Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Januari 8
Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 13: “Acheni Nuru Yenu Ing’ae.” Tia ndani maelezo kuhusu Mnara wa Mlinzi, Juni 1, 1997, ukurasa wa 15, fungu la 12-13. Watie moyo wote watumie kwa manufaa kila fursa ya kuhubiri.
Dak. 25: Maandalizi ya Upendo kwa Ajili ya Afya Yetu. Hotuba itolewe na mzee mwenye kustahili, ikitegemea Matendo 15:28, 29 na barua ya Februari 15, 1997 na Desemba 1, 1998. Kazia kwamba ulinzi bora kabisa wa kisheria dhidi ya kutiwa damu mishipani wapatikana kwa kujaza kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia. Wahubiri waliobatizwa watapewa kadi hii baada ya mkutano huu, lakini HAIPASI kujazwa leo. Kutaniko lapaswa kuwa na kadi za kutosha ili kugawia kila familia. Kutia sahihi, kushuhudia, na kuandika tarehe katika kadi zote kutafanywa baada ya Funzo la Kitabu la Kutaniko linalofuata, chini ya usimamizi wa kiongozi wa funzo la kitabu. Wale wanaotia sahihi wakiwa mashahidi wanapaswa kuona mwenye kadi akitia sahihi kadi hiyo. Viongozi wa funzo la kitabu wapaswa kuhakikisha kwamba wote walio katika kikundi chao wanapata msaada wanaohitaji ili kujaza kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia. Wazazi watapata Kadi ya Utambulishi kwa ajili ya watoto wao baada ya mkutano huu. Kwa kugeuza usemi ulio katika kadi hii kulingana na hali zao na masadikisho yao wenyewe, wahubiri wasiobatizwa wanaweza kuandika mwelekezo wao wenyewe na wa watoto wao.
Wimbo 1 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu na Sanduku la Swali.
Dak. 20: Je, Unachunguza Maandiko Kila Siku? Hotuba na mahoji. Zungumzia Mnara wa Mlinzi, Desemba 15, 1996, ukurasa wa 17-18, fungu la 12-14, ukikazia kwamba ni jambo la hekima familia kuzungumzia andiko la kila siku. Hoji washiriki wa familia ambao kila mmoja wao akumbuka mazungumzo ya hivi majuzi ya andiko la kila siku ambalo lilimnufaisha sana na atoe sababu yake. Kazia kwamba kufanya hivyo kwapasa kuwa sehemu ya programu ya kawaida ya funzo la familia linalokusudiwa kuimarisha familia zetu na kudumisha utendaji wake katika huduma.
Wimbo 67 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 22
Dak. 7: Matangazo ya kwenu.
Dak. 18: Jinsi ya Kutayarisha Utangulizi Mbalimbali. Hotuba na maonyesho. Zungumzia mambo ya msingi kutoka katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 9. Onyesha jinsi tunavyoweza kuchagua utangulizi bora unaofaana na utoaji wetu, utu, na eneo letu. Zungumzia baadhi ya mifano ya utangulizi unaoweza kutumiwa tutoapo broshua Anataka, kisha upange kuwe na onyesho moja au mawili. (Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1997, ukurasa wa 8.) Watie moyo wote watumie kwa manufaa madokezo yaliyotolewa katika kitabu Kutoa Sababu na Huduma Yetu ya Ufalme wanaposhiriki utumishi wa shambani.
Dak. 20: “Uwe Msikilizaji Mzuri.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Zungumzia mambo yaliyo katika kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 27-28, fungu la 15-17. Jaribu bora zaidi la mazoea yetu ya kusikiliza ni mambo tunayokumbuka. Waombe wasikilizaji wakumbuke baadhi ya mambo yenye kutokeza yaliyozungumziwa na wale walioshiriki kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi leo.
Wimbo 96 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Januari. Taja toleo la vichapo la Februari, na utaje vitabu ambavyo kutaniko linavyo akibani.
Dak. 15: Mjue Muumba Vizuri Zaidi. Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1999, ukurasa wa 24-26, kuchochea hamu ya kujifunza kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? katika funzo la kitabu la kutaniko. Watie moyo vijana washiriki katika mazungumzo ya kila juma kwenye funzo la kitabu. Ingefaa wote wahudhurie kwa ukawaida, wakiwa na hamu ya kujifunza mengi iwezekanavyo kuhusu Muumba wetu Mtukufu.
Dak. 20: “Wazazi—Fundisheni Watoto Wenu Mazoea Mazuri.” Hotuba na kuhoji wazazi ambao watoto wao wanafanya vizuri kiroho. Wazazi wanakumbuka mambo yanayofaa ambayo wamefanya ili kuwahusisha watoto wao katika huduma ya shambani. Wakati uruhusupo, tia ndani madokezo kutoka katika kitabu Furaha ya Familia, ukurasa wa 55-59.
Wimbo 149 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Na Uwe Mtendaji Mwenye Furaha.”a Taja mambo ambayo huongeza shangwe yetu katika utumishi wa Mungu, kama yaonyeshwavyo katika kitabu Insight, Buku la 2, ukurasa wa 120, fungu la 6-8.
Dak. 20: Waweza Kupata Vitumbuizo Vifaavyo. Kikundi cha familia chazungumzia ushauri uliotolewa katika Amkeni!, Mei 22, 1997. Baba anahangaishwa na tafrija za familia yake. Baada ya kuzungumzia kifupi “Ni Nini Kimepata Vitumbuizo?” (ukurasa wa 4-7), wanazungumzia aina ya vitumbuizo ambavyo vyaweza kuwa vyenye kujenga na vyenye manufaa. Chunguzeni habari iliyo katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 131-132, chini ya kichwa kidogo “Tafrija” na ukurasa wa 135-136, chini ya kichwa kidogo “Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu.” Kazia fungu wanalotimiza wazazi katika kuongoza na uhitaji wa washiriki wa familia kushirikiana kwa manufaa ya familia nzima.
Wimbo 190 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.