Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/01 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Mei 14
  • Juma Linaloanza Mei 21
  • Juma Linaloanza Mei 28
  • Juma Linaloanza Juni 4
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 5/01 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Mei 14

Wimbo 3

Dak. 6: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 9: Una Mipango Gani Katika Miezi ya Mkusanyiko? Mzee au mtumishi wa huduma na familia yake wazungumzia mipango yao ya miezi ya mkusanyiko. Wanazungumza juu ya kuhudhuria vipindi vyote vya mkusanyiko wa wilaya, kufanya upainia msaidizi, na labda kuchukua likizo na kufurahia tafrija. Wote wanakubali kwamba hawangependa kupuuza mambo ya kitheokrasi, kama vile kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kushiriki katika utumishi wa shambani, na kuwa na funzo la Biblia la familia, hata kama watasafiri. Watahakikisha kwamba wanatoa ripoti ya utumishi wa shambani kwa wakati, iwe wako nyumbani au wamesafiri.

Dak. 14: “Mikusanyiko Ni Wakati wa Shangwe!” Hotuba itolewe na mzee. Eleza sababu ya kufanywa kwa mikusanyiko mikubwa ya watu wa Yehova nyakati za Biblia na pia manufaa yake leo. Pindi hizo huandaa ushirika wenye kuimarisha na chakula muhimu cha kiroho. Kazia umuhimu wa kila mtu kuhudhuria siku zote tatu za mkusanyiko wa wilaya.

Dak. 16: “Kupangwa ‘kwa Adabu na kwa Mpango.’”a Zungumzia baadhi ya mipango mingi ambayo lazima ifanywe ili kupanga mkusanyiko. Kazia umuhimu wa kushirikiana kabisa na utaratibu uliowekwa kwa manufaa yetu. Zungumzieni njia ambazo sisi sote twaweza kuonyesha staha ifaayo na kuepuka matatizo yasiyo ya lazima.

Wimbo 31 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 21

Wimbo 52

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 17: “Sikiliza Uongezewe Elimu.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Eleza sababu ambayo mafundisho yanayotolewa kwenye mikusanyiko ni chakula muhimu cha kiroho tunachohitaji. Eleza juu ya wakati mwingi zaidi na jitihada zinazotumiwa ili kuandaa programu kama hiyo. Alika wasikilizaji watoe maelezo ya jinsi ambavyo kila mmoja wao anavyoweza kufanya ili kuhakikisha anapata manufaa kubwa zaidi yeye mwenyewe na wengine pia. Kazia sababu ambazo sisi sote twapaswa kuwa tumeketi kila kipindi kinapoanza.

Dak. 18: “Fanya Mema Usifiwe!”b Eleza sababu ambayo hufanya watu wengi wavutiwe nasi tunapohudhuria mkusanyiko mkubwa. Maelezo yenye kupendeza kutoka kwa watazamaji hutoa pia ushahidi wa Ufalme, lakini maelezo ya kuchambua yanaweza kuwafanya wasivutiwe. Eleza mambo hususa ambayo tunapaswa kufanya ili tuonyeshe kwamba tuna sifa za Kikristo zinazotia ndani kuwahangaikia wengine kikweli.

Wimbo 105 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 28

Wimbo 58

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Mei. Zungumzia “Toa Magazeti kwa Bidii!” Taja jumla ya magazeti yaliyoangushwa na kutaniko mwezi jana. Hiyo yalinganaje na idadi iliyopokewa kutoka kwa Sosaiti? Ikiwa kuna tofauti kubwa, ni nini kinachohitaji kufanywa? Tia moyo waandikishaji wote wasiruhusu maandikisho yao ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yaishe.

Dak. 13: Sanduku la Swali na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 17: “Neno la Mungu. . . . Hukazia Nguvu.”c Tia ndani maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri, yakionyesha jinsi utoaji mfupi waweza kuvuta fikira kwenye Neno la Mungu.

Wimbo 79 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 4

Wimbo 100

Dak. 12: Matangazo ya kwenu na mambo yaliyoonwa ya utumishi wa shambani.

Dak. 15: “Shiriki Kabisa Katika Mavuno.”d Unapozungumzia fungu la 4, tia ndani mfano ulio katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1996, ukurasa wa 19, fungu la 10 kuonyesha vile wengine wanavyofanya ili kupanua huduma yao.

Dak. 18: “Tumehubiri Eneo Letu Mara Nyingi Sana!”e Itolewe na mwangalizi wa utumishi. (Makutaniko yaliyo na eneo lisilohubiriwa mara nyingi yanaweza kuzungumzia makala “Magazeti Yatangaza Ufalme,” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1998.) Zungumzia linaloweza kufanywa ili mhubiri eneo lenu kikamili. Simulia mambo yaliyoonwa yaliyo kwenye 1997 Yearbook, ukurasa wa 204, na Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1996, ukurasa wa 26. Kazia umuhimu wa kuweka maandishi mazuri ya nyumba kwa nyumba, ukirudi kwa wasiokuweko nyumbani, na kufanya ziara za kurudia bila kukawia.

Wimbo 142 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

e Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki