Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/00 uku. 2
  • Ratiba Ya Mikutano Ya Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mikutano Ya Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Februari 14
  • Juma Linaloanza Februari 21
  • Juma Linaloanza Februari 28
  • Juma Linaloanza Machi 6
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 2/00 uku. 2

Ratiba Ya Mikutano Ya Utumishi

Juma Linaloanza Februari 14

Wimbo 113

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu. Panga painia au mhubiri mwenye uzoefu atoe wonyesho wa jinsi ya kutambua kupendezwa kabla ya kutoa kichapo katika mpango wa upaji wa hiari.

Dak. 15: “Lihubiri Neno . . . kwa Hima.” Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Tia ndani maelezo yaliyo katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 170. Toa madokezo kadhaa yenye kutumika ya kuonyesha jinsi ya kuongeza utendaji wa kuhubiri mwezi huu.

Dak. 20: “Jinsi ya Kusitawisha Uwezo wa Kutoa Sababu.” Hotuba na maonyesho. Eleza ni kwa nini uwezo wa kusababu ni wa maana sana katika huduma na ueleze jinsi ya kuupata. Panga wahubiri wawili wenye uwezo wazungumzie jinsi ya kujitayarisha kwa ajili ya huduma kwa kufuata hatua zinazoonyeshwa katika fungu la 3 la makala hiyo kisha watoe wonyesho wa utoaji wao.

Wimbo 182 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 21

Wimbo 17

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: “Wanawake Wanaofanya Kazi kwa Bidii Katika Bwana.” Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Tia ndani maelezo yaliyo katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1996, ukurasa wa 14-15, fungu la 18-19. Pongeza akina dada kwa uchangamfu kwa tegemezo lao la hiari, huduma zenye manufaa wanazowafanyia wengine, na kazi yao ya bidii ya kuhubiri.

Dak. 20: “Ni Nini Kinachoweza Kutusaidia Tusimame Imara Katika Imani?” Hotuba itolewe na mzee. Twaishi katika nyakati zenye hatari, na sisi sote twahitaji msaada kwa njia fulani. Zungumzia yale ambayo wazee na watumishi wa huduma wanaweza kufanya ili kuimarisha wale wanaosumbuliwa na matatizo yenye kuvunja moyo. (Ona kichwa kidogo “Uchungaji Unaojenga” katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1993, ukurasa wa 21-23.) Eleza jinsi tunavyoweza kutiana moyo katika njia ambazo zitatuimarisha kiroho.—Rom. 1:11, 12.

Wimbo 82 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 28

Wimbo 46

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti za utumishi za Februari. Chunguzeni kifupi “Hatua Nne Sahili” za kutumia trakti kuanzisha mazungumzo zilizoelezwa kwenye ukurasa wa 4 wa Huduma ya Ufalme Yetu ya mwezi uliopita. Toa wonyesho wa jinsi trakti Ulimwengu Mpya Wenye Amani inavyoweza kutumiwa kutoa utangulizi kwa kitabu Ujuzi. Baada ya kutokeza maswali hayo kutoka katika fungu la kwanza la trakti hiyo, soma fungu la kwanza kwenye ukurasa wa 3, kutia ndani Zaburi 37:29. Ikiwa kuna upendezi, fungua kitabu Ujuzi, ukurasa wa 5, soma sanduku, na mwulize kama angependa kujifunza. Mwezi huu, sote twapaswa kufanya jitihada ya kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani mapya.

Dak. 5: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.

Dak. 12: Kuthamini Kazi ya Halmashauri za Ujenzi za Mkoa. Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Agosti 1995. Halmashauri za Ujenzi za Mkoa 9 ambazo sasa zafanya kazi katika eneo la ofisi ya tawi ya Kenya zimesaidia kujenga, kurekebisha upya, na kudumisha Majumba ya Ufalme 106, yakinufaisha makutaniko 252. Bado kuna kazi nyingi ya kufanywa. Zungumzia kazi ya halmashauri za mkoa, na uchochee shauku kuelekea ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Eleza ni nani wanaoweza kustahili kuwa wafanyakazi wa kujitolea, na uchochee wengi zaidi wajitolee. Hoji watu fulani ambao wameshiriki katika mradi wa ujenzi wa Jumba la Ufalme, na katika maelezo yao waeleze shangwe ambayo wamepata.—Ona Mnara wa Mlinzi, Juni 1, 1999, ukurasa wa 18-19, fungu la 15-16.

Dak. 18: “Kuhubiri Habari Njema kwa Usadikisho Wenye Nguvu.” Toa utangulizi wa dakika mbili au tatu wa kutoka moyoni unaotegemea habari hiyo na vilevile maandiko yaliyotajwa na kunukuliwa katika fungu la 1 na la 2. Kisha zungumzia fungu la 3-12 kwa maswali na majibu.

Wimbo 61 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 6

Wimbo 116

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 10: Mahitaji ya kwenu. Tia ndani wonyesho wa jinsi ya kutoa toleo la vichapo katika mpango wa upaji wa hiari ukirejezea Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1999.

Dak. 10: “Kazia Uangalifu Jinsi Unavyosikiliza.” Kichwa cha familia azungumza pamoja na mke na watoto wake jambo wanaloweza kufanya ili kunufaika kikamili na mikutano ya kutaniko, makusanyiko, na mikusanyiko. Ahisi kwamba wote katika familia wanaweza kukaza fikira zaidi. Wapitia madokezo yaliyoorodheshwa na kuona jinsi wanavyoweza kutumia kila moja yao, kutia ndani uhitaji wa kuwa na mazungumzo zaidi kuhusu mambo waliyojifunza. Wanafikiria jinsi wanavyoweza kuishi kupatana na azimio lao la kutokosa mikutano yoyote au kipindi chochote cha mkusanyiko au kusanyiko ikiwa kwa vyovyote yawezekana.

Dak. 20: “Kuhubiri Habari Njema kwa Usadikisho Wenye Nguvu.” Baada ya pitio fupi la mazungumzo ya juma lililopita la mafungu ya kwanza 12 ya nyongeza, fanya mazungumzo ya maswali na majibu ya fungu la 13-24. Tumia uwezavyo maandiko yaliyonukuliwa na kutajwa.

Wimbo 186 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki