Sanduku La Swali
◼ Je, inafaa kupiga makofi kunapokuwa na tangazo la kurudishwa?
Yehova Mungu, kwa fadhili yake yenye upendo ameandaa njia ya Kimaandiko ya wakosaji wenye kutubu kupata tena kibali chake na kufikia kurudishwa katika kutaniko la Kikristo. (Zab. 51:12, 17) Hilo litukiapo, twatiwa moyo kuwahakikishia upendo wetu waliotubu kwa moyo mweupe.—2 Kor. 2:6-8.
Hata hivyo, ijapokuwa tuna shangwe sana mtu wa jamaa au rafiki au mtu tunayemfahamu anaporudishwa, kwapaswa kuwa na utulivu wenye adhama wakati tangazo la kurudishwa kwa mtu fulani linapotolewa katika kutaniko. Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1998, ukurasa wa 17, lilieleza mambo kwa njia hii: “Hata hivyo, ni lazima tukumbuke kwamba walio wengi kutanikoni hawafahamu hali hasa zilizofanya mtu aondoshwe au arudishwe. Kwa kuongezea, huenda kukawa na watu fulani ambao wameathiriwa au kuumizwa kibinafsi na kosa la mwenye kutubu, hali ambayo labda hata itadumu kwa muda mrefu. Kwa hiyo, kwa kuwa wana hisia nyepesi kuhusu mambo hayo, tangazo la kurudishwa litolewapo, kwa uelewevu tungejizuia na wonyesho mbalimbali wa ukaribishaji hadi tuwezapo kufanya hivyo kibinafsi.”
Ijapokuwa tuna furaha zaidi kuona mtu akirudi kwenye kweli, haitafaa kupiga makofi anaporudishwa.