Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme
“Mtakuwa Watakatifu”
MWONGOZO wa Mungu kwa Wakristo ni “msijifananishe na tamaa zenu za kwanza, za ujinga wenu; bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.” (1 Petro 1:14-16) Mara nyingi mwenendo kama huo wa utakatifu unakuwa ushuhuda mzuri kwa wengine. (1 Petro 2:12) Duniani pote, kama vile mambo yafuatayo yalioonwa yanavyoonyesha, watu wenye mioyo myeupe wanafanya mabadiliko yaliyo ya lazima kuleta mwenendo wao upatane na shauri hilo.
◻ Katika Ekwedori mwanamume mmoja aliacha funzo lake la Biblia wakati Shahidi aliyekuwa akijifunza naye alipotengwa na ushirika kwa sababu ya ukosefu wa adili. Uhitaji wake wa kiroho ulimwongoza achunguze dini nyinginezo. Yeye alijiunga na dini ya Kievanjeli na akafanya maende-eo kufikia hatua ya kuwa mchungaji wa kanisa lake mwenyewe. Hata hivyo, dhamiri yake ilimsumbua, kwa kuwa yeye hakuwa amefunga ndoa na yule mwanamke aliyekuwa akiishi pamoja naye. Aliposhauriana na wachungaji wa makanisa mengine, wao walimhakikishia kwamba hili halikuwa tatizo. Hata hivyo, yeye alihisi kwamba hilo halikuwa sawa, kwa kuwa yule Shahidi mwenyewe aliyekuwa akijifunza pamoja naye alikuwa ametengwa na ushirika kwa sababu ya ukosefu wa adili. Yeye hakuweza kuelewa kwa sababu gani yeye hakukaripiwa na kanisa lake mwenyewe. Baadaye, mwenzi wake aliyekuwa akiishi naye alionana na Mashahidi wa Yehova na akaanza kujifunza Biblia pamoja nao. Mwanamume huyo alianza kujifunza pamoja na mwanamke huyo. Wote wawiii sasa wanahudhuria mikutano, wakifanya maendeleo katika maarifa ya kanuni za Biblia, na wanachukua hatua za kufunga ndoa ili waweze kutumikia Yehova katika njia safi inayokubalika.
◻ Katika jambo jingine lililoonwa kutoka Ekwedori, Shahidi anaeleza hivi: “Katika Februari 1984, bibi wa umri wa makamu alituuliza sisi tujifunze naye. Ni jambo gani lililomsukuma atoe ombi hilo? Ndugu ya bibi huyo alikuwa amekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, naye alikuwa amevutiwa sana na mwenendo wake bora. Wakati wa funzo la Biblia la pili, waligusia habari ya kuvuta sigareti, lililokuwa mojapo ya matatizo ya bibi huyo. Hata hivyo, kwenye funzo lililofuata juma moja baadaye yeye alijivunia kutangaza kwamba tangu ajifunze maoni ya Biblia juu ya kuvuta sigareti hajagusa hata sigareti moja! Alikuwa na tatizo jingine—nyumba yake ilijaa mifano ya kidini. Lakini aliposoma Kumbukumbu 7:26, linalosema: “Na machukizo usitie ndani ya nyumba yako . . . kwa kuwa ni kitu kilichoharimishwa,” alianza kuvichoma vyote.
Tangu wakati huo na kuendelea, alianza kuhudhuria mikutano na hajakosa hata mmoja tangu hapo. Muda mfupi baada ya hapo, aliweza kukishinda kizuizi kilichokuwa kigumu kupita yote—alivunja uhusiano usio wa kiadili aliokuwa nao pamoja na mwanamume aliyeoa. Sasa, kwa mara ya kwanza katika maisha yake, aliweza kupata furaha halisi, kwa kuwa sasa aliweza kumtumikia Yehova akiwa na dhamiri safi. Alibatizwa katika Aprili 1985 na wakati huo alikuwa akiongoza mafunzo manne ya Biblia pamoja na wengine. Mradi wake unaofuata ni kuwa painia, kwa kuwa anahisi hiyo ndiyo njia bora anayoweza kuonyesha uthamini wake kwa Yehova, aliyemkomboa kutoka “maisha ya ubatili ya ukosefu wa adili.”
◻ Matokeo mazuri ya mwenendo wa kimungu yalionekana katika shule ya bweni ya wasichana katika Kenya, ambapo mwenendo mwema wa Shahidi ulionek-na katika njia yenye kutokeza. Walimu wanaume tisa waliajiriwa kazi na shule hiyo, kutia ndani mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Lakini mmoja baada ya mwingine walilazimika kufutwa kazi kwa sababu ya ngono zisizo na adili pamoja na wanafunzi. Baada ya muda, ni mmoja tu wa wale tisa aliyebaki—yule mwalimu aliyekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova!
Kweli kweli, inawezekana kwa watu waliokuwa wameishi maisha yasiyo na adili kubadilika. Tunapokuwa ‘watakatifu katika mwenendo wetu wote,’ si kwamba tu tunaandaa ushuhuda mwema kwa wengine bali pia tunaufurahisha moyo wa Yehova. Hivyo, tunajiweka wenyewe katika mstari wa kupata uzima wa milele.—Mithali 27:11.
[Sanduku katika ukurasa wa 21]
“Kwa kuwa mimi ni Yehova Mungu wenu; na ni lazima ninyi mjitakase wenyewe na ni lazima ninyi mjithibitishe wenyewe kuwa watakatifu kwa sababu mimi ni mtakatifu.”—Walawi 11:44, NW.
[Sanduku katika ukurasa wa 21]
“Na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho.”—2 Wakorintho 7:1.