Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/01 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Februari 12
  • Juma Linaloanza Februari 19
  • Juma Linaloanza Februari 26
  • Juma Linaloanza Machi 5
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 2/01 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Februari 12

Wimbo 6

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Vidio The Bible—Mankind’s Oldest Modern Book itazungumziwa kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Februari 26. Mazungumzo hayo yatategemea maswali yaliyo kwenye ukurasa wa 7 wa toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 15: “Mtukuze Yehova kwa Kazi Bora.”a Tia ndani maelezo kutoka katika kitabu Wapiga-Mbiu, ukurasa wa 187, fungu la 2-3.

Dak. 20: “Jinsi ya Kuwashawishi Wengine.” Mazungumzo kati ya kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko na painia au mhubiri mwenye matokeo, yakitegemea makala hii na vilevile mambo yaliyoteuliwa katika Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1998, ukurasa wa 21-23. Chunguzeni sanduku lililo kwenye ukurasa wa 23, “Kuufikia Moyo wa Mwanafunzi Wako.” Baada ya kuchagua fundisho la kidini lisilo la kweli ambalo watu wengi katika eneo lenu wanaamini, zungumzieni jinsi ya kumsadikisha mtu kile ambacho Biblia husema juu ya habari hiyo.

Wimbo 208 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 19

Wimbo 221

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu, Habari za Kitheokrasi, na Sanduku la Swali.

Dak. 22: “Julisheni Jina la Yehova na Matendo Yake.”b Mzee azungumzia mipango ya pekee inayofanywa kwenu ili kuongeza utendaji mwezi wa Machi na Aprili, kutia ndani jitihada za kutia moyo wahubiri wengi iwezekanavyo wafanye upainia msaidizi. Panga wengine waliofanya upainia mwezi wa Aprili mwaka uliopita waeleze jinsi walivyopata uradhi kwa kufanya hivyo. Zingatia kusaidia kila mhubiri mwenye kustahili asiyetenda ajiunge nasi tena katika utumishi na pia kusaidia watoto na wanafunzi wengine wa Biblia wastahili kuwa wahubiri wasiobatizwa.—Ona Sanduku la Swali la Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 2000.

Wimbo 27 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 26

Wimbo 48

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani wa Februari.

Dak. 12: Madokezo ya Utoaji wa Kitabu Ujuzi. Je, umefikiria jinsi ya kutoa kitabu Ujuzi mwezi wa Machi? Unapotazama kurasa za nyuma za matoleo yaliyopita ya Huduma Yetu ya Ufalme, utapata madokezo ya ziara za kwanza, mengi yakiwa na madokezo ya kufanya ziara za kurudia. Zungumzia utoaji wa aina mbili au tatu kati ya ule uliodokezwa. (Machi, Juni, Novemba 1996; Juni 1997; Machi 1998) Toa wonyesho wa madokezo mawili yaliyo katika toleo la Novemba 1996 ya kuanzisha mafunzo ya Biblia moja kwa moja. Tia moyo kila mtu ajitahidi sana kuanzisha mafunzo mapya ya Biblia.

Dak. 25: “Kujenga Uthamini kwa Ajili ya Vidio The Bible—Mankind’s Oldest Modern Book.” Mazungumzo na wasikilizaji ukitumia maswali yaliyo kwenye ukurasa wa 7. Kazia kwamba, nakala milioni 100 za Biblia ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, ikiwa nzima au kwa sehemu katika lugha 37, zafanya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya kuwa mojawapo ya Biblia zilizogawanywa zaidi. Mwezi wa Aprili tutazungumzia vidio ya tatu katika mfululizo huu, The Bible—Its Power in Your Life.

Wimbo 64 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 5

Wimbo 81

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 18: “Yehova Hupa Nguvu.”c Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi maandiko yanavyotumika.

Dak. 22: “‘Nyakati za Hatari Zilizo Ngumu Kushughulika Nazo’—Tunaweza Kukabilianaje Nazo?” Makala hiyo ishughulikiwe kwa njia ya hotuba ikitolewa na mwangalizi-msimamizi, wasikilizaji wakishiriki. Tia ndani mahoji ya mhubiri mmoja au wawili ambao wamerekebisha mitindo yao ya maisha ili wakabiliane na nyakati hizi ngumu.

Wimbo 108 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki