Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 4/1 uku. 9
  • Matendo Mema Yamtukuzayo Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matendo Mema Yamtukuzayo Yehova
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • “Mungu Hana Upendeleo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • “Mwenye Furaha Ni Yule Mtu Ambaye Amepata Hekima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Mtakuwa Watakatifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kondoo wa Yesu Husikiliza Sauti Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 4/1 uku. 9

Wapiga-Mbiu wa Ufalme Waripoti

Matendo Mema Yamtukuzayo Yehova

KATIKA Mahubiri yake ya Mlimani, Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.” (Mathayo 5:16) Vivyo hivyo, Wakristo wa kweli leo hujishughulisha katika ‘matendo mema’ yamtukuzayo Yehova.

Matendo mema haya ni yapi? Hayo hutia ndani kuhubiri habari njema, lakini mwenendo wetu mzuri pia ni sehemu muhimu. Mara nyingi ni mwenendo wetu mwema ambao mara ya kwanza huvutia watu kwenye kutaniko la Kikristo. Mambo yaliyoonwa yafuatayo yanaonyesha jinsi Mashahidi wa Yehova katika Martinique ‘wanavyoacha nuru yao iangaze mbele ya watu.’

◻ Alipokuwa akifanya kazi ya kuhubiri, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alimtembelea mwanamke mmoja Mkatoliki. Kwa miaka 25 mwanamke huyu alikuwa ameishi na mwanamume ambaye hakuwa amefunga ndoa naye. Alikuwa amefahamu mafundisho ya Mashahidi wa Yehova, kwa kuwa, yapata miaka saba iliyopita, alikuwa amepokea kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.a Mwanamke huyo alimwambia yule Shahidi hivi: “Kuna dini nyingi sana. Sijui nimwamini nani katika mvurugo huu wote.” Yule Shahidi alimwelezea kwamba kweli yaweza kupatikana katika Biblia pekee na kwamba ili aipate, alipaswa kujifunza Maandiko kwa uangalifu na kumwomba Mungu roho yake na mwelekezo wake.

Kwa muda fulani, ijapokuwa mwanamke huyo alipendezwa na kujifunza Biblia, alikataa mialiko kadhaa ya kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova. Kwa nini? Alikuwa mwenye haya sana. Hata hivyo, baada ya kualikwa kwenye Ukumbusho wa kifo cha Kristo, alishinda haya yake akahudhuria.

Jambo lililompendeza zaidi kuhusu mikutano lilikuwa hali ya upendo katika Jumba la Ufalme. Hakuwa amepata kuona urafiki wa kweli kama huo katika kanisa lake! Baada ya mkutano huo alianza kuhudhuria mikutano yote iliyoongozwa na Mashahidi wa mahali hapo, na upesi akaolewa na mwanamume aliyekuwa akiishi naye. Sasa yeye ni mshiriki aliyebatizwa wa kutaniko hilo.

◻ Matendo mema ya Shahidi mwingine yalitokeza matokeo mazuri. Alikuwa na kazi yenye daraka kubwa katika ofisi moja. Baada ya kuajiriwa kwa mwanamume mmoja kutoka kisiwa cha Réunion, baadhi ya wafanyakazi walianza kumdhihaki kwa sababu ya ufupi wake. Yeye akawa mtu wa kuchekwa. Kwa kinyume, Shahidi huyo sikuzote alikuwa mwenye fadhili na mwenye staha kwa mwanamume huyo. Punde akauliza kwa nini mwanamke huyo alikuwa tofauti sana.

Shahidi huyo akamwambia kwamba mwenendo wake wa staha ulitokana na kanuni za Biblia alizokuwa amejifunza kutoka kwa Mashahidi wa Yehova. Pia alimwonyesha Maandiko yasema nini kuhusu makusudi ya Mungu na tumaini la ulimwengu mpya. Mwanamume huyo akakubali funzo la Biblia, akaanza kuhudhuria mikutano ya Kikristo, na kumwoa mwanamke aliyekuwa akiishi naye.

Hatimaye alirudi Réunion. Zamani alikuwa amepata magumu kutoka kwa watu wake wa ukoo, hasa na familia ya mke wake. Lakini sasa walivutiwa sana na mwenendo wake wa Kikristo. Mwanamume huyo alibatizwa naye sasa ni mtumishi wa huduma. Washiriki kadhaa wa familia yake, kutia ndani mke wake na mabinti wawili, pia wanatumikia katika kutaniko la Kikristo wakiwa watangazaji wa habari njema za Ufalme wa Mungu.

[Maelezo ya Chini]

a Kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki