Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/01 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 11
  • Juma Linaloanza Juni 18
  • Juma Linaloanza Juni 25
  • Juma Linaloanza Julai 2
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 6/01 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Juni 11

Wimbo 178

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Mahali inapowezekana, tia moyo kila mtu atazame video Jehovah’s Witnesses Stand Firm Against Nazi Assault anapojitayarisha kwa ajili ya mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Juni 25. Katika juma hilo, mahali ambapo hakuna video makutaniko yatazungumzia makala “Jinsi ya Kupata Tumaini Katikati ya Hali ya Kukata Tumaini” kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1997, ukurasa wa 22-25.

Dak. 15: “Endelea Kufanya ‘Lililo Bora.’” Hotuba ya Kimaandiko yenye kutia moyo, itolewe na mzee.

Dak. 20: “Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako.”a Tia ndani madokezo yafaayo ya jinsi ya kusaidia wapya wasitawishe imani na upendo mioyoni mwao kwa Yehova na Yesu. Tumia mambo makuu kutoka Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1999, ukurasa wa 14, fungu la 18-20.

Wimbo 184 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 18

Wimbo 194

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 10: Kushughulika na Vizuia-Mazungumzo Ambavyo Vyaweza Kutokea. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Zungumzieni “Maelezo” katika kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 15-16. Kuanzia ukurasa wa 16-20, teua vipingamizi fulani ambavyo hupatikana katika eneo lenu. Alika wasikilizaji wasimulie ni majibu gani yenye matokeo kwao na kwa nini.

Dak. 30: “Je, Waweza Kujitolea?” Hotuba yenye kutia moyo ikitia ndani maelezo kutoka kwa wasikilizaji wakijibu maswali yaliyotayarishwa katika fungu la 13 na 18-24. Tia moyo wazazi wasaidie watoto wao wafanye utumishi wa Betheli kuwa kazi-maisha yao. Pendekeza familia zisome nyongeza hii pamoja katika funzo lao la familia.

Wimbo 197 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 25

Wimbo 2

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Zungumzieni toleo la vichapo la Julai na Agosti. Onyesha broshua mbili zilizo akibani kwenu. Panga kuwe na maonyesho yaliyotayarishwa vizuri ya jinsi ya kuzitoa katika huduma. Ili upate madokezo ya utoaji mbalimbali, ona ukurasa wa nyuma wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai na Agosti 1995 hadi matoleo ya 1998. Pia zungumzieni Habari za Kitheokrasi.

Dak. 10: “Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza.” Isomwe na Mwangalizi-Msimamizi.

Dak. 20: “Nasimama Imara! Nasimama Imara! Nasimama Imara!” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji juu ya video Stand Firm, ukitumia maswali yaliyo katika fungu la 2. Kisha zungumzieni fungu la 3-4. Mahali inapofaa, taja tangazo lililo kwenye ukurasa wa 7 juu ya video Stand Firm kwa ajili ya walimu. Malizia kwa kusimulia jambo lililoonwa katika Amkeni!, Novemba 22, 1999, ukurasa wa 31. Mwezi wa Agosti tutazungumzia video The New World Society in Action. Mahali ambapo hakuna video, tayarisha hotuba yenye kichwa “Jinsi ya Kupata Tumaini Katikati ya Hali ya Kukata Tumaini” kutoka kwenye Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1997, ukurasa wa 22-25.

Wimbo 29 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 2

Wimbo 5

Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Juni. Zungumzieni sanduku lenye kichwa “Je, Kuna Vitabu Vyovyote vya Yearbook Ambavyo Huna Katika Maktaba Yako?” Simulia baadhi ya mambo mafupi yaliyoonwa kutoka katika vitabu vya Yearbook vya mwaka wa 1992 na 1994 ili kuonyesha thamani ya vitabu hivyo. Tia moyo wote ambao hawana vitabu hivyo vya Yearbook katika maktaba yao waviagize wakati vingali vyapatikana.

Dak. 15: Vijana—Tumieni Hekima Mnapochagua Kazi-Maisha Yenu. Hii ni sehemu ya kwanza kati ya sehemu tatu za Mkutano wa Utumishi ambazo zitazungumzia kanuni za Kimaandiko zinazohusiana na elimu ya ziada. Vijana wengine Wakristo wanafuatia kazi-maisha za kilimwengu kupitia elimu ya juu, ambazo zinakuwa na matokeo mabaya kwa hali yao ya kiroho. Sehemu hii ni ya mazungumzo kati ya wazazi wawili na mwana au binti yao tineja. Kijana huyo amefikia hatua ambayo anapaswa kufanya uamuzi mkubwa kuhusu miradi yake ya wakati ujao. Ijapokuwa wengine wangependa kufuatia faida za kifedha, umashuhuri, au starehe za maisha, familia hiyo yachunguza Biblia ili kuona inapendekeza nini. (Ona Vijana Huuliza, ukurasa wa 174-175; Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1997, ukurasa wa 21, na Septemba 1, 1999, ukurasa wa 19-21, fungu la 1-3 na 5-6.) Kijana akubali kwamba ni jambo la hekima kufuatia mwendo wa maisha utakaomsaidia kufikia miradi ya kitheokrasi ili kuendeleza masilahi ya Ufalme.

Dak. 17: “Uwe Macho Kutafuta Viziwi Katika Eneo Lenu.”b Uliza wasikilizaji kama wameshakutana na kiziwi yeyote katika eneo la kutaniko lenu. Simulia jambo lililoonwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 1998, ukurasa wa 3, fungu la 7.

Wimbo 32 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki