Jinsi Kweli Inavyoweza Kukunufaisha
Mungu, ambaye sikuzote anasema kweli, anaahidi kukupatia “uzima wa milele.”—Yohana 3:16.
UNAHITAJI KUFANYA NINI?
Jifunze mambo ambayo Neno la Mungu la kweli linasema.—Yohana 17:3, 17.
Chagua kumtii Mungu.—Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.
Tumia mwongozo tunaopata kutoka kwa Mungu maishani mwako.—Yakobo 1:25.
Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wamejionea faida za kujifunza kweli za Biblia. Watafurahi kukueleza mambo wanayojifunza.
Ili ujifunze kweli zaidi kutoka katika Biblia, soma broshua Furahia Maisha Milele! iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova na inayopatikana kwenye tovuti ya www.jw.org.