Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/01 uku. 8
  • Upendo Hutuchochea Kuhubiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo Hutuchochea Kuhubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • “Upendo Alio Nao Kristo Hutulazimisha”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
  • “Lazima Umpende Yehova Mungu Wako”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Lo Lote Ufanyalo—Hubiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Huduma Yetu—Wonyesho wa Upendo wa Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 3/01 uku. 8

Upendo Hutuchochea Kuhubiri

1 Tukiwa Mashahidi wa Yehova, twajulikana sana kwa bidii yetu ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme. (Mt. 24:14) Kuna zaidi ya wahubiri milioni sita ulimwenguni pote na idadi yao huongezeka wapya wanapojiunga nasi katika mahubiri. Tarakimu huonyesha idadi ya wanaoshiriki kazi hiyo.

2 Ni nini ambacho hutuchochea kushiriki katika kazi hiyo ngumu? Hatulazimishwi wala kushawishiwa na vitu vya kimwili, au vyeo vya heshima. Mwanzoni, wengi wetu tuliogopa kwa sababu tulihisi hatustahili na mara nyingi watu hawakupendezwa. (Mt. 24:9) Watu wengi huwa hawaelewi kinachotuchochea. Lazima kuwe na sababu yenye nguvu inayofanya tuvumilie.

3 Nguvu za Upendo: Yesu alitaja amri iliyo kuu zaidi ya zote aliposema kwamba ‘lazima tumpende Yehova kwa moyo, nafsi, akili, na nguvu zetu zote.’ (Mr. 12:30) Upendo wetu kwa Yehova unatokana na kuthamini sana utu wake—Mtawala Mwenye Enzi Kuu, Muumba wa vitu vyote ambaye ‘anastahili kupokea utukufu, heshima, na nguvu.’ (Ufu. 4:11) Sifa zake za ajabu hazina kifani.—Kut. 34:6, 7.

4 Kumjua na kumpenda Yehova hutuchochea kuangaza nuru yetu mbele ya wanadamu. (Mt. 5:16) Nuru yetu hung’aa tunapomsifu hadharani, tunaposema juu ya matendo yake ya ajabu, na tunapoeneza ujumbe wa Ufalme. Kama vile malaika arukaye katika mbingu, sisi pia tuna ‘habari njema idumuyo milele ya kutangaza kuwa taarifa za mteremo kwa kila taifa na kabila na lugha na watu.’ (Ufu. 14:6) Upendo ndio unaochochea kazi yetu ya kuhubiri ulimwenguni pote.

5 Ulimwengu huona kazi yetu ya kuhubiri kuwa “upumbavu” ambao wapaswa kupuuzwa. (1 Kor. 1:18) Jitihada zimefanywa ulimwenguni pote ili kukandamiza kazi yetu. Upendo wetu mshikamanifu hututia nguvu kusema kama mitume: “Hatuwezi kukoma kusema juu ya mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia. . . . Lazima sisi tumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.” (Mdo. 4:20; 5:29) Kazi ya kuhubiri yaendelea kuenea katika sehemu zote za dunia ujapokuwa upinzani.

6 Upendo wetu kwa Yehova ni kama moto uwakao ambao hutuchochea kutangaza kotekote sifa zake bora. (Yer. 20:9; 1 Pet. 2:9) Tutaendelea ‘kuyatangaza matendo yake kati ya mataifa . . . kwa kuwa ametenda makuu’!—Isa. 12:4, 5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki