Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/00 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 11
  • Juma Linaloanza Desemba 18
  • Juma Linaloanza Desemba 25
  • Juma Linaloanza Januari 1
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 12/00 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Desemba 11

Wimbo 50

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Ikiwa kutaniko lina nakala za Mtu Mkuu Zaidi au Mwalimu Mkuu akibani, onyesha jinsi zinavyoweza kutumiwa kwa manufaa katika huduma wakati huu wa majira ya sikukuu. Tia moyo kila mtu aone vidio The Bible—Accurate History, Reliable Prophecy anapojitayarisha kwa mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Desemba 25. Wale ambao wana vidio hiyo wanaweza kuwaazima wengine ambao hawana, au labda wanaweza kuitazama wakiwa pamoja. Mahali ambapo hakuna vidio, zungumzieni mahitaji ya kwenu.

Dak. 15: “Mhofu Yehova Mchana Kutwa.”a Tia ndani maelezo ya hofu ya kimungu yaliyo kwenye ukurasa wa 26 wa Amkeni!, Januari 8, 1998. Kazia manufaa zenye kujenga za kumhofu Yehova.

Dak. 20: “Msongo wa Marika na Pendeleo Lako la Kuhubiri.” Hotuba pamoja na mahoji. Alika watu ambao wamepatwa na msongo wa marika wasimulie jinsi walivyoweza kuendelea kwa bidii katika kazi ya kuhubiri ujapokuwa msongo huo.

Wimbo 78 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 18

Wimbo 94

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Taja mipango ya pekee ya utumishi wa shambani ya Desemba 25 na Januari 1. Jibu swali hili: Je, kuna katazo lolote la kushiriki maadhimisho ambayo huenda yakawa na mizizi isiyo ya Kikristo mradi yanafanywa kwa sababu zisizo za kidini?—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 292-293.

Dak. 12: “Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya Mwaka 2001.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Tia moyo wote waende sambamba na usomaji wao wa Biblia wa kila juma na kujitahidi kutimiza migawo yao ya shule.

Dak. 18: “Je, Wahubiri kwa Ujasiri?”b Omba maelezo juu ya maandiko yaliyo katika makala hiyo. Kwa kutumia kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 86, onyesha jinsi tunavyoweza kupata ujasiri zaidi na kuwa wenye matokeo zaidi katika utumishi wa shambani.

Wimbo 124 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 25

Wimbo 126

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Alika wasikilizaji wasimulie mambo yoyote waliyoona walipokuwa wakitoa ushahidi. Zungumzia toleo la vichapo la Januari.

Dak. 10: Sanduku la Swali.

Dak. 25: “Kujifunza Kutokana na Vidio The Bible—Accurate History, Reliable Prophecy.” Mazungumzo na wasikilizaji. Toa madokezo ya jinsi ambavyo vidio hiyo inaweza kutumiwa kuchochea wengine. (1999 Yearbook, ukurasa wa 51-52) Mwezi wa Februari tutazungumzia vidio ya pili katika mfululizo huu, The Bible—Mankind’s Oldest Modern Book. Mahali ambapo hakuna vidio hii, zungumzieni mahitaji ya kutaniko lenu.

Wimbo 151 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 1

TAARIFA: Makutaniko hayapaswi kusogeza Mkutano wao wa Utumishi kwa juma la Januari 1 hadi siku inayotangulia hiyo isipokuwa mwangalizi wa mzunguko awe anazuru. Katika kila kutaniko, nyongeza ya mkusanyiko yapasa kuzungumziwa kwenye Mkutano wa Utumishi kama ilivyoratibiwa. Ikiwa kuna kusanyiko la mzunguko juma hilo, viongozi wa funzo la kitabu wanapaswa kutangaza mahali na tarehe ya mkusanyiko kwenye mafunzo yao ya kitabu ya kawaida.

Wimbo 171

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ikiwa kutaniko lenu litabadili saa za mikutano mwaka ujao, sihi wote kwa fadhili waendelee kuhudhuria mikutano kwa ukawaida wakati wa saa mpya za mikutano. Wajulishe wanafunzi wa Biblia na watu wengine wenye kupendezwa juu ya mabadiliko yoyote, na waanze kutumia vikaratasi vya kukaribisha watu vinavyoonyesha ratiba mpya. Toa maelezo juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Agosti ya nchi na ya kutaniko lenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Desemba.

Dak. 17: Jinsi ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Ziara za Kurudia. Baba azungumza na familia yake jinsi wanavyoweza kuwa na matokeo zaidi katika huduma yao. Anakazia sababu za Kimaandiko za kufuatia watu wowote wenye kupendezwa waliopatikana. Wakitumia miongozo iliyo katika Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1999, ukurasa wa 22, fungu la 18, wanajitayarisha kufanya ziara za kurudia. Wote wanakubali kwamba wameongea na watu ambao wanapasa kurudiwa. Kila mmoja wao aeleza itikio alilopata katika ziara ya kwanza, na wengine wanatoa maoni na andiko la kutumia kwenye ziara ya kurudia. Wanachunguza mambo wanayoweza kutumia kwa matokeo katika broshua Anataka. Wazazi wanapanga mtoto mmoja ajizoeze atakayosema kwenye ziara yake. Wanapanga wakati hususa wa kufanya ziara za kurudia juma linalofuata.

Dak. 20: “Mkusanyiko wa Wilaya wa 2001 wa ‘Walimu wa Neno la Mungu’ wa Mashahidi wa Yehova.” Mwandishi ashughulikia makala hii ya nyongeza kwa maswali na majibu. Tumia maandiko yaliyotajwa kuonyesha sababu zinazofanya iwe muhimu sote tufuate sana mwelekezo wa Sosaiti. Kazia umuhimu wa kuomba ruhusa kazini mapema iwezekanavyo ili uwe huru kuhudhuria siku zote tatu za mkusanyiko. Pongeza kila mmoja kwa ushirikiano wake na mipango ya Sosaiti.

Wimbo 212 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki