Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/00 uku. 8
  • Je, Wewe Ni Mtangazaji wa Kawaida wa Ufalme?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Ni Mtangazaji wa Kawaida wa Ufalme?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Wewe Hutoa Ripoti Iliyo Sahihi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Ripoti Utumishi wa Shambani kwa Usahihi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Je, Agosti Utakuwa Mwezi Muhimu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Iweni wa Kawaida Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 4/00 uku. 8

Je, Wewe Ni Mtangazaji wa Kawaida wa Ufalme?

1 Sisi sote tulifurahi tulipojua kwamba kuna zaidi ya wahubiri 37,300 katika nchi sita zilizo chini ya ofisi ya Tawi ya Kenya kufikia Agosti 1999. Hiki ni kilele kikuu kuliko vyote. Hizo ni jitihada za muungano na zilizoazimiwa kwelikweli! Yaelekea baadhi ya wahubiri hao wamepata ugumu wa kuwa watangazaji wa kawaida wa Ufalme. Katika makutaniko mengine ukawaida umepungua kwa asilimia 86. Hiyo yaonyesha kwamba idadi kubwa ya wahubiri hairipoti huduma kila mwezi. Twaamini kwamba kitia-moyo kifuatacho chaweza kusaidia kurekebisha hali hiyo.

2 Thamini Pendeleo Hilo: Twapaswa kuthamini sana mapendeleo tuliyo nayo ya kuwaambia wengine habari njema ya Ufalme. Utendaji huu hufanya moyo wa Yehova ufurahi na husaidia watu wenye mioyo ya haki wajifunze njia ya uhai. (Mit. 27:11; 1 Tim. 4:16) Kutoa ushahidi kwa ukawaida huongeza uzoefu wetu katika huduma na hutokeza hisia ya shangwe na mafanikio.

3 Ripoti Utendaji Huo: Watu fulani ambao huenda kwenye utumishi wa shambani hupuuza kuripoti utendaji wao kwa wakati. Hatupaswi kamwe kuhisi kwamba jitihada zetu hazikustahili kuripotiwa. (Linganisha Marko 12:41-44.) Kwa vyovyote vile, twapaswa kuripoti kile ambacho tumetimiza! Kuwa na utaratibu nyumbani, kama vile kutumia kalenda ili kurekodi wakati uliotumiwa katika huduma, kutakuwa kikumbusha daima cha kutoa ripoti sahihi bila kukawia mwisho wa mwezi.

4 Toa Msaada Uhitajiwao: Huenda mipango ya kwenu ikahitaji kuboreshwa ili kusaidia wale wanaohitaji msaada wa kwenda kwenye huduma kwa ukawaida. Mwandishi wa kutaniko na viongozi wa funzo la kitabu wapaswa kupanga wahubiri wenye uzoefu wawasaidie. Ikiwa una watoto au wanafunzi wengine wa Biblia ambao ni wahubiri wasiobatizwa, wazoeze kuripoti utendaji wao kila mwezi.

5 Kumbuka simulizi la maisha, “Kushukuru kwa Ajili ya Maisha Marefu Katika Utumishi wa Yehova,” kwenye Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1997. Dada Ottilie Mydland wa Norway alikuwa mhubiri wa habari njema wa kawaida kabla ya ubatizo wake mwaka wa 1921. Miaka 76 baadaye, akiwa na umri wa miaka 99, alisema hivi: “Ninaterema kwamba bado naweza kuwa mhubiri wa kawaida.” Huo ni mtazamo wa ajabu kama nini kwa watumishi wote wa Yehova kuiga!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki