Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/01 uku. 1
  • Jinsi ya Kuwashawishi Wengine

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuwashawishi Wengine
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Kuifikia Mioyo kwa Ufundi wa Ushawishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Wasaidie Wengine Wakubali Ujumbe wa Ufalme
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Fundisha kwa Ushawishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Tunapaswa “Kumjibu Kila Mtu” Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 2/01 uku. 1

Jinsi ya Kuwashawishi Wengine

1 Mtume Paulo alijipatia sifa ya kuwa mhudumu mwenye kushawishi. (Mdo. 19:26) Hata Mfalme Agripa alimwambia hivi: “Kwa muda mfupi ungenishawishi niwe Mkristo.” (Mdo. 26:28) Ni nini kilichofanya huduma ya Paulo iwe yenye kushawishi jinsi hiyo? Alitoa sababu yenye maana dhahiri kwa kutumia Maandiko, akibadilisha hoja zake kupatana na wasikilizaji wake.—Mdo. 28:23.

2 Kwa kumwiga Paulo, twahitaji kuwa wenye kushawishi katika huduma yetu. Jinsi gani? Kwa kutumia ufahamu tunapoongea na wengine na kuwasikiliza. (Mit. 16:23) Hatua tatu muhimu zitatusaidia tutimize hilo.

3 Sikiliza kwa Makini: Mtu yule mwingine anapoongea, sikiliza uone kama kuna jambo mnaloafikiana ili upate njia ya kuendeleza mazungumzo. Mtu akipinga, jaribu kutambua kwa nini anapinga. Itasaidia kujua kwa usahihi anachoamini, kwa nini anaamini hivyo, na kilichomsadikisha aamini hivyo. (Mit. 18:13) Kwa busara, jaribu kumfanya akueleze maoni yake.

4 Uliza Maswali: Mtu akisema kwamba anaamini Utatu, unaweza kuuliza: “Je, umeamini Utatu sikuzote?” Kisha endelea kuuliza: “Je, umefanya utafiti wa kutosha juu ya vile Biblia husema kuhusu habari hiyo?” Pia unaweza kuuliza hivi: “Kama Mungu ni sehemu ya Utatu, je, hatungetazamia kwamba Biblia iseme hivyo waziwazi?” Majibu utakayopata yatakusaidia kusababu na mtu huyo kuhusu kile ambacho Maandiko husema.

5 Tumia Kusababu Timamu: Shahidi mmoja alimwuliza mwanamke mmoja ambaye aliamini kwamba Yesu ni Mungu: ‘Kama ungejaribu kutoa kielezi cha watu wawili wanaolingana, ungetumia watu wenye uhusiano gani wa kifamilia?’ Akajibu: “Naweza kutumia ndugu wawili.” Ndugu akaongeza kusema: “Labda hata mapacha wanaofanana. Lakini anapotufunza tumwone Mungu kuwa Baba na yeye mwenyewe kuwa Mwana, Yesu alikuwa akituambia nini?” Mwanamke huyo alipata kuelewa kwamba mmoja ni mkuu na ana mamlaka zaidi. (Mt. 20:23; Yn. 14:28; 20:17) Akili yake na moyo wake ulifikiwa kwa ustadi wa ushawishi.

6 Bila shaka, si wote watakaokubali kweli, hata utoaji wetu uwe sahihi au wenye maana dhahiri jinsi gani. Lakini kama Paulo acheni tuwe wenye bidii katika kutafuta wale wenye mioyo minyoofu katika eneo letu, tukiwashawishi wakubali ujumbe wa Ufalme.—Mdo. 19:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki