Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 7
  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Sitawisha Nguvu Zako za Ufahamu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Programu ya Kusanyiko la Pekee la Mwaka wa 2010
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 7

Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee

“Iweni Watu Wazima Katika Nguvu za Kuelewa” ndicho kichwa cha programu ya siku ya kusanyiko la pekee kuanzia Septemba 2000. (1 Kor. 14:20) Kwa nini tutafaidika tukihudhuria? Twaishi katika ulimwengu uliojaa ubaya. Ili tuukinze, lazima tusitawishe nguvu zetu za uelewevu wa kiroho ili tuweze kushinda uovu kwa wema. Hivyo ndivyo programu ya siku ya kusanyiko la pekee itakavyotusaidia kufanya.

Katika kipindi cha kufungua, mwangalizi wa mzunguko atazungumzia “Misaada ya Kutufanya Tuwe Watu Wazima Katika Uelewevu wa Biblia.” Atatuonyesha jinsi tunavyoweza kuimarishwa katika imani ya Kikristo. Msemaji mwenye kuzuru atakazia jinsi ambavyo matumizi ya kanuni za Biblia ni muhimu katika kusitawisha utambuzi, anapoongea juu ya kichwa “Linda Hali ya Kiroho kwa Kuzoeza Nguvu Zako za Ufahamu.”

Vijana pia lazima wasitawishe nguvu za uelewevu. Hilo litazungumziwa katika sehemu “Kwa Nini Tuwe Watoto Wachanga Kuhusu Ubaya?” na “Vijana Wanaojipatia Uelewevu Sasa.” Sikiliza vijana wakisema wanachofanya kujiimarisha kiroho ili waweze kudhibiti udadisi wowote juu ya utendaji mwovu wa ulimwengu na kuepuka taabu.

Twaweza kupataje furaha kubwa zaidi maishani? Msemaji mwenye kuzuru ataeleza hilo katika hotuba yake ya kumalizia “Nufaika kwa Kutumia Kanuni za Biblia kwa Uelewevu.” Atatoa mifano ya kuonyesha kwamba kutumia Neno la Mungu hutusaidia kushughulikia matatizo, kufanya maamuzi, na kunufaika kikweli kutokana na yale ambayo Yehova anatufundisha.

Wale wanaotaka kuonyesha wakfu wao kwa Mungu kupitia ubatizo wa maji kwenye kusanyiko wanapaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi upesi iwezekanavyo. Tia alama kwenye kalenda yako mara tu tarehe ya siku ya kusanyiko la pekee itangazwapo, na ufanye mipango hususa ili unufaike na programu hiyo yenye kujenga. Usikose sehemu yoyote ya siku ya kusanyiko la pekee! Itakuimarisha uendelee kuvumilia mfumo huu mwovu na udumu ukiwa mwaminifu kwa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki