Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Oktoba 9
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 12: “Zingatia Kazi za Ajabu za Mungu.” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatie kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Taja picha chache katika kitabu kipya zinazojenga uthamini kwa unabii wa Isaya.
Dak. 25: “Milenia Mpya—Unaweza Kutarajia Nini Wakati Ujao?” Mazungumzo yenye uchangamfu yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Baada ya kusoma tangazo lililotolewa katika barua ya Sosaiti kwa wazee ya Julai 3, 2000, gawia kila msikilizaji nakala moja ya trakti Habari za Ufalme Na. 36. Kisha endelea na mazungumzo ya maswali na majibu ya makala hiyo. Eleza mipango ya kwenu ya kukamilisha eneo lenu. Zungumzia jinsi ya kusaidia wapya na watoto wastahili kuwa wahubiri wasiobatizwa. Toa onyesho fupi la utoaji huo. Kazia uhitaji wa kila mtu kushiriki kikamili katika kampeni hii.
Wimbo 53 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 16
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Wakumbushe wahubiri kwamba wakati wa utendaji wa mwisho-juma, magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yatatolewa pamoja na trakti Habari za Ufalme Na. 36.
Dak. 15: “Vifaa Vinavyoelimisha, Vinavyochochea, na Vinavyoimarisha.” (Fungu la 1 na la 2 peke yake.) Hotuba. Zungumzia kifupi historia ya jinsi Sosaiti ilivyoanza kutayarisha vidio. (Ona kitabu Wapiga-Mbiu, ukurasa wa 600-601.) Tia moyo kila mtu aitazame vidio Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name anapojitayarisha kwa ajili ya mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Oktoba 30. Wale ambao wana vidio hiyo wanaweza kuwaazima wengine ambao hawana, au labda wanaweza kuitazama pamoja. Mahali ambapo watu hawana vidio, makutaniko yanaweza kuzungumzia mahitaji ya kwao.
Dak. 20: Sisi Sote Twaweza Kuonyesha Roho ya Upainia. Mazungumzo kati ya kiongozi wa funzo la kitabu na msaidizi wake, yakitegemea Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1997, ukurasa wa 22-23. Zungumzieni sababu kwa nini lingekuwa jambo zuri kuwa na mapainia wengi katika kutaniko na jinsi ambavyo wote wanaweza kufikia mradi huo. Pia zungumzieni njia za kutia moyo wale ambao kwa sasa wanapainia waendelee na jinsi ambavyo wote kutanikoni wanaweza kuongeza bidii katika huduma.
Wimbo 131 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu na Sanduku la Swali.
Dak. 20: Jitayarishe Vizuri kwa Ajili ya Mikutano. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Manufaa tunazopata kutokana na mikutano hutegemea sana jitihada tunayotia katika kutayarisha. Zungumzia madokezo yenye kutumika yaliyotolewa katika Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 1998, ukurasa wa 15-16, fungu la 8-11. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuonyesha jinsi wanavyositawisha hamu ya mikutano na kupata wakati unaohitajika wa kutayarisha vizuri.
Wimbo 211 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 30
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Oktoba.
Dak. 12: Mambo Yaliyoonwa Wakati wa Kutoa Trakti Habari za Ufalme Na. 36. Omba wahubiri mbalimbali wasimulie matokeo yenye kutia moyo ambayo wamefurahia kufikia sasa katika kugawanya trakti Habari za Ufalme Na. 36. Omba mapainia wa kawaida na wasaidizi waeleze wanavyothamini utendaji ulioongezeka wakati wa kampeni hii na fursa waliyo nayo ya kuhubiri na wahubiri wengi mbalimbali.
Dak. 25: Vidio Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name. Mazungumzo na wasikilizaji. Zungumzieni maswali yaliyo kwenye fungu la 3 la makala “Vifaa Vinavyoelimisha, Vinavyochochea, na Vinavyoimarisha.” Toa madokezo ya jinsi vidio hiyo inavyoweza kutumiwa kusaidia wenye kupendezwa wafahamu vizuri tengenezo letu. Tia ndani jambo lililoonwa moja au mawili mafupi.—Ona Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1992, ukurasa wa 30-31.
Wimbo 15 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 6
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Zungumzia maendeleo ya ugawanyaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 36. Eleza eneo limehubiriwa mpaka wapi kufikia sasa na kinachohitajika ili kulikamilisha kufikia Novemba 17.
Dak. 20: Sisi Huamini Nini? Ndugu afanya ziara ya kurudia kwa mtu ambaye aliuliza hivi, “Mashahidi wa Yehova hufundisha nini ambacho huwafanya wawe tofauti na dini nyingine?” Zungumzia mambo yaliyo katika sanduku kwenye ukurasa wa 6 katika Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1998. Eleza jinsi ambavyo dini nyingine hupuuza au hukataa kweli hizo za msingi za Biblia na kupendelea mafundisho ya binadamu.
Dak. 10: Kuimba—Sehemu Muhimu ya Ibada Yetu. Kiongozi wa funzo la kitabu azungumza na wahubiri wawili juu ya kuimba kwao katika mikutano ya kutaniko. Ameona kwamba hawaimbi kwa uchangamfu sana. Ashiriki nao mambo fulani kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 1997, ukurasa wa 27-28. Wanachunguza maneno ya mojawapo ya nyimbo zitakazoimbwa kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi juma hilo, kama inavyopendekezwa kwenye Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1999, ukurasa wa 20, fungu la 12. Kwa kuchukulia kuimba kwa uzito, twamsifu Yehova kwa uchangamfu kutoka moyoni.
Wimbo 223 na sala ya kumalizia.