Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/00 uku. 8
  • Kupata Shangwe Katika Utumishi Wako Mtakatifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kupata Shangwe Katika Utumishi Wako Mtakatifu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Shangwe
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Shangwe​—Sifa Inayotoka kwa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Tumikia Yehova kwa Shangwe ya Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Mtumikie Yehova kwa Moyo Wenye Kujaa Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 5/00 uku. 8

Kupata Shangwe Katika Utumishi Wako Mtakatifu

1 Walirudi “wakiwa na shangwe.” Simulizi la Biblia huonyesha jinsi wanafunzi 70 walivyohisi waliporipoti kwa Yesu, baada ya safari ndefu ya kuhubiri. Walipendezwa sana kufanya mapenzi ya Mungu. (Luka 10:17) Ni nini kinachoweza kukusaidia upate shangwe kama hiyo katika utumishi mtakatifu?

2 Mtazamo Unaofaa: Una pendeleo kutoka kwa Mungu la kujulisha watu kusudi kuu la Yehova. Kwa kuhubiri, waweza kusaidia mtu ajitenge na mazoea ya ulimwengu yaliyoshuka na vizuizi vya dini isiyo ya kweli. Unaweza kuwapa watu tumaini la uhai katika ulimwengu usio na ugomvi unaotuzunguka leo. Fikiria shangwe ambayo Yehova hupata unapofanikiwa kupanda mbegu za kweli katika moyo wenye kuitikia. Uwe na mtazamo unaofaa unaposali kwa ajili ya roho ya Mungu ili itokeze tunda la shangwe unapofuatia huduma kwa moyo wako wote.

3 Mazoezi Yenye Kutumika: Kipindi cha maagizo alichoongoza Yesu pamoja na wale wanafunzi 70 kimefananishwa na Mkutano wa Utumishi wa kisasa. Aliwazoeza ili waweze kutimiza huduma yao kwa matokeo. (Luka 10:1-16) Leo, Mkutano wa Utumishi hukuzoeza njia za kuwafikia watu, jinsi ya kuanzisha mazungumzo, na jinsi ya kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Kwa kujitoa mwenyewe na kuboresha stadi zako za kuhubiri, hutahisi tena mashaka au kutofaa badala yake utakuwa na uhakika na shangwe kubwa sana.

4 Elekeza Fikira Katika Wakati Ujao: Yesu alipata shangwe katika utumishi wake mtakatifu licha ya mateso aliyovumilia. Kwa nini? Kwa sababu alielekeza jicho lake kwenye baraka na mapendeleo yaliyokuwa mbele yake. (Ebr. 12:2) Unaweza kufanya vivyo hivyo kwa kuelekeza akili na moyo wako kwa jina la Yehova na kwenye baraka zitakazokuja katika ulimwengu mpya wa Mungu. Utapata shangwe na kusudi katika huduma yako.

5 Unaweza kuwa na pendeleo kubwa zaidi leo kwa kumtolea Yehova utumishi mtakatifu. Hivyo, na useme: “Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu.”—Zab. 40:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki