Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Septemba 9
Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tumia madokezo kwenye ukurasa wa 8 na panga maonyesho mawili ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 15 na Amkeni! la Agosti 22. Katika kila moja ya maonyesho hayo, onyesha jinsi ya kujibu kizuia-mazungumzo “Sipendezwi na Mashahidi wa Yehova.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 17-18.
Dak. 17: “Kuwasaidia Wengine Wamtukuze Yehova.”a Wakati ukiruhusu, taja jambo moja au mawili katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 425-427.
Dak. 15: Kwa Nini Watu Hukosa Imani? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Nyakati nyingine sisi hukutana na watu wasio na imani. (2 The. 3:2) Ili kuwaeleza kweli kumhusu Yehova, kwanza tunapaswa kujitahidi kujua maoni yao kumhusu Mungu. Chunguza yale mambo manne yanayotajwa katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 92-93, ambayo yanaweza kumzuia mtu asiwe na imani. Omba wasikilizaji watoe madokezo ya jinsi ya kushughulikia kila moja ya hali hizo. Simulia jambo lililoonwa linaloonyesha njia nzuri ya kushughulikia hali hizo, au simulia lile lililomo katika toleo la Amkeni! la Agosti 22, 1993, ukurasa wa 14-15.
Wimbo 122 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 16
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Watie moyo wote warudie maandishi yao ya kusanyiko la mzunguko lililopita, wanapotayarisha Mkutano wa Utumishi wa juma linalofuata.
Dak. 18: Tulitimiza Nini Mwaka Uliopita? Hotuba hii itolewe na mwangalizi wa utumishi. Taja mambo mazuri katika ripoti ya kutaniko ya mwaka wa utumishi wa 2002. Wapongeze wote kwa yale yaliyotimizwa. Kazia kile ambacho kimetimizwa kuhusiana na hudhurio la mikutano, ziara za kurudia, mafunzo ya Biblia, na kile ambacho mapainia wasaidizi wametimiza. Kisha toa mapendekezo ya jinsi ya kufanya maendeleo. Weka miradi unayoweza kutimiza mwaka ujao.
Dak. 17: Matatizo Ambayo Wazazi Wasio na Wenzi wa Ndoa Hukabili. Mzee amhoji mzazi mmoja au wawili wasio na wenzi (au wazazi ambao wana wenzi ambao si Mashahidi) ili kujua jinsi wanavyoshughulikia matatizo ya kuwazoeza watoto wao, kuwatia nidhamu, na kuwaongoza kiroho. Wanafanya nini ili waweze kuwatunza watoto wao na pia kuhudhuria mikutano na kushiriki katika utumishi wa shambani kwa ukawaida? Kazia madokezo kadhaa yanayoonyeshwa katika kitabu Furaha ya Familia, ukurasa wa 104-110. Kama inavyoonyeshwa kwenye ukurasa wa 113-115, taja jinsi wengine wanavyoweza kusaidia.
Wimbo 149 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Panga mzee aonyeshe jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1 na mtumishi wa huduma aonyeshe jinsi ya kutoa gazeti la Amkeni! la Septemba 8, kwa kutumia madokezo kwenye ukurasa wa 8. Baada ya kila onyesho, rudia sentensi ya kwanza au sentensi mbili za kwanza zilizotumiwa ili kufanya mwenye nyumba apendezwe.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 25: “Hofuni Mungu na Kumpa Utukufu.” (Ufu. 14:7) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji ili kurudia programu ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi uliopita. Omba ndugu na dada watoe maelezo juu ya mambo makuu waliyojifunza na jinsi walivyoweza kuyatumia katika maisha yao wenyewe, au kama familia. (Sehemu zinaweza kugawiwa mapema.) Kazia hotuba hizi: (1) “Wasaidie Wapya Wasitawishe Hofu Kumwelekea Mungu.” Tunawezaje kuwasaidia watu wanaopendezwa waliohudhuria Ukumbusho kufanya maendeleo ili wawe watumishi wa Yehova wenye bidii? (2) “Kumhofu Yehova Ni Kuchukia Lililo Baya.” (w87-SW 4/15 16-18) Andiko la Mithali 6:16-19 linawezaje kutusaidia kuacha mambo ambayo Yehova huchukia kama vile kiburi, kusema uwongo, kutafuta mali sana, burudani zisizofaa, na kutumia Internet kwa njia isiyofaa? (3) “Na Uwe na Uhusiano wa Karibu Zaidi na Wale Unaowapenda.” Tunampenda Yehova, Yesu, watu wa familia yetu, na wengine kutanikoni; kuwakaribia kunawezaje kutulinda na ulimwengu? (4) “Hofuni Yehova, Wala Si Wanadamu.” Kuhofu kumchukiza Yehova kumekusaidiaje kushinda haya unapohubiri, kufuata kanuni za Mungu kazini au shuleni, au kusimama imara mwajiri wako anapokushawishi ukose mikutano na makusanyiko? (5) “Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu.” (Zab. 119:37; Ebr. 4:13) Kwa nini kumhofu Mungu kunapaswa kutuzuia tusinywe vileo kupita kiasi, tusitazame picha chafu, au kufanya dhambi nyingine za siri? (6) “Endeleeni Kutembea kwa Kumhofu Yehova.” Yehova amekubariki jinsi gani unaporuhusu roho yake kutenda kazi kikamili zaidi katika maisha yako?—Zab. 31:19; 33:18; 34:9, 17; 145:19.
Wimbo 171 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 30
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za mwezi wa Septemba. Zungumzia “Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Unasonga Mbele.”
Dak. 15: Ni Nini Kinachofanya Magazeti Yetu Yawe ya Kipekee? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Toleo la mwezi wa Oktoba ni Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Zungumzia sababu magazeti yetu ni ya kipekee: (1) Yanatukuza jina la Yehova. (2) Yanajenga imani katika Yesu. (3) Yanatangaza Ufalme wa Mungu. (4) Yanaonyesha kwamba maoni ya Biblia ndiyo ya kweli. (5) Yanaeleza jinsi unabii wa Biblia unavyotimizwa. (6) Yanaeleza maana ya matukio ya ulimwengu. (7) Yanaonyesha jinsi ya kushughulikia matatizo ya siku zetu. (8) Yanavutia watu wa aina zote. (9) Hayaungi mkono upande wowote katika mambo ya siasa. Panga maonyesho mawili mafupi ili kuonyesha jinsi mambo mawili kati ya hayo yanavyoweza kutumiwa kuanzisha mazungumzo.
Dak. 15: “Onyesha Kwamba Unathamini Vichapo vya Biblia.”b Sehemu hii ishughulikiwe na mzee. Taja matatizo fulani ambayo huenda yameonekana kwenu kuhusiana na jambo hilo na onyesha jinsi kutaniko lenu linavyoweza kutumia vichapo kwa hekima. Himiza wote waagize vichapo wanavyohitaji tu. Kumbuka pendeleo letu la kutoa michango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote.
Wimbo 21 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 7
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Kuchukua Msimamo Imara Upande wa Kweli Shuleni. Hoji mhubiri mmoja au wawili vijana ambao huenda shule na wanaotambua kwamba ni lazima wapunguze ushirikiano pamoja na wanashule wenzao wasioamini. Wanapanga kushughulikia jinsi gani matatizo na vishawishi vinavyosababishwa na sherehe za kizalendo, dansi za shuleni, michezo ya ziada, mikutano ya harakati mbalimbali, na mwenendo usio wa maadili? Taja pia jinsi ambavyo wamepanga kutoa ushuhuda shuleni.
Dak. 20: “Epuka Kufuatia ‘Mambo ya Upuzi.’”c Baada ya kuzungumzia fungu la 4, taja mambo mbalimbali yanayozungumziwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1999, fungu la 30-32. Fungu la 5 linapozungumziwa, tia ndani maelezo kutoka katika sanduku lililomo katika Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1994, ukurasa wa 8. Fungu la 6 linapozungumziwa, soma fungu la 18 katika nyongeza ya Novemba 1999.
Wimbo 105 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Baada ya maneno ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, zungumzia sehemu hii kwa kutumia maswali na majibu.
b Baada ya maneno ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, zungumzia sehemu hii kwa kutumia maswali na majibu.
c Baada ya maneno ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, zungumzia sehemu hii kwa kutumia maswali na majibu.