Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/01 uku. 1
  • Mtukuze Yehova kwa Kazi Bora

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mtukuze Yehova kwa Kazi Bora
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Matendo Mema Yamtukuzayo Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Je, Una “Bidii kwa Ajili Ya Kazi Njema”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Watu Wenye Juhudi ya Kazi Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kuchocheana kwa Bidii Katika Matendo Mazuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 2/01 uku. 1

Mtukuze Yehova kwa Kazi Bora

1 Unapopatwa na dhoruba kali, inaburudisha kama nini kupata kinga! Ikiwa kuna joto la kutosha na usalama na ikiwa wenye nyumba ni wakaribishaji, utafurahia kukaa huko. Kazi ya kuhubiri Ufalme huelekeza watu walio katika mfumo wa Shetani mahali salama kama hapo. Je, mwenendo wetu wa kila siku waweza kusaidia wengine waone jinsi mahali hapa salama panavyovutia? Ndiyo, kwa kuwa Yesu alisema kwamba watu ‘wangeona kazi zetu bora na kumpa utukufu Baba yetu aliye mbinguni.’—Mt. 5:16.

2 Twaweza kujiendeshaje ili kazi zetu zivutie wengine waje kwa Yehova na tengenezo lake? Kwa kuacha maneno ya Yesu yaliyorekodiwa kwenye Luka 6:31 na 10:27 yafinyange maisha yetu kila siku. Kufanya hivyo kutatuchochea tuhangaikie wanadamu wenzetu, kukitutofautisha na ulimwengu huu wenye baridi na usiojali.

3 Dada mmoja kwenye feri aliona mwanamke kijana ambaye alishikwa na uchefuchefu kwa sababu ya bahari hivi kwamba hakuweza kumshughulikia mtoto wake mdogo. Dada huyo akajitolea kumtunzia mtoto wake. Mwanamke huyo alipomwuliza jinsi ambavyo angeweza kuonyesha shukrani, dada alisema: ‘Tafadhali sikiliza Mashahidi wa Yehova watakapokutembelea.’ Mwanamke huyo alifanya hivyo, na sasa yeye na mume wake ni Mashahidi. Kazi bora zilifanya watu hao wausikilize ujumbe wa Ufalme.

4 Maisha Yetu Yote Yanahusika: Mwenendo wetu kwenye ujirani, kazini, au shuleni, na wakati wa tafrija hufanya wengine wawe na maoni fulani kutuhusu na kuhusu dini yetu. Kwa hiyo, twapaswa kujiuliza hivi: ‘Wengine wananionaje mimi na familia yangu? Je, majirani huona nyumba yetu na uwanja wetu kuwa safi na wenye kupendeza? Je, wafanyakazi wenzetu na wanafunzi wenzetu hutuona kuwa watu wenye kufika kwa wakati na wenye bidii? Je, wengine wataona sura yetu kuwa ya kiasi na yenye kuheshimika?’ Kazi zetu bora zaweza kufanya ibada ya Yehova ivutie zaidi wengine.

5 Petro alionya kwamba Wakristo wangedhihakiwa. (1 Pet. 4:4) Lazima tuhakikishe kwamba mwenendo wetu hautokezi mazungumzo yasiyofaa. (1 Pet. 2:12) Kazi zetu za kila siku zikimtukuza Mungu tunayemwabudu, basi tutakuwa kama taa zilizowekwa juu, zinazovutia wengine waje mahali salama ambapo Yehova huandaa.—Mt. 5:14-16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki