Sehemu ya 3
“Upendo Alio Nao Kristo Hutulazimisha”
Ni nini kinachotuchochea kuendelea kumfuata Yesu? Mtume Paulo anajibu: “Upendo alio nao Kristo hutulazimisha.” (2 Wakorintho 5:14) Katika sehemu hii, tutajifunza kuhusu upendo alio nao Yesu—jinsi anavyompenda Yehova, anavyowapenda wanadamu kwa ujumla, na anavyompenda kila mmoja wetu. Kujifunza kuhusu upendo huo kutatuchochea kwelikweli. Mioyo yetu itachochewa, nasi tutaona kwamba lazima tuchukue hatua, tufanye maendeleo, na kufuata mfano wa Bwana wetu.