Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 10/8 kur. 26-27
  • Upendo Unaoshikamanisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo Unaoshikamanisha
  • Amkeni!—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Dhoruba Zinapozuka
  • Upendo Unaotushikamanisha
  • Nanga Yao Ni Tumaini, Nao Huchochewa na Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • “Hakuna Hata Mmoja Wenu Atakayepotea”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Dini Yako—Je, Ni Merikebu Isiyopaswa Kuachwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Paulo Ashinda Janga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 10/8 kur. 26-27

Maoni ya Biblia

Upendo Unaoshikamanisha

KATIKA 1978 dhoruba kubwa katika Atlantiki Kaskazini iliipiga meli ya abiria ya kianasa ya bahari-kuu Queen Elizabeth 2. Mawimbi yenye kimo cha jengo lenye orofa kumi yaliangukia meli hiyo yakiifanya iruke-ruke kama kizibo ndani ya maji. Fanicha na abiria walirushwa huko na huko chombo hicho kilipokuwa kikizama na kuibuka kwa fujo. Kwa kutazamisha, abiria hao 1,200 walipata majeraha madogo tu. Uhandisi, maunzi, na ujenzi mzuri ulizuia meli hiyo kuvunjika.

Karne nyingi zilizopita kulikuwa na meli nyingine katika dhoruba kali mno. Mtume Paulo na wengine 275 walikuwa melini. Wakihofia kwamba meli hiyo ingevunjika vipande-vipande kutokana na ukali wa dhoruba hiyo, yaelekea mabaharia hao walipitisha “misaada”—minyororo au kamba—chini ya meli kutoka upande mmoja hadi mwingine ili kushikanisha pamoja vipande vya mbao vilivyofanyiza sehemu za nje za meli hii ya kibiashara. Abiria wote waliokuwamo walisalimika, ingawa meli hiyo haikusalimika.—Matendo, sura 27.

Majaribu katika maisha nyakati fulani huenda yakatufanya tuhisi kana kwamba tulikuwa katika meli kwenye bahari zenye msukosuko. Mawimbi ya mahangaiko, kukata tamaa, na mshuko-moyo yaweza kutupata, yakijaribu upendo wetu hadi kikomo. Ili kustahimili dhoruba hizo na kuepuka kuvunjika, twahitaji misaada fulani.

Dhoruba Zinapozuka

Imani na uvumilivu wa mtume Paulo hufafanuliwa vizuri katika Biblia. Alifanya kazi kwa bidii kwa ajili ya makutaniko ya mapema ya Kikristo. (2 Wakorintho 11:24-28) Matimizo yake katika kazi ya Bwana hutoa ushahidi wa wazi wa upendo wake mwingi kwa majirani wake na uhusiano wake imara pamoja na Mungu. Hata hivyo maisha ya Paulo hayakuwa tu shwari sikuzote. Kihalisi na kitamathali, mtume Paulo alistahimili dhoruba nyingi.

Katika siku ya Paulo, meli ilipokabili dhoruba kali, kusalimika kwa abiria na meli kulitegemea ustadi wa wafanyakazi wa melini na vilevile jinsi meli hiyo imeshikamanishwa pamoja. Ilikuwa hivyo pia katika maana ya kitamathali. Ingawa Paulo alikuwa amestahimili unyimivu wa kimwili, kufungwa gerezani, na kuteswa, dhoruba kali kupita zote ambayo ilitahini uthabiti na uwezo wake wa kiroho na kihisia-moyo wa kuendelea kupenda, ilikuja kutoka ndani ya kutaniko la Kikristo.

Kwa kielelezo, Paulo alifanya kazi kwa bidii sana kwa mwaka mmoja na nusu ili kuanzisha kutaniko katika jiji la Korintho. Maono yake na Wakorintho yalimfanya akuze hisia nyororo kwa ajili ya kundi hilo. Paulo hata alijiita kuwa baba kwao. (1 Wakorintho 4:15) Hata hivyo, licha ya rekodi yake ya upendo na kazi ngumu kwa ajili ya kutaniko hilo, wengine katika Korintho walisema kwa maneno mabaya kuhusu Paulo. (2 Wakorintho 10:10) Kulingana na yote ambayo alikuwa amefanya kwa kujidhabihu, lazima jambo hilo lilimvunja moyo kama nini!

Wale waliokuwa wamepokea upendo wa Paulo wenye ukarimu wangewezaje kuwa wakatili na wenye kukosa heshima jinsi hiyo? Ni lazima Paulo alihisi kana kwamba alikuwa akipasuliwa, kama meli katika tufani. Ingekuwa rahisi kama nini kwake kufa moyo, kuhisi kwamba jitihada zake za wakati uliopita zilikuwa bure, au awe mwenye chuki! Ni nini kilichomfanya Paulo awe mtulivu katika akili? Ni nini kilichomzuia kupasuliwa kwa sababu ya kukata tamaa?

Upendo Unaotushikamanisha

Paulo hakuacha shaka yoyote katika akili za wasomaji wake kuhusu chanzo cha nguvu na kichocheo chake. Yeye aliandika hivi: “Upendo wa Kristo watubidisha.” (2 Wakorintho 5:14) Paulo alitaja chanzo kikuu cha nguvu na kichocheo. Kani yenye kushurutisha ni “upendo wa Kristo.” Msomi fulani wa Biblia alitaja hivi kuhusu andiko hili: “Paulo hasemi kwamba upendo wetu kwa Kristo hutushikamanisha na huduma yetu . . . Hiyo ni nusu tu. Upendo wetu kwa Kristo huwashwa na kukuzwa daima na upendo wake kwetu.”—Italiki ni zetu.

Upendo ambao Kristo alidhihirisha kwa kujitiisha kwa kifo chenye maumivu makali kwenye mti wa mateso—hivyo akitoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kuwa dhabihu ya fidia ili kuokoa wanadamu wote wenye kuamini—kulimhamasisha, kulimshurutisha, na kumlazimisha Paulo kuendelea kutumikia mapendezi ya Kristo na udugu. Hivyo, upendo wa Kristo ulimdhibiti Paulo, ukimzuia kutokuwa na ubinafsi, na kufungia malengo yake kwa utumishi wa Mungu na wanadamu wenzake.

Kwa kweli, chanzo cha kichocheo kwa mwendo mwaminifu wa maisha wa Mkristo ni upendo wa Kristo. Tunapokabiliwa na majaribu yawezayo kutudhoofisha kimwili, kihisia-moyo, na kiroho, kani yenye kushurutisha ya upendo wa Kristo hutuwezesha kuenda hadi kiwango ambacho mtu asiye na kichocheo kingi angekufa moyo. Huo hutupa nguvu ya kuvumilia.

Hatuwezi kutegemea hisia-moyo zetu zisizokamilika zitutegemeze na kutuhamasisha. Hilo ni kweli hasa wakati majaribu yanatokana na kukata tamaa au hangaiko. Kwa upande ule mwingine, upendo wa Kristo una uwezo wa kutushikamanisha kwa huduma yetu, kututegemeza na kutuchochea, licha ya majaribu yetu ya kibinafsi. Upendo wa Kristo humwezesha Mkristo kuvumilia si tu kupita matarajio ya wengine bali labda hata kupita matarajio yake mwenyewe.

Isitoshe, kwa kuwa upendo wa Kristo ni wenye kuvumilia, athari hiyo haikomi. Ni kani yenye kushurutisha ambayo haitikisiki wala kupungua. “Upendo haushindwi kamwe.” (1 Wakorintho 13:8, NW) Hutusaidia kuendelea kumfuata kwa uaminifu, hata nini kitukie.

Majaribu ya kihisia moyo hutokeza kani iwezayo kutupasua. Kwa hivyo, ni muhimu kama nini, kwamba tutafakari juu ya upendo ambao Kristo alituonyesha. Upendo wa Kristo utatushikamanisha pamoja. Upendo wake hufanya iwezekane kuepuka mvunjiko wa meli wa imani yetu. (1 Timotheo 1:14-19) Na zaidi, upendo wa Kristo hutubidisha kufanya yote tuwezayo ili kumtukuza yule aliyefanya wonyesho wa upendo wa Kristo uwezekane, Yehova Mungu.—Warumi 5:6-8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki