Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba
Juma Linaloanza Novemba 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 15: “Kuhubiri Hutufanya Tuwe Tofauti.” Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Ukitumia kitabu Ujuzi, ukurasa wa 173, fungu la 8, simulia kifupi jambo tunaloweza kusema ili kumtia moyo mwanafunzi wa Biblia afikie hatua ya kushiriki katika huduma.
Dak. 20: “Ni Nani Ambaye Huenda Akakubali Funzo la Biblia?” Hotuba na maonyesho. Kupatana na fungu la 4, dokeza njia mbalimbali za kuchochea kupendezwa katika kujifunza yale yaliyo katika vichapo vyetu. Panga uwe na maonyesho mawili mafupi yakionyesha jinsi hilo linavyoweza kufanywa. Omba wasikilizaji wasimulie jinsi ambavyo wamepata mafanikio katika kuanzisha mafunzo.
Wimbo 198 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 8
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Toa utangulizi kwa ajili ya sehemu inayofuata ya programu ambayo itazungumzia barua ya Oktoba 15, 1999, Kwa Makutaniko Yote.
Dak. 30: Mwangalizi-msimamizi atoa muhtasari mfupi wa fungu la kwanza la barua ya Oktoba 15, 1999, Kwa Makutaniko Yote. Kisha mwandishi amwuliza mwangalizi-msimamizi kila moja la maswali hayo. Mwangalizi-msimamizi apaswa kusoma kila jibu moja kwa moja kutoka katika barua. Mwandishi wa kutaniko amalizia kwa muhtasari wa dakika mbili juu ya ile sehemu yenye kichwa, “Kila Mmoja Apaswa Kuuonaje Mpango Huu Mpya?” Toa utangulizi kwa ajili ya sehemu inayofuata, ambayo itaonyesha jinsi fasihi zapasa kutolewa shambani.
Dak. 10: Mwangalizi wa utumishi atashughulikia sehemu hii. Apaswa kuwa amesoma kwa makini barua ya Oktoba 15, 1999, Kwa Makutaniko Yote. Wahubiri wenye uzoefu au mapainia wapaswa kutoa maonyesho yaliyotayarishwa na kufanyiwa mazoezi vizuri.
(Dak. 2) Mwangalizi wa utumishi akazie kwamba matayarisho zaidi yatahitajiwa wakati ujao ili wote wazoee jinsi ya kutoa fasihi na magazeti, na pia jinsi mtu anavyoweza kumwuliza kwa busara mtu mwenye kupendezwa ikiwa angependa kuchangia kazi ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova. Tia moyo kutaniko lisikilize kwa makini maonyesho matatu yanayofuata na kuandika mambo makuu.
(Dak. 2) Mhubiri au painia amtolea kitabu cha Ujuzi mwenye nyumba ambaye ameonyesha upendezi wa kweli katika mazungumzo ya Biblia. Mhubiri huyo aweza kusema hivi: “Mashahidi wa Yehova ni wafanyakazi wa kujitolea ambao wanaona kwamba ni muhimu watu wanaomhofu Mungu wapate habari njema. Michango ya hiari inayotolewa na Mashahidi wa Yehova na watu wengine wanaoona thamani ya elimu ya Biblia leo husaidia kutegemeza kazi hiyo na kutuwezesha kutoa kitabu hiki bila malipo kwa watu ambao kwa kweli wanapendezwa kujifunza juu ya mambo ambayo Mungu amewawekea wanadamu akiba.” Mwenye nyumba auliza: “Wamaanisha kwamba naweza kupata kitabu hiki?” Mhubiri ajibu: “Naam waweza, ikiwa kwa kweli wapendezwa na ujumbe ulio katika Biblia. Nami ningependa kurudi tena na kujadiliana nawe zaidi baadhi ya habari hizi. Ukipenda kutoa mchango mdogo wa kuendeleza kazi hii ya elimu ya Biblia, waweza kufanya hivyo. Mchango wako utathaminiwa na kutumiwa wote ili kusongeza mbele habari njema ya Ufalme.” Mwenye nyumba atoa mchango naye mhubiri au painia amruhusu auweke moja kwa moja kwenye bahasha iliyotengwa kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote.
(Dak. 2) Tumia onyesho hilohilo, ukionyesha jinsi mhubiri angeweza kutoa kitabu Ujuzi, ampe mwenye nyumba, kisha aulize ikiwa angetaka kuchangia kazi ya ulimwenguni pote. Wakati huu mwenye nyumba asema, “Sidhani nitakisoma kitabu hiki.” Mhubiri akichukua kitabu kutoka kwa mwenye nyumba na kusema: “Nitampa mtu mwingine atakayefurahia kusoma kitabu hiki. Kwa sasa huenda trakti hii ikakupendeza.”
(Dak. 2) Mhubiri au painia huyohuyo aonyesha jinsi ya kutoa magazeti ya karibuni zaidi. “Habari ya asubuhi. Jina langu ni ______. Nimekuja kukuletea habari fulani zenye thamani sana juu ya [taja habari au kichwa]. Nilifurahia hoja hii. [Onyesha hoja hususa au utoe kielelezo fulani.] Ilinisaidia [simulia ulivyonufaika], nami nafikiri wewe utaifurahia pia. Ikiwa utalisoma gazeti hili, nitafurahi kukuachia.” Mwenye nyumba auliza “Magazeti haya ni bei gani?” Mhubiri au painia ajibu, “Fasihi zetu hazitozwi, lakini ikiwa ungependa kutoa mchango mdogo kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote ya elimu ya Biblia, tutafurahi kuukubali.” Mwenye nyumba atoa mchango naye mhubiri au painia amruhusu auweke moja kwa moja kwenye bahasha iliyotengwa kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote.
(Dak. 2) Mwangalizi wa utumishi awakumbusha wahubiri watumie fasihi kwa busara na kueleza kwa busara mpango wa kutoa michango kwa watu wanaoonyesha upendezi wa kweli na wanaochukua fasihi. Ili ziwe na manufaa halisi, lazima watu wanaotafuta kweli, yaani, wale wanaopendezwa na ujumbe wetu na kazi yetu wapewe fasihi. Kwa kawaida hilo huamuliwa wakati wa ziara ya kwanza. Wahubiri hawapaswi kuepuka kutoa fasihi. (Mt. 10:11) Kwa upande mwingine, twapaswa kuepuka kuwapa fasihi ovyoovyo watu ambao hawajaonyesha kwamba wanathamini kikweli ujumbe wa Biblia. Taja kwamba huenda baadhi ya wahubiri wachanga wakahitaji kuhubiri pamoja na wazazi wao katika huduma ya nyumba hadi nyumba mpaka wawe stadi wa kuzungumza na wenye nyumba. Wahubiri wapya na wasio na uzoefu wapaswa kuhubiri na wale wawezao kuwafundisha jinsi ya kutumia utoaji huo kisha kuwaeleza kikamili juu ya utaratibu uliorahisishwa wa kugawanya fasihi. Kwa kuendeleza huduma hivyo, kazi ya kuhubiri yaweza kukaziwa zaidi nasi tutaweza kutambua waziwazi zaidi watu wanaoonyesha upendezi wa kweli. Tunalohangaikia sana ni kupata na kulisha kondoo za Bwana na kuwasaidia wawe tayari kuokoka na kuingia katika ulimwengu mpya wa Yehova. Kwenye Mikutano ya Utumishi ya wakati ujao ambapo fasihi au magazeti yatatolewa, maonyesho yapaswa kutia ndani jinsi mtu anavyotambua iwapo upendezi unaoonyeshwa wastahili kuacha fasihi. Mhubiri huyo pia apaswa kuonyesha jinsi ya kujulisha umma kwamba michango inakubaliwa ili kusaidia katika kazi ya ulimwenguni pote.
Wimbo 208 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 15
Dak. 8: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: “Matumizi ya Internet—Uwe Chonjo Kuhusu Hatari Zake!” Mazungumzo ya maswali na majibu ya fungu la 1-18. Soma fungu la 4-7, 12, 16, 17. Tia moyo wote wajitayarishe vizuri kwa ajili ya mazungumzo ya juma linalofuata ya fungu la 19-36.
Dak. 17: Wazazi—Je, Mnaongoza Funzo la Familia kwa Ukawaida? Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Eleza kwa nini familia zahitaji kujifunza pamoja. (Ona kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 37-38.) Zungumzia vizuizi vifuatavyo vya funzo la familia: (1) kuhisi kwamba watoto ni wachanga mno kuweza kunufaika, (2) kufikiria kwamba kuhudhuria mikutano ya kutaniko tu kwatosha, (3) kuchoka kwa sababu ya ratiba zenye shughuli nyingi, na (4) kukengeushwa na kutazama televisheni. (Ona Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1994, ukurasa wa 11-12.) Omba walio vichwa vya familia wasimulie jinsi walivyoshinda vizuizi ili kudumisha funzo la familia la ukawaida. Kazia kwamba hilo huhitaji jitihada, azimio, na ushirikiano.
Wimbo 217 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 22
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Sanduku la Swali. Iwe hotuba. Eleza mipango ya kwenu ya kuendeleza Jumba la Ufalme lenu likiwa safi na katika hali nzuri.
Dak. 15: “Utamwambia Nini Mwislamu?” Maswali na majibu. Kazia uhitaji wa utambuzi unapoongea na watu wa utamaduni mwingine. Toa wonyesho wa utoaji uliotayarishwa vizuri. Ili upate habari zaidi juu ya Uislamu, ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1998; kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 23-24; na Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, sura ya 12.
Dak. 18: “Matumizi ya Internet—Uwe Chonjo Kuhusu Hatari Zake!” Mazungumzo ya maswali na majibu ya fungu la 19-36. Soma fungu la 23-25 na 34-36.
Wimbo 223 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Novemba.
Dak. 15: Tia Moyo Wapya Wahudhurie Mikutano. Mazungumzo kati ya mzee na mtumishi wa huduma mmoja au wawili, yakitegemea broshua Kufanya Mapenzi ya Mungu, ukurasa wa 14-15. Zungumzeni juu ya sababu zinazoonyesha umuhimu wa wapya kuhudhuria mikutano. Wakiwa huko watapokea sehemu kubwa zaidi ya mafundisho, kitia-moyo, na usaidizi. Zungumzeni juu ya mikutano mitano ya kila juma, mkieleza manufaa za kila mkutano. Zungumzeni juu ya jinsi ambavyo mikutano huendeleza mwenendo wa kimungu, huimarisha hali ya kiroho, hutuvuta kwenye tengenezo, hutusaidia kuwa na uhusiano wa karibu na wengine, na kutusaidia tuelewe kusudi la huduma yetu. Tia moyo wasikilizaji watumie broshua hiyo kuchochea wapya waje kwenye mikutano.
Dak. 20: Uchaguzi Wetu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Hotuba na maonyesho. Kati ya matengenezo mengine ya kidini, letu ni la pekee kwa sababu twachapisha, twatumia, na kugawanya tafsiri ya Biblia iliyotolewa na waabudu watiwa-mafuta wa Yehova. Si kwamba twataka kupata faida za kifedha au kueneza itikadi za kifarakano. Badala yake, tunachochewa na tamaa ya kuheshimu jina la Mungu na kusaidia wengine wapate kumjua vema. Tafsiri nyingine mara nyingi hueleza Neno la Mungu katika njia iliyo ngumu kuelewa, kwa hiyo zungumzia manufaa zilizo dhahiri za Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. (Ona “Kila Andiko,” ukurasa wa 327-331. Ona maelezo katika fungu la 3, taja vielelezo vya tafsiri iliyoboreshwa katika fungu la 6, na ukazie manufaa zilizo katika fungu la 22-23.) Panga kuwe na maonyesho mafupi mawili yanayodokeza jinsi tunavyoweza kuitikia wengine wanaposema, “Nyinyi mna Biblia yenu wenyewe.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 251-252.
Wimbo 205 na sala ya kumalizia.