Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 kur. 3-4
  • Je, Wajinufaisha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajinufaisha?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Mikutano ‘Inayotuchochea Katika Upendo na Matendo Mazuri’
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kukusanyika Pamoja kwa Ajili ya Ibada
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Mikutano Hunufaisha Vijana
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Mikutano ya Kuhimizana Ili Kupenda na Kufanya Kazi Nzuri
    Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 kur. 3-4

Je, Wajinufaisha?

1 Mamilioni ya watu leo wanataka kujua jinsi ya kushinda matatizo na kufurahia maisha. Wao hufurahia sana kusoma vitabu vya ushauri au kuendea vikundi na mashirika ya kutoa mashauri ya jinsi ya kuboresha maisha yao. Labda wengine wanaweza kueleza manufaa chache walizopata. Lakini, tukipima ubora wa maisha leo, je, kwa ujumla watu wamejifunza kufurahia maisha yenye amani, yenye kutosheleza kabisa kupitia programu za mafundisho ya binadamu? La hasha!—1 Kor. 3:18-20.

2 Kwa upande mwingine, Muumba wetu huandaa bila malipo mafundisho yenye kusaidia sana kwa wote watakaosikiliza. Yehova anataka kila mtu anufaike na mafundisho yake. Yeye ameandaa kwa ukarimu Neno lake lililopuliziwa liongoze mwanadamu katika unyoofu, na amefanya habari njema ya Ufalme wake itangazwe katika dunia yote. (Zab. 19:7, 8; Mt. 24:14; 2 Tim. 3:16) Maisha yenye furaha ya kweli yanahusiana moja kwa moja na kusikiliza amri za Yehova.—Isa. 48:17, 18.

3 Mwongozo wa Yehova ni bora zaidi kuliko ule unaoandaliwa na vitabu vya ushauri au mipango ya kuboresha hali zako inayotolewa na ulimwengu. Twaweza kupata msaada halisi na wenye manufaa za kudumu tukitumia kikamili maandalizi ya Yehova kama yaonyeshwavyo katika Neno lake na kama tufundishwavyo na tengenezo lake.—1 Pet. 3:10-12.

4 Jinufaishe Kwenye Mikutano ya Kutaniko: Leo, Yehova hupendezwa kutufundisha njia zake, nasi twanufaika kwa kusikiliza mafundisho yake. Mikutano yetu mitano ya kila juma yaonyesha jinsi Yehova anavyotuhangaikia kwa upendo. Tunapohudhuria mikutano ya kutaniko, ujuzi wetu kuhusu Mungu huongezeka. Twajifunza jinsi ya kujilinda wenyewe na mabaya kwa kuwa na uhusiano wa karibu na Yehova. Katika njia hii, tutachangamshwa.

5 Kuna mengi zaidi. Kwenye mikutano ya kutaniko twaweza ‘kupanuka.’ (2 Kor. 6:13) Hiyo yatia ndani kuwajua wengine kutanikoni. Twanufaika kutokana na badilishano la kitia-moyo, kama lile aliloandika mtume Paulo kwenye barua yake kwa Waroma. (Rom. 1:11, 12) Akiandikia Waebrania, aliwashauri sana wale ambao labda walikuwa wakisitawisha desturi ya kuacha ushirika wa Kikristo.—Ebr. 10:24, 25.

6 Uradhi wenye shangwe katika maisha wahusiana moja kwa moja na kupendezwa na masilahi ya wengine. Twatiwa moyo kutafuta njia za kuchangia furaha ya wengine. Kwa hiyo, mikutano yetu ya Kikristo, kwa hakika hutunufaisha binafsi na wale ambao twashirikiana nao katika ushirika wenye kujenga. Kinachohitajiwa upande wetu ni kushiriki kwa moyo wote.

7 Mtume Paulo alionyesha jambo kama hilo alipomshauri Timotheo akiandika hivi: “Uwe ukijizoeza mwenyewe ujitoaji-kimungu ukiwa shabaha yako.” (1 Tim. 4:7) Twaweza kujiuliza: ‘Je, ninajizoeza? Je, ninajifunza kunufaika kutokana na yale ninayosikia kwenye mikutano ya kutaniko?’ Majibu yetu yatakuwa ndiyo tukisikiliza kwa makini yale tunayosikia kwenye mikutano na kujitahidi kutumia tunayojifunza. Kwa macho ya imani, lazima tuweze kumwona Yehova kuwa Mfunzi Mkuu wa watu wake wala si ndugu wanaofundisha.—Isa. 30:20.

8 Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi: Mikutano hii miwili imekusudiwa kutusaidia tuwe wenye matokeo katika huduma ya Kikristo. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi—ni shule hasa yenye wanafunzi ambao wanapokea maagizo na mashauri kwa ukawaida. Una fursa ya kuonyesha maendeleo yako ukiwa msemaji wa hadharani na mwalimu wa Neno la Mungu. Lakini ili kupata faida kutokana na shule, lazima ujiandikishe, uihudhurie, ushiriki kwa ukawaida, na uzingatie moyoni migawo yako. Kukubali na kutumia mashauri yanayotolewa kutakusaidia ufanye maendeleo.

9 Mkutano wa Utumishi hutufundisha umuhimu wa huduma ya Kikristo na hutuonyesha jinsi ya kufanya wanafunzi. Je, wewe na familia yako mnanufaika kikamili kutokana na yale yaliyo katika mikutano hii miwili? Wenzi wa ndoa Wakristo wasema hivi: “Kwenye Mkutano mmoja wa Utumishi, tulisikia kwamba twapaswa kuchunguza andiko la siku tukiwa familia. Hatukuwa tukifanya hivyo, lakini sasa tunafanya hivyo.” Wamejinufaishaje? Wanakubali hivi: “Twaona kwamba mazungumzo wakati wa chakula mezani yanafurahisha zaidi. Hatubishani tena wakati wa chakula.” Je, hata watoto wadogo hunufaika na mikutano? Ndiyo. Mama huyo asema: “Ni wazi kwamba mikutano ina matokeo makubwa kabisa kwa watoto wetu. Juma moja tulimshika kijana wetu mwenye umri wa miaka sita akisema uwongo. Lakini kwenye mikutano juma hilo, hotuba ya maagizo ilikuwa ikiongea juu ya kusema uwongo. Akionekana kuwa na hatia, kijana wetu alimtazama baba yake na kujikunyata kitini. Alijifunza somo, nasi hatukuwa na tatizo baada ya hapo.”

10 Dada painia anasema kwamba ana furaha kuwa madokezo ya kuboresha huduma yetu hutolewa kwenye Mkutano wa Utumishi. Kwa nini? Anaeleza hivi: “Mimi huyachukulia kuwa ya kawaida tu. Nyakati nyingine nafikiri kwamba mambo yaliyodokezwa katika Huduma ya Ufalme Yetu hayatafaulu. Lakini kwenye Mkutano wa Utumishi, ninaposikia kwamba twapaswa kujaribu, mimi huchochewa kwa uchangamfu kutumia madokezo hayo. Hufanya huduma iwe yenye kusisimua!” Baada ya majuma kadhaa ya kutumia madokezo ya kujaribu kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza, alianzisha funzo kwenye ziara ya kwanza na msichana aliyekuwa akisali apate msaada.

11 Unaposikia hotuba inayotia ndani shauri la Biblia juu ya uchaguzi wa kibinafsi unaofanya, je, wewe huhisi kwamba Yehova anaongea nawe moja kwa moja? Ndugu mmoja alihisi hivyo. Alisema: “Hivi majuzi kwenye mkutano mmoja, kulikuwa na hotuba ambayo ndugu aliyeitoa alizungumzia aina za vitumbuizo vinavyowafaa Wakristo na vile visivyowafaa. Nilikuwa nikipenda kutazama ndondi kwenye televisheni. Lakini baada ya mkutano huo, niliamua kwamba mchezo huo ulikuwa aina ya kitumbuizo kisichofaa kwa Wakristo. Kwa hiyo siutazami tena.” Naam, ijapokuwa ndugu huyu alipenda sana jambo lililokuwa lenye jeuri, aliitikia mwongozo wa Yehova kwa unyenyekevu.—Zab. 11:5.

12 Mkutano wa Watu Wote, Funzo la Mnara wa Mlinzi, na Funzo la Kitabu la Kutaniko: Hotuba za watu wote tunazosikia kila juma hushughulikia habari mbalimbali za Biblia. Unapata faida gani kutokana na hotuba hizi? Mume mmoja Mkristo alieleza juu ya manufaa aliyopokea kwa kusema hivi: “Hotuba moja ya watu wote ilikazia matunda yote ya roho. Msemaji alitaja kwamba ili yeye mwenyewe ajitahidi kusitawisha matunda haya, angechagua sifa moja hususa na kuifanyia kazi juma moja. Mwishoni mwa juma, alitafakari jinsi alivyoonyesha sifa hiyo katika shughuli zake za kila siku. Kisha akafanyia kazi sifa nyingine juma lililofuata. Nilipenda wazo hilo nami nikaanza kufanya hivyo mwenyewe.” Alitumia vizuri kama nini alichokuwa amejifunza!

13 Funzo la Mnara wa Mlinzi hutufundisha kutumia kanuni za Biblia katika hali mbalimbali za maisha. Hilo hutusaidia tudumishe akili na mioyo iliyotulia yajapokuwa mahangaiko ya maisha. Funzo la Mnara wa Mlinzi pia hutupeleka sambamba na kweli mpya. Kwa mfano, tulinufaika na funzo la makala za gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 1999, zenye kichwa: “Mambo Haya Lazima Yatukie,” “Mwacheni Msomaji Atumie Ufahamu,” na “Kesheni na Mwe na Bidii Yenye Kuendelea!” Makala hizo zilikuathirije wewe binafsi? Je, kwa matendo yako waonyesha kwamba unatii kwa moyo wote onyo la Yesu juu ya wakati ujao? Je, unajitayarisha kwa ajili ya majaribu yaliyo mbele tunapoona “kitu chenye kuchukiza sana ambacho husababisha ukiwa . . . kikiwa kimesimama katika mahali patakatifu”? (Mt. 24:15-22) Je, miradi na maisha yako yanaonyesha kwamba jambo la maana kwako ni kutakasa jina la Yehova wala si kulundika mali za kimwili tu? Kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi, je, hatujifunzi kujinufaisha sasa?

14 Ebu wazia jinsi tunavyojifunza mambo mengi kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko kila juma. Kwa sasa tunajifunza kitabu cha Biblia cha Danieli. Katika miezi minne ambayo tumejifunza kitabu hiki, je, hatujaona imani yetu ikiongezeka kila juma? Kama nabii mpendwa wa Yehova, Danieli, twaimarisha imani yetu ili tuweze kuvumilia.

15 Yehova Hutufundisha Kuishi Tukiwa na Shangwe: Twaepuka huzuni nyingi tunaposikiliza amri za Mungu. Zaidi ya hilo, twajionea jinsi maisha yenye shangwe yalivyo. Kwa kufuata mwongozo wa Yehova, hatuwi tu watazamaji bali pia washiriki wa kazi yake. Na wanaofanya kazi ya Mungu ni watu wenye furaha.—1 Kor. 3:9; Yak. 1:25.

16 Fikiria kwa uzito jinsi unavyoweza kutumia mambo unayosikia kwenye mikutano ya kutaniko. (Yn. 13:17) Mtumikie Mungu kwa uchangamfu, kwa moyo wako wote. Shangwe yako itakuwa nyingi mno. Maisha yako yataboreshwa, yawe na maana zaidi. Naam, utakuwa ukijinufaisha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki