayo yamejengwa, wazia jinsi yanavyowasaidia Mashahidi wa Yehova katika kazi yao! Matokeo hayo mazuri yanaonekana katika sehemu tatu hasa—udugu wetu wa ulimwenguni pote umeimarishwa, watu katika ujirani wamevutiwa, na hudhurio kwenye mikutano ya makutaniko limeongezeka. Ijapokuwa nyongeza hii inaonyesha Majumba ya Ufalme yaliyojengwa Afrika, makala zinazokuja za Huduma Yetu ya Ufalme zitazungumzia ujenzi wa Majumba ya Ufalme unaoendelea katika sehemu nyingine duniani.

[Picha katika ukurasa wa 3]

JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

Bimbo, Bangui

Begoua, Bangui

[Picha katika ukurasa wa 4]

Ukonga, Tanzania

[Picha katika ukurasa wa 4]

Accra, Ghana

[Picha katika ukurasa wa 4]

Salala, Liberia

[Picha katika ukurasa wa 4]

Karoi, Zimbabwe

[Picha katika ukurasa wa 4, 5]

Allada, Benin—Jumba la Ufalme la zamani

Allada, Benin—Jumba la Ufalme jipya

[Picha katika ukurasa wa 5]

Kpeme, Togo

[Picha katika ukurasa wa 5]

Sokodé, Togo

[Picha katika ukurasa wa 5]

Fidjrosse, Benin

[Picha katika ukurasa wa 6]

Lyenga, Zambia—Jumba la Ufalme la zamani

[Picha katika ukurasa wa 6]

Lyenga, Zambia—Jumba la Ufalme jipya

[Picha katika ukurasa wa 6]

Kinshasa, Kongo

[Picha katika ukurasa wa 6]

Musambira, Rwanda

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki